Jumanne, 12 Mei 2015

Waziri Mkuu afungua Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Kitaifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Peter Pinda amewataka wazazi na jamii kutambua umuhimu wa watoto kupata elimu na kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanaandikishwa na wanahudhuria bila kukosa hadi kuhitimu elimu ya msingi. Aidha almewataka walimu kufundisha ipasavyo ili elimu itolewayo iwe bora kwa maendeleo ya Taifa.

Waziri Mkuu alisema hayo wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya elimu kitaifa yanayofanyika kwa mara ya pili nchini katika uwanja wa Jamhuri, Mjini Dodoma. Maadhimsho haya yaliyoanza tarehe Mei 11 yanakwenda sambamba na maonesho ya wadau mbalimbali wa Elimu na  yanatarajiwa kuhitimishwa siku ya Ijuma tarehe Mei 15 na Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Aidha, katika ufunguzi huu Mhe. Waziri Mkuu ametoa tuzo kwa Shule, Mikoa na Halmashauri zenye ufaulu uliotukuka na zilizoongeza ufaulu kwa kiwango cha juu katika mitihani 2014 ikilinganisha na matokeo ya 2013. Sambamba na utoaji wa tuzo pia alitoa pikipiki kwa Waratibu Elimu Kata sita waliowakirisha Waratibu Elimu Kata wa nchi nzima

 
 
 



 
 
 
 
 









 

Jumanne, 5 Mei 2015

AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA KKK - CHUO KIKUU CHA DODOMA

Awamu ya pili ya mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu wa shule za Msingi wanaofundisha darasa la I na II yakiendelea katika Chuo Kikuu cha Dodoma ambapo walimu wengine zaidi ya elfu nne wameshiriki kutoka mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Kagera, Katavi, Geita na Mwanza

 Katika awamu ya kwanza mikoa iliyoshiriki ni pamoja na Arusha, Dar es Salaam, Morogoro, Pwani, Rukwa, Ruvuma, Tanga na Singida







.