Ijumaa, 10 Oktoba 2014

WAZIRI MKUU AKAGUA UTEKELEZAJI MRADI WA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA ELIMU YA JUU SUA



Waziri Mkuu, Mhe. Kayanza Peter Mizengo Pinda (MB) ametembelea na kukagua Mradi wa  Sayansi, Teknologia na Elimu ya Juu katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine Mkoani Morogoro, na kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo chuoni hapo.

Mhe, Waziri Mkuu amefanya ziara hiyo jana, ambapo alipata nafasi ya kujionea majengo matatu, vifaa vya kisasa vya kujifunzia na kufundishia katika maabara za chuo pamoja na kupata nafasi ya kuongea na wanajumuiya ya chuo wakiwemo waliopata ufadhili wa mafunzo kutoka katika mradi huo.

Mradi wa Sayansi, TeknoloJia na Elimu ya Juu katika  chuo Kikuu cha Sokoine umejenga jengo la ghorofa mbili kwa ajili ya idara ya Uchumi kilimo na biashara, jengo la ghorofa moja katika idara ya uandisi kilimo na Mipango Ardhi. Pia imejenga maabara ya kisasa ya Zoolojia. 

Aidha, mradi umewezesha kuanzishwa kwa mitaala mipya miwili ya Shahada ya Uzamili katika uhakiki wa ubora na Usalama wa Chakula na Mtaala mwingine ni ule wa Uhandisi na Usimamizi wa Uchakataji mazao baada ya kuvunwa.

Makamu Mkuu wa Chuo Bw Gerald Monella, alisema mradi huo umesaidi kupatika kwa ofisi za wahadhiri na wafanyakazi wengine wa Chuo, kufadhili wahadhiri 21 katika mafunzo Uzamili na Uzamivu, ujenzi wa miundombinu ya madarasa na maabara pamoja na ununuzi wa vifaa vya maabara na TEHAMA.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni