Jumatano, 29 Aprili 2015




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI




MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU MWAKA 2015

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inawatangazia wadau wa Elimu na wananchi wote kwa ujumla kuwa Maadhimisho ya Wiki ya Elimu kwa mwaka 2015 yatafanyika kuanzia mwezi April 2015 hadi Mei 2015.
Maadhimisho haya yatafanyika kwa mara ya Pili kitaifa mwaka huu 2015.

Maadhimisho ya Wiki ya Elimu yataanzia katika  ngazi za Halmashauri, Mikoa na baadaye kuhitimishwa kitaifa. Uzinduzi wa maadhimisho hayo kitaifa utafanyika tarehe 11/05/2015 katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma ambapo mgeni Rasmi atakuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda. Kilele cha Maadhimisho kitafanyika tarehe 15/05/2015 katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma ambapo mgeni Rasmi atakuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pamoja na kuongea na wananchi atatoa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi, shule, mikoa na Halmashauri zilizofanya vizuri na zilizoongeza ufaulu kwa kiasi cha Juu katika Mitihani   ya Taifa Darasa la Saba na Kidato cha Nne mwaka 2014.

Maadhimisho ya kitaifa yataenda sambamba na maonesho ya wadau mbalimbali wa elimu yatakayofanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma kuanzia tarehe 11-15/05/2015.
Ili kufanikisha maonesho hayo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inakaribisha wadau wote wa Elimu na Mafunzo kushiriki katika Maadhimisho hayo katika ngazi za Halmashauri, Mikoa na Taifa.

.
Elimu Msingi ni Haki ya Kila Mtoto kwa Maendeleo ya Taifa


IMETOLEWA NA:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
7 Mtaa wa Magogoni,
11479  DAR ES SALAAM.
Tovuti: www.moe.go.tz
19/04/2015

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni