Jumanne, 29 Mei 2018

PROFESA MDOE ASHIRIKI KONGAMANO LA SAYANSI NA TEKNOLOJIA NCHINI ISRAEL


Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe yuko mjini Jerusalem nchini Israel, kwa ajili ya kushiriki kongamano la Mawaziri la kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia katika kuhudumia wanadamu.

Mkutano huo ulioanza jana ulifungukiwa rasmi na Waziri Mkuu wa Israel ambapo Mada kuu ya mkutano huo ni “kufikiria nje ya boksi”.
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Israel wakati wa kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia.

Kongamano hilo la siku 4 linawashirikisha Mawaziri, Naibu Mawaziri na viongozi mbalimbali.
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wengine wa kongamano la Mawaziri la kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia katika kuhudumia wanadamu nchini Israel.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni