Ijumaa, 14 Julai 2017

Naibu Waziri wa Elimu agiza shule zilizotengwa kwa ajili ya elimu maalum kupatiwa mahitaji muhimu


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha shule zilizotengwa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum zinapewa haki zake ikiwa ni pamoja na kupatiwa vifaa vya kufundishia na kujifunzia  ili kuwezesha wanafunzi hao kupata elimu sawa na wanafunzi wengine.

Naibu Waziri Manyanya ametoa agizo hilo alipofanya ziara kwenye shule ya msingi  Sinza Maalum iliyopo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujionea mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji katika shule hiyo, mbapo  pia amezitaka halmashauri hizo kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni yatakayosaidia kupunguza ugumu wa wanafunzi hao kuhudhuri masomo  kutokana na sababu mbalimbali za kimaumbile za watoto hao na hivyo kuwafanya wengine kushindwa kutembea umbali  mrefu kufuata shule.

Pia Naibu waziri alitembelea shule ya sekondari ya Mbweni Teta kukagua ujenzi wa madarasa, mabweni na vyoo unaofanywa na Wizara ya Elimu, Sayasni na Teknolojia Kupitia Programu ya lipa kulingana na matokeo, P4R kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha Tano wanaotarajiwa kuanza shule Julai 17, mwaka huu.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni