Jumanne, 3 Julai 2018

NAIBU WAZIRI OLE NASHA: VYUO VYA UFUNDI VINAMUANDAA KIJANA KUJIAJIRI NA KUAJIRIWA


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknlojia Mheshimiwa William Ole Nasha amewataka vijana kuachana na dhana ya kuwa ili kufanikiwa katika maisha lazima uwe umesoma hadi chuo Kikuu lakini ukweli ni kuwa vyuo vya ufundi  vinamuandaa kijana kuwa na uwezo wa kujiajiri na pia kuajiriwa ndani na nje ya nchi.

Naibu Waziri Ole Nasha ameyasema hayo wakati alipotembelea Baadhi ya Taasisi zilizochini ya Wizara hiyo ambazo zinashiriki maonesho ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknlojia Mheshimiwa William Ole Nasha akisikiliza maelezo ya jinsi mtambo wa kusaidia kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi kutoka kwa mmoja wa mwanafunzi wa VETA Moshi alipotembelea Baadhi ya Taasisi zilizochini ya Wizara hiyo ambazo zinashiriki maonesho ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.


Mheshimiwa Ole Nasha amewahakikishia Watanzania kuwa Elimu inayotolewa hapa nchini ina viwango vya ubora unaokubalija na ndiyo maana  vijana wengi wanaajiriwa nje ya nchi  kutokana na kile wanachokuwa wamekisomea.

Naibu Waziri ameleza kuwa serikali ya awamu ya Tano imeboresha Mazingira ya kujifunzia na kufundishia katika vyuo vya Ufundi kwa kununua mitambo na vifaa vya kisasa ili kuimarisha mafunzo yanayotolewa na vyuo hivyo.

“ Uwekezaji huu mkubwa unalenga kuhakikisha vijana wanaohitimu katika vyuo vya Ufundi nchini wanakidhi soko la ajira la ndani na nje y nchi,”amesema Mheshimiwa Ole Nasha.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknlojia Mheshimiwa William Ole Nasha akiwa katika banda la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati alipotembelea maonesho ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Taasisi zinazoshiriki Mamlaka ya Ufundi stadi- VETA, CHUO Kikuu Cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu Cha Mzumbe, Taasisi ya Teknolojia-DIT, Baraza la Ufundi la Taifa-NACTE, Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS  na Tume ya nguvu za Atomiki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni