Jumamosi, 19 Mei 2018

WANAFUNZI WA CHIDYA WAIPONGEZA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MAJI.


Wanafunzi wa shule ya Sekondari Chidya iliyopo Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara wameipongeza serikali kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo pamoja na kuchimba kisima ambacho kimewapungizia adha ya upatikanaji wa Maji kwa urahisi.

Wanafunzi hao wametoa kauli hiyo wakati walipofanya mahojiano na waandishi wa habari kufuatia ziara ya ufuatiliaji wa uboreshaji wa miundombinu ya shule na ujifunzaji na ufundishaji wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu - KKK.

 Wanafunzi hao wamesema mwanzoni miundombinu ilikuwa imechakaa pia walikuwa wanafuata Maji umbali takribani kilometa moja na pia iliwalazimu kila siku kuamka alfajiri ili kufuatilia Maji hivyo iliwafanya wachoke na hata kupunguza morali ya kusoma.

 Jengo la Utawala lililokarabatiwa katika Shule ya Sekondari Chidya Wilayani Masasi Mkoani Mtwara.

“Kwa kweli hili la Maji wanafunzi lilikuwa linakera sana maana inatulazimu kuamka kila siku alfajiri kufuatilia maji na kisha kujindaa kuelekea shuleni kwa ajili ya masomo, kwa kweli hii ilikuwa inatuchosha na pia ilikuwa ni hatari kwa sababu tulikuwa tunakutana na wadudu wabaya kama vile nyoka,” anasema mmoja wa wanafunzi hao Saidi Mnguvu.

 “Nakumbuka tulikuwa tunatolewa darasani kwa ajili ya kuafuatilia maji, hata vipindi wakati mwingine vilikuwa vinakatishwa ili tuweze kwenda kufuata Maji sasa adha hii ya Maji kwa kweli imeisha na sasa tunaishi kwa raha na tunapata Maji muda wote,” anasema Mnguvu.
Muonekano wa vyumba vya madarasa vilivyojengwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) katika Shule ya Sekondari Chidya iliyopo Wilayani Masasi Mkoani Mtwara. 


 Mkuu wa shule hiyo ya Sekondari ya Chidya Zawadi Mdimbe ali
sema shule hiyo ilipokea zaidi ya milioni Mia mbili kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa kulingana na matokeo yaani (EP4R) ambazo zimetumika kukarabati Miundombinu ya vyumba vya madarasa, ujenzi wa Nyumba za walimu, kuboresha miundombinu ya Maji, bwalo, Jiko pamoja na kukarabati ofisi za walimu za shule hiyo.
Muonekano wa majengo mawili yenye vyumba vya madarasa vilivyokarabatiwa katika Shule ya Sekondari Chidya Wilayani Masasi Mkoani Mtwara.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni