Alhamisi, 28 Desemba 2017

Waziri Ndalichako afungua vyumba vya madarasa Simiyu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Profesa Joyce Ndalichako amesema serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya kujifunzia na ile ya kufundishia lengo likiwa ni kuhakikisha Elimu bora inatolewa.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo wakati akifungua vyumba viwili vya madarasa vilivyojengwa kupitia Mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (P4R)  katika Shule ya Msingi Mahembe iliyopo Kijiji cha Mahembe kata ya Sawida mkoani Simiyu

Kupitia ziara hiyo  Profesa Ndalichako pia alizungumza na wananchi wa Kijiji cha Habiya kilichopo  Wilaya ya Itilima na kuwataka wazazi kuhakikisha watoto wote waliofika umri wa kwenda shule wanakwenda.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Itilima, Mkoani Simiyu Njalu Silanga amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali za kuboresha miundombinu huku akiwataka wananchi wa Jimbo lake kuitunza miundombinu hiyo kwa faida ya kijiji  hicho.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni