Jumatano, 29 Aprili 2015



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI




MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU MWAKA 2015

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inawatangazia wabunifu wote wa namna ya kutoa elimu kwa njia mbalimbali kuwasilisha andiko la ubunifu wao, ili waweze kushiriki katika maonesho yatakayokwenda sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Elimu itakayoanza tarehe 11- 15 Mei 2015 katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Andiko la ubunifu liwe limewasilishwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo, 7 Mtaa wa Magogoni, 11479 DAR ES SALAAM siku ya Jumamosi tarehe 02/05/2015.



Elimu Msingi ni Haki ya Kila Mtoto kwa Maendeleo ya Taifa


IMETOLEWA NA:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni