Alhamisi, 19 Oktoba 2017

Mradi wa kuwawezesha watoto wa kitanzania kupata elimu wazinduliwa


Kaimu Mkurugenzi mafunzo ya Ualimu Basiliana Mrimi  amezindua mradi wa shilingi milioni 500 utakaosaidia kuimarisha Ufundishaji na ujifunzaji kwenye Chuo cha Ualimu, Patandi kilichopo mkoani Arusha.

Akizundua Mradi huo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mrimi amesema  mradi huo utasaidia Kupima macho watoto wa shule za msingi na kuwapatia vifaa wanafunzi wenye uoni hafifu, Kutoa mafunzo kazini kwa wakufunzi 12 na walimu 4 wa shule za msingi zilizopo kwenye mradi.

Pia mradi huo utasaidia Kusomesha mkufunzi 1 kwa ngazi ya Shahada ya Uzamivu (PhD), Kusomesha wakufunzi 4 kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili (Masters) na kuwa mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano wa Tanzania na Norway.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni