Jumamosi, 27 Januari 2018

waziri Ndalichako asisitiza michango ya hiari haijakatazwa

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema Serikali haijakataza uchangiaji wa hiari na kuwa kilichokatazwa ni michango ya lazima ambayo imekuwa kero kwa wazazi kwani imekuwa kama kiingilio, ambapo mtoto haruhusiwi kuingia shuleni kabla mzazi hajalipa michango hiyo.

Waziri Ndalichako amesema Serikali haizuii wananchi kwa hiari yao wenyewe kuchangia Maendeleo ya Elimu ya watoto wao iwapo michango itakusanywa kwa utaratibu uliowekwa na kuratibiwa na mmoja wa wazazi na siyo mkuu wa shule.

Waziri Ndalichako ametoa kaui hiyo mjini Makambako mkoani Njombe wakati akishiriki uzinduzi wa kampeni ya upimaji wa kansa ya matiti na mlango wa kizazi, kifua kikuu na magonjwa mengine yasiyoambukiza kampeni ambayo iliratibiwa na mkoa huo wa Njombe.

Akikagua ujenzi wa mabweni unaoendelea katika shule ya sekondari Sovi iliyopo mkoani Njombe Waziri Ndalichako amekiri kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa mabweni hayo ambapo aliwasifu wananchi kwa kazi nzuri inayofanywa na viongozi wao wa mkoa.

Waziri Ndalichako amewataka wananchi kuendelea na moyo wa kuchangia Ujenzi huo na kamwe wasikatishwe tamaa na uvumi uliopo kuwa hawaruhusiwi kuchangia maendeleo yao ya Elimu ya watoto wao.

Akiwa Wilayani Makete Waziri Ndalichako aliamrisha kusimamishwa Ujenzi wa chuo cha ufundi stadi VETA kwa kuwa gharama zilizotajwa zipo juu sana na hazina uhalisia, ambapo amemuagiza Meneja wa VETA wa kanda kwa kushirikiana na mhandisi wa Halmashauri asimamie ili gharama hizo ziangaliwe upya.

Waziri Ndalichako alisikitishwa kuona ujenzi haujaanza mpaka sasa japo kuwa mkataba wa kazi hiyo ulisainiwa Agosti, 2017 na kazi ya Ujenzi kukabidhiwa kwa Mkandarasi ambaye ni Wakala Wa Majengo - TBA Oktoba 2017.

Pia Waziri Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dk. Leonrd Akwilapo kutuma Mkaguzi ili afuatile matumizi ya fedha ya mradi huo.





Maoni 2 :

  1. Magnumax Middle aged bodybuilders should take meals and nutritional supplements as a part of the plan. Cut fast foods. Building the muscles requires protein carbs and nutrients. Need to know have to meals just a day . http://jackedmuscleextremeadvice.com/magnumax/

    JibuFuta
  2. MagnuMax How it works: As we've talked about right before, ingesting for max muscle mass development will involve generally getting enough energy and protein. There you might have it; all the things you need to know about creating muscle mass. An all-time beloved of bodybuilder all over the world for making biceps mass.
    http://www.healthmegamart.com/magnumax/

    JibuFuta