Ijumaa, 9 Machi 2018


Ole Nasha apiga  marufuku Wanafunzi wa Shule kunyimwa vyeti kwa kutokamilisha michango
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amepiga Marufuku Wanafunzi kunyimwa vyeti pindi wanapomaliza shule kwa madai ya kutokamilisha michango pindi walipokuwa wanasoma.

 Naibu Waziri Ole Nasha ametoa agizo hilo mkoani Tabora alipokutana na Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari kuzungumzia namna ambavyo wanapaswa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John PombeMagufuli la kukataza michango shuleni kwa kuwa Serikali inagharamia ElimuMsingi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa William Ole Nasha akikagua Vifaa vyama Maabara katika Chuo cha UalimuTabora kilichopo Manispaa ya Tabora Mkoani humo.

Naibu Waziri huyo amesema Magufuli hajakataza uchangiaji wahiari isipokuwa amekataza michango holela ambayo ilikuwa ikichangishwa bila utaratibu na kumzuia Mwanafunzi kuendelea na masomo kwa madai kuwa hajachanga mchango wa aina fulani.

 ‘Waraka wa Elimu Namba 6 wa mwaka 2016 unaeleza wazi namna Elimu bila malipo itakavyotekelezwa na nijukumu la mzazi kwa mtoto wake hivyo ni marufuku Mwanafunzi kubakizwa nyumbani au kutopewa cheti chake anapomaliza Shule kwa madai kuwa hajakamilisha mchango fulani’.amesema Ole Nasha

Pia ametoa rai kwa walimu wote nchini kujielekeza kwenye jukumu lao la msingi la kufundisha badala ya kujihusisha na uchangishaji wa mchango wa aina yoyote na kwamba michango yote ya hiari itaratibiwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri husika kupitia watendaji wake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni