Jumanne, 24 Aprili 2018

NAIBU WAZIRI OLE NASHA AFUNGA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI


·        ASISITIZA UWAJIBIKAJI MAHALI PA KAZI


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amewataka Wafanyakazi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa kufuata kanuni, taratibu  ikiwa ni pamoja na kuwa na ushirikiano miongoni mwao ili kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Mkutano huo wa siku mbili umehitimishwa leo  Mkoani Morogoro.

Naibu Waziri huyo ametoa kauli hiyo wakati akifunga mkutano wa 25 wa baraza la wafanyakazi ambapo amesisitiza kuwa mkutano huo upo kisheria na kuwa unasaidia kuainisha haki za Wafanyakazi pamoja na Wajibu wao katika utumishi wa Umma.
Viongozi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakiwa wameshikana mikono kuonesha umoja wao wakati wa  kufunga Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mkoani Morogoro.

Mheshimiwa Ole Nasha amewataka Wafanyakazi hao kuhakikisha Elimu inayotolewa hapa nchini inakuwa bora kwa kuwa Elimu ndiyo msingi pekee wa kufikia Uchumi wa viwanda.
Wajumbe wa Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara  wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wakati wa kufunga Mkutano wa baraza la Wafanyakazi mkoani Mkoani Morogoro.

Pia amewataka makatibu wakuu wa Wizara hiyo kushughulikia kikamilifu maazimio yote yalifikiwa katika mkutano huo wa siku mbili wa baraza la Wafanyakazi kabla ya kufanyika kwa mkutano mwingine wa baraza hilo unaotarajiwa kufanyika mapema Oktoba mwaka huu.


Kauli mbiu ya mkutano wa baraza hilo inasema: “Elimu Jumuishi, Sayansi na Teknolojia ni msingi wa Maendeleo, Endelevu ya Uchumi wa viwanda Tanzania.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akizungumza na wajumbe wa mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (hawapo pichani), wakati wa kufunga mkutano huo uliofanyika Mkoani Morogoro amabye amesisitiza kuwa jukumu la Wizara hiyo ni kuweka viwango vya ubora vya Elimu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni