Ijumaa, 9 Machi 2018

Ndalichako awataka Wanawake kufanya kazi kwa bidii


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amewataka Wanawake nchini kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuonyesha Thamani ya Mwanamke katika jamii na Taifa kwa ujumla.

 Waziri Ndalichako amesema bidii pekee katika shughuli mbalimbali za kujiletea Maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla ndiyo itaonyesha mchango wa Mwanamke na kumfanya athaminiwe na kumuwezesha kupata nafasi kubwa na nzuri zaidi za kutumikia Taifa ikiwa ni pamoja na kufuta dhana potofu ya kuwa Mwanamke hawezi.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Jukwaa la Akademia katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani shughuli ambayo  imefanyika jijini Dar es salaam.

Waziri Ndalichako amesema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyoandaliwa na  Taasisi ya Akademia ya Sayansi Tanzania walati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ili kujadili mchango wa Mwanamke katika kuleta Maendeleo Endelevu ambalo limeshirikisha Wanawake na Wadau wengine kutoka nchi mbalimbali.

Kwa upande wake Spika Mstaafu Anne Makinda amesema wanawake wanapaswa kuhakikisha wanapata Elimu ambayo itawawezesha kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuwa na uthubutu wa kufanya shughuli ambazo wanaamini watazifanya kwa umakini ili kuonyesha uwezo walionao katika jamii inayowazunguka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni