Jumanne, 7 Novemba 2017

Naibu Katibu Mkuu Dkt. Semakafu asisitiza umuhimu wa kuboresha Sera na Programu za watot

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Avemaria Semakafu amesema zaidi ya watoto milioni mia mbili duniani hawafikii malengo kutokana na umasikini  na utapiamlo wanaoupata wakiwa katika umri mdogo.

 Dkt. Semakafu ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa kimataifa wa kujadili maendeleo ya makuzi ya watoto na kusisitiza kuwa kupitia mkutano huo wadau wataweza kuboresha sera na kuwa na programu ambazo zitasaidia katika makuuzi ya watoto wa kitanzania.

Kupitia mkutano huo wadau watapata fursa ya kuwa na uelewa wa pamoja, kushirikisha uzoefu kati ya nchi moja na nyingine pamoja na kushawishi wadau kuweka nguvu ya pamoja kwa ajili ya watoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chuo Kikuu Cha Aghakan Tanzania na Taasisi ya IHD Profesa. Kofi Marfo amesema kuwa maendeleo na makuzi ya watoto hutegemea  wazazi, familia na  jamii  kwa ujumla amesisitiza pia suala la  lishe bora kwa watoto, kukua na kuandaa vituo vya afya na hospitali kwa ajili ya upatikanaji wa huduma zilizo bora.

Mkutano huo wa siku tatu umeanza leo na umehusisha nchi ishirini na tano ambapo Tanzania mwenyeji wa Mkutano huo.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni