Alhamisi, 12 Juni 2014

Waziri Kawambwa Afunga Mafunzo ya Maafisa Elimu Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, Mwishoni mwa Wiki amefunga Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu (SLOs) na Maafisa Elimu Taaluma (DAOs) (Msingi Na Sekondari) Tanzania Bara Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu, Yaliyofanyika ADEM - Bagamoyo Kuanzia tarehe 19/05/2014  hadi  06/06/2014.

Mafunzo haya yalishirikisha jumla ya Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu na Maafisa Elimu Taaluma (Msingi na Sekondari) wapatao 636 kutoka Tanzania Bara. Maafisa hawa wanahusika moja kwa moja katika kusimamia utekelezaji wa utoaji Elimu bora nchini katika ngazi ya halmashauri chini ya mkakati mpya wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) katika sekta ya elimu.
Mafunzo haya yatawawezesha kusimamia utoaji wa elimu bora shuleni na pia kutumia mbinu mbalimbali walizojifunza katika kuzuia na kukabiliana na majanga yanapotokea katika maeneo yao. Maafisa hao wataweza kutoa elimu kuhusu majanga kwa walimu, wanafunzi, viongozi na wadau wote wa elimu katika halmashauri zenu. Aidha, Elimu waliyoipata itawawezesha pia kuwa na uwezo wa kusimamia, kufuatilia na kuimarisha miundombinu shuleni na kuchukua hatua za tahadhari zitakayowezesha kukabiliana na majanga, mbalimbali kama vile umuhimu wa milango ya majengo ya shule kufungukia nje, kuwa na vifaa vya kuzima moto na kuwa na visanduku vya huduma ya kwanza.
Shule zetu zimekuwa zikikumbwa na majanga mbalimbali kwa mfano moto, mafuriko na vimbunga. Majanga haya yameleta athari kubwa kwa maisha ya walimu na wanafunzi, katika majengo yakiwemo madarasa, nyumba za walimu, maabara na vyoo.  Samani za shule, vifaa vya kufundishia na kujifunzia, barabara, huduma za maji na umeme, viwanja vya michezo na mazingira yote ya shule yamekuwa yakiharibiwa na majanga. Imeshuhudiwa moto ukiteketeza shule za Sekondari za Shauritanga, Idodi, Morogoro n.k na kusababisha vifo kwa wanafunzi na kuharibika kwa miundo mbinu ya shule. Pia tumeshuhudia mafuriko yakisababisha kutoendelea kwa masomo katika Wilaya za Kilosa, Kyela, Ilala, Mvomero n.k mafuriko haya yalisababisha shughuli za shule kukwama.
Serikali inaamini kuwa baada ya mafunzo haya, washiriki wataweza kutimiza majukumu haya mapya kama ifuatavyo:
  •  kuunda Kamati za kukabiliana na Majanga Shuleni;
  • kuandaa mipango kazi ya kukabiliana na majanga katika ngazi ya halmashauri na shule;
  • kuboresha miundombinu ya shule ikiwemo milango kufungikia nje, kuweka vizima moto (fire extinguishers), ndoo za michanga na kuboresha mazingira ya shule;
  • kujenga uelewa wa pamoja wa namna ya kukabiliana na majanga miongoni mwa walimu, wanafunzi na jumuiya inayozunguka shule
  •  kujenga mtandao (network) wa kukabiliana na majanga kati ya shule na jumuiya inayozunguka shule;
  • kufanya ufuatiliaji na tathmini kuhusu majanga shuleni; nakuandika taarifa sahihi kuhusu uwezekano wa kutokea majanga na madhara ya majanga shuleni mara yanapotokea.


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa akimtunuku Cheti mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu (SLOs) na Maafisa Elimu Taaluma (DAOs) (Msingi Na Sekondari) Tanzania Bara Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa akitoa hotuba ya kufunga Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu (SLOs) na Maafisa Elimu Taaluma (DAOs) (Msingi Na Sekondari) Tanzania Bara Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu;



Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa akimtunuku Cheti mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu (SLOs) na Maafisa Elimu Taaluma (DAOs) (Msingi Na Sekondari) Tanzania Bara Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu;


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa akimtunuku Cheti mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu (SLOs) na Maafisa Elimu Taaluma (DAOs) (Msingi Na Sekondari) Tanzania Bara Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa (mwenye suti nyeusi katikati)  akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Maafisa Elimu Vifaa na Takwimu (SLOs) na Maafisa Elimu Taaluma (DAOs) (Msingi Na Sekondari) Tanzania Bara Kuhusu Kukabiliana na Majanga Katika Taasisi za Elimu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni