Ijumaa, 12 Mei 2017

MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA-MOROGORO


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Saimon Msanjila amezindua mkutano wa 24 wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ulioanza leo katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mjini Morogoro ambapo amewaasa watumishi kufanya kazi kwa weledi na maarifa zaidi ili kuleta ufanisi utakaokuwa na tija.

 Profesa Msanjila amesema ili kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu ni lazima watumishi kubadilika na kufanya kazi kwa kujituma na kuachana na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea.

Profesa Msanjila  amesisitiza kuwa wizara ina wajibu wa kuhakikisha nchi inakuwa na elimu bora ili kupata wahitimu na wataalam watakaowezesha nchi kufikia lengo la kuwa na  uchumi wa viwanja.

Aidha, amewataka wajumbe wa mkutano kujielekeza zaidi katika mbinu na mikakati ya utekelezaji kwa kushirikiana na uongozi wa Wizara ili kukamilisha malengo ya mwaka 2016/17 na malengo mapya ya mwaka 2017/18.
 




 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni