Alhamisi, 27 Julai 2017

Waziri Mkuu afungua Maonyesho ya 12 ya Vyuo vya Elimu ya Juu


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassimu Majaliwa Majaliwa ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania TCU kuhakikisha programu za masomo zinazoanzishwa na Vyuo vya elimu ya juu nchini zinazingatia mahitaji ya Taifa na soko la ajira.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo katika ufunguzi wa maonyesho ya kumi na mbili (12) ya vyuo vya elimu ya juu yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam ambapo amesema serikali inayathamini maonesho hayo kwa kuwa yanatoa fursa ya vijana kujifunza na kupata taarifa za vyuo na programu wanazoendesha  moja kwa moja

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Saimon Msanjila ameitaka TCU kuhakikisha utaratibu uliotumika kufanya uhakiki wa vyuo na programu na kupelekea baadhi ya vyuo na programu kufungiwa utumike huohuo kuhakiki pindi vitakaporekebisha  mapungufu yaliyojitokeza awali. Aidha, amevitaka vyuo vyote vilivyofungiwa kupeleka TCU majibu ya maeneo  walioambiwa yana mapungufu  kama utaratibu unavyotaka badala ya kuyapeleka Wizarani.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni