Alhamisi, 7 Agosti 2014

MRADI WA KUKUZA STADI KUANZISHWA

Wizara  ya  Elimu na Mafunzo  ya  Ufundi  kwa kushirikiana  na Asasi  za vyuo na  taasisi za Canada wataanzisha Mpango wa kutekeleza mradi  wa  Mafunzo  ya kukuza  stadi kwa ajili ya uajiri (Improving Skills Training for Employment Programme - ISTEP ). Mpango huu utajenga uwezo wa asasi za Mafunzo ya ufundi nchini kufundisha kwa umahiri stadi zinazoitajika katika sekta za uchimbaji wa madini, mafuta, gesi na sekta ya utalii.

Kaimu  Mkurugenzi wa Idara ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas   Katebalirwe  alieleza hayo jijini Dar es Salaam katika warsha   ya makubaliano  na wadau  iliyokuwa  ikijijadili hatua  mbalimbali  katika kujenga  ushirikiano wa jinsi wanafunzi  na tasnia zitakavyofaidika na mpango huu.

Alisema  Mradi  huu  utajikita  katika sekta   za madini, gesi  na utalii, kwamba  utajenga uwezo wa asasi za kitanzania za Mafunzo ya ufundi kufundisha kwa umahiri stadi zinazohitajika katika sekta zote za uchimbaji wa madini, mafuta na gesi na sekta ya utalii, na hivyo kuwapatia vijana takribian 1,200 stadi mwafaka zitakazowawezesha  kujiajiriwa kwenye sekta ya uchimbaji na utalii ama kujiajiri.

“Tayari wataalanu wamefanya   upembuzi   katka  maeneo  mbalimbali  , ili  kupata    mahitaji  ya utekelezaji  wa mradi huo wa miaka  mitano, ambao utagharamia Dola za Canada million  13   na utawanufainisha  watanzania   12,000 hasa  katika  masuala  ya gesi .” alisema Katabalirwe.

Aidha,    alisema  taasisi  11  zitashirikiana katika kukuza uelewa  kwa vijana   kwa kuwa  gesi  ni kitu kipya  kinachohitaji nguvu  kazi  ya kutosha na yenye Mafunzo maalum. Vijana hao watatoka katika taasisi za utalii, Madini na Gesi ambao watapatiwa Mafunzo ya uchimbaji wa madini na uchomeleaji wa mabomba ya gesi.  
Mwenyekiti  kutoka shirikisho  la wachimbaji na watafutaji  wa Madini Tanzania , Nyanda  Shuli  alisema  mpango huo  ni muhimu  katika  kuendeleza  Sekta  ya  Madini    na Nishati  kwa kuwa inahitaji   nguvu kazi  ya kutosha  kukuza  sekta  hiyo.

Alisema   kila mwaka shirikisho  huandaa Mafunzo  kwa kuangalia  mahitaji ya  Sekta  ya  Madini. Alisisitiza kuwa vyuo vilivyosajiliwa   vitanufaika  kutumia  fursa  hiyo  kwani ni  ya kipekee, sekta hiyo inahitaji kufikia lengo la kuchangia pato la Taifa kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2025, kwa kuwa miaka iliyopita ni asilimia 3 pekee iliyotoka katika sekta hiyo.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni