Jumatano, 9 Mei 2018

WAZIRI NDALICHAKO: MAABARA YA KISASA INAYOJENGWA TANZANIA KUDHIIBTI MIONZI NCHI ZA AFRIKA.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako Leo ametembelea na kukagua hatua za mwisho za usimikaji wa vifaa mbalimbali ndani ya maabara ya kisasa ya Kuhakiki vifaa vinavyopima mionzi katika Tume ya nguvu za Atomiki- TAEC iliyopo mkoani Arusha.

Akizungumza mara baada ya kutembelea maabara hiyo Waziri Ndalichako amesema serikali imejenga maabara hiyo ya kisasa ili kudhibiti masuala ya mionzi kwa nchi za Afrika.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipokea maelezo kuhusu usimikaji wa vifaa vya kisasa katika maabara ya nyuklia kwenye Tume ya nguvu za Atomiki iliyoko mkoani Arusha.

Alisema maabara hiyo ambayo sasa ipo katika hatua za kufungwa vifaa mbalimbali vya kisasa itawezesha nchi mbalimbali kuja kujifunza namna ya kupima masuala mbalimbali ya mionzi.

Waziri Ndalichako amesema kuwa hadi sasa serikali imeshatoa kiasi cha sh. bilioni 2.38 huku Umoja wa Ulaya (EU) ikitoa vifaa vyenye thamani ya sh.  bilioni 11.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiangalia kwa karibu moja ya kifaa kilichosimikwa kwa ajili ya upimaji wa mionzi kwenye maabara ya kisasa ya nyuklia kwenye Tume ya nguvu za Atomiki, TAEC mkoani Arusha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni