Jumanne, 6 Oktoba 2015

WATAALAM WA ELIMU KUTOKA SWEDEN WAFANYA ZIARA YA KIKAZI NCHINI

 
Wataalam wa Elimu kutoka Sweden ambao ni Wajumbe wa Baraza la Elimu ya Juu nchini humo wameanza ziara ya kikazi nchini  kwa lengo la kujifunza mfumo wa elimu katika ngazi zote, mipango ya maendeleo pamoja na mageuzi mbalimbali ya Elimu.
 
Wataalam hao ni Wakaguzi wawili toka Kitengo cha Elimu ya Juu (Cecilia George na Petra Nord); Wakaguzi wawili kutoka Kitengo cha Elimu ya Sekondari (Eva Neihoff na Isabelle Nilsson); na Mkaguzi mmoja toka katika Kitengo cha Elimu ya Ufundi (Stefan Lofkvist).
 
Ujumbe huo umekutana na kufanya mazungumzo na watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakiongozwa na Kamishna wa  Elimu nchini Prof. Eustella Bhalalusesa aliyemwakilisha Katibu Mkuu. Mazungumzo yao yalijikita zaidi katika kubadilishana uzoefu kuhusu mifumo ya elimu inayotumika katika nchi hizo mbili.
 
Aidha, wataalam hao katika ziara yao iliyoanza tarehe 5 hadi 7 Oktoba, 2015  wanatembelea taasisi zilizo chini ya Wizara zikiwemo; Taasisi ya Elimu Tanzania, Baraza la Mitihani, Tume ya Vyuo Vikuu, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi.  Pia watatembelea shule mbili za sekondari zenye kidato cha tano na cha sita kwa lengo la kuanzisha uhusiano wa kirafiki na shule kama hizo nchini Sweden.









Hakuna maoni:

Chapisha Maoni