Alhamisi, 1 Oktoba 2015

MKUTANO WA KUTATHMINI SEKTA YA ELIMU NCHINI WAFANYIKA


Mkutano wa kutathmini Sekta ya Elimu nchini kwa mwaka 2015 umefanyika jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuanzia tarehe 28 hadi 30 Septemba, 2015 ambapo Wadau mbalimbali wa Elimu ikiwa ni pamoja na Serikali, Washirika wa Maendeleo na Taasisi Zisizokuwa za Serikali zinazojihusisha na Elimu walikutana na kujadiliana kuhusu mafanikio, changamoto na mikakati ya kuboresha elimu nchini.

 Mkutano huo ambao ulifanyika sambamba na Maonesho ya Matumizi ya TEHAMA katika Elimu ya Msingi ulifunguliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome ambae aliwataka washiriki wa mkutano huo kujadili kwa kina namna bora ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika Sekta ya Elimu nchini.









Mkutano huo umefungwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anaeshughulikia Elimu Mhe. Kassimu Majaliwa ambae alisema ushirikiano ulioko kati ya Serikali na Washirika wa Maendeleo unasaidia kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika kuimarisha mahudhurio ya shule, kugharamia Elimu  Msingi  kwa wanafunzi wote, kupatikana kwa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati katika Elimu Msingi.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni