Alhamisi, 18 Januari 2018

TBA yaagizwa kukamilisha ukarabati kabla ya Januari 22

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.  Joyce Ndalichako amewataka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuhakikisha  inakamilisha ukarabati wa shule za Jangwani na Azania kabla ya Januari  22, mwaka huu ili kuwezesha masomo kuanza.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya  kukagua  Maendeleo ya ukarabti wa  shule hizo.

Waziri ndalichako amesema  ameridhishwa na namna  ukarabati wa shule hizo unavyofanyika, licha ya kuwa bado kuna  kazi kubwa ambayo bado haijafanyika. 

Waziri ameitaka TBA kuhakikisha wanakamilisha miundombinu muhimu mapema ikiwemo madarasa, mabweni, na vyoo ili kuwawezesha wanafunzi kuanza masomo  kabla ya januari 22, mwaka huu.


Kwa upande wake Msanifu Majengo Cecilia Muhongo wa TBA amesema wamejipanga kuhakikisha ukarabati wa miundombinu muhimu itakayowawezesha   wanafunzi kuanza masomo inakamilika mapema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni