Ijumaa, 14 Julai 2017

Naibu Waziri wa Elimu akagua ujenzi na Ukarabati katika shule ya Sekondari Mbweni Tete


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya ameonyesha kutokuridhishwa na hatua ya Halmashauri ya Kinondoni kuhamisha fedha za ujenzi wa madarasa, mabweni na vyoo zilizokuwa zimetolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknlojia kupitia mradi wa lipa kwa matokeo kwa shule ya Sekondari ya Kambwangwa na kupelekwa katika Shule ya sekondari Mbweni tete bila kufuata utaratibu wa kuitaarifu wizara iliyotoa fedha hizo.

Mhandisi Manyanya ameyaeleza hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kuzitembelea shule mbalimbali kwa lengo la kukagua utekelezaji wa ujenzi na ukarabati unaofanywa na Mradi wa Lipa kwa Matokeo (P4R). Amesema kuhamishwa kwa mradi si tatizo lakini kuhamisha bila kutoa taarifa ndo tatizo lilipo kwani wizara imetoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi huo hivyo ni lazima kufanya ufatiliaji ili kuweza kujirizisha kama ujenzi unafanyika lakini wakati najiandaa kwenda Kambagwa ndipo alipotaarifa kuhusu kuhamishwa kwa  mradi huo.

“Leo wakati tunataka kuanza kwenda kuangalia ujenzi ulipofikia lakini tukapewa taarifa kuwa mradi huo haupo Kambangwa na ulihamishwa kupelekwa eneo jingine, hivyo ni muhimu kupeana taarifa maana kuhamishwa kwa mradi kunaleta hoja za ukaguzi” alisisitiza Mhandisi Manyanya.

Naibu Waziri amesema ujenzi wa miundombinu hiyo katika Halmashauri mbali mbali imekuja baada ya wizara ya Elimu kwa kushirikiana na TAMISEMI uwepo wa umuhimu wa kuongeza  miundombinu ya madarasa, mabweni na vyoo katika baadhi ya shule ili kuongeza idadi ya wanafunzi  wanaodahili kwa ajili ya kujiunga na masomo ya kidato cha tano. Amesma lengo la serikali ni kuona wanafunzi wote waliofaulu wanapata nafasi ya kuendelea na masomo yao ya kidato cha tano bila mmoja kuachwa.




Maoni 1 :

  1. Shule nyingi zimezidiwa na idadi ya wanafunzi.
    Lengo liwe kuongeza miundo mbinu bila kuvunja sheria na taratibu tulizojiwekea ili wanafunzi wa Shule za Msingi wasizidi 45 kwenye chumba 01 cha darasa, sekondari kidato cha I-IV wasizidi 40 na kidato cha V-VI wasizidi 30. Tukifanya hivyo tutakuwa sawa.

    Ukubwa wa shule kulingana na usajili uzingatiwe katika kila shule hasa wakati wa mgawo wa wanafunzi wa Kidato cha Kwana na cha Tano. Shule zisipelekewe wanafunzi kama Tahasusi husika haikusajiliwa katika shule hiyo.

    JibuFuta