Jumanne, 31 Oktoba 2017

Waziri Ndalichako ashiriki mkutano wa UNESCO, nchini Ufaransa.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni -UNESCO -IRINA BOKOVA amesema Tume hiyo   ina nguvu kwa sababu ya ushirikiano inaoupata kutoka kwa nchi wanachama, hivyo ameziomba  nchi hizo kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Bukova ameyasema hayo hii leo wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa 39 wa UNESCO unaohusiha nchi wanachama duniani kote ambapo amesisitiza pia suala la kudumisha amani, upendo miongoni mwa nchi hizo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako pamoja na Balozi wa Tanzani nchini Ufaransa balozi Samweli Shelukindo wameshiriki mkutano huo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni