Jumatatu, 10 Agosti 2015

Serikari yakabidhiwa Shule ya Sekondari

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Dkt. Shukuru Kawambwa amekabidhiwa shule ya sekondari na Balozi wa Korea Kusini Mhe. Chung Il iliyojengwa na Shirika la Good Neighbors International na Washirika wake. Shule hiyo ya sekondari ya Fukayosi imejengwa wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani kwa msaada wa mashirika mbalimbali ikiwemo KOICA kutoka Korea ya Kusini.