Jumanne, 27 Machi 2018

Wizara ya Elimu yawasilisha Taarifa ya Utekelezaji, Makadirio ya Bajeti kwa mwaka 2018/19 kwa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imewasilisha Taarifa ya Utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2017/18 na Makadirio ya Bajeti kwa mwaka 2018/19 kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Uwasilishaji wa taarifa hiyo umefanyika leo katika ofisi za Bunge zilizopo Mkoani Dodoma ambapo wajumbe wa Kamati hiyo wamepata fursa ya kupitia na kujadili Fungu 46. 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Pro.Joyce Ndalichako  akifafanua jambo wakati wa uwasilishaji wa Taarifa ya Utekelezaji  2017/18 na Makadirio ya Bajeti kwa Mwaka 2018/19 kwenye Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.


Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Juma Nkamia akisitiza jambo wakati wa uwasilishaji wa Taarifa ya utekelezaji na Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka 2018/19 Mkoani Dodoma.

Wajumbe wa Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakifuatilia kwa makini uwasilishaji wa Taarifa ya utekelezaji na Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka 2018/19.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni