Ijumaa, 3 Machi 2017

WAZIRI WA ELIMU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA DFID.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako jana amekutana na kufanya mazungumzo na  washirika wa Maendeleo kutoka nchini Uingereza (DFID)  mjini Dodoma ambapo Kwa pamoja wamekubaliana kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kuboresha Miundombinu katika sekta ya Elimu
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akifurahia jambo na wageni wake ambao ni washirika wa Maendeleo kutoka nchini Uingereza, DFID waliofika katika ofisi za wizara hiyo mkoani Dodoma


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na washirika wa Maendeleo DFID wa nchini Uingereza kwenye ofisi za wizara ya Elimu mkoani Dodoma ambapo Kwa pamoja wamekubaliana kuboresha miundombinu ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu

Waziri wa Elimu akisalimia na wageni wake kabla ya kuanza Kwa mazungumzo yao ambayo yalijikita zaidi katika masuala mbalimbali ya sekta ya Elimu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mabweni ya wasichana Kwa wanafunzi wa vijijini  ili kuwaondolea adha wanafunzi kutembea umbali mref.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni