Jumanne, 4 Septemba 2018

RAIS MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA CHUO CHA UALIMU MURUTUNGURU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt John Magufuli leo ameweka jiwe la msingi kwa ajili ya upanuzi wa Chuo Cha Ualimu Murutunguru, kilichopo Wilayani Ukerewe mkoani Mwanza.

Rais Magufuli amesema Chuo Cha Murutunguru kwa sasa walimu wanaohitimu ni ngazi ya cheti, lengo la serikali ni kianze kutoa ngazi ya Diploma na baadae kikiongezewa miundombinu kiweze kutoa shahada.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli akiweka Jiwe la Msingi katika Chuo cha Ualimu Murutunguru Wilayani Ukerewe mkoani Mwanza ambapo amewapongeza Viongozi wa Wizara ya Elimu kwa kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa na Wizara hiyo.

Rais Magfuli pia amewapongeza Viongozi wa Wizara ya Elimu kwa kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa na Wizara hiyo.

Pia Rais amewashukuru  washirika wa Maendeleo hususan nchi ya Uingereza kwa kuendelea kufadhili miradi ya Elimu.
Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakishuhudia uwekaji wa jiwe la Msingi kwa ajili ya upanuzi wa Chuo cha Ualimu Murutunguru kilichopo Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza. 

Upanuzi wa ujenzi wa Chuo hicho unahusisha jengo la Utawala, vyumba vya madarasa, bwalo la Chakula, hosteli za wanafunzi, jengo maalumu la kupokelea umeme na ujenzi wa mifumo ya Maji na umeme.
Muda mfupi baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako kumpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli kwa ajili ya kuweka Jiwe la Msingi la upanuzi wa Chuo cha Ualimu Murutunguru. 

Ujenzi huo utagharimu takriban bilioni mbili nukta Tatu na inatarajia kukamilika oktoba mwaka huu.
Muonekano wa vyumba vya madarasa katika Chuo cha Ualimu Murutunguru, ambapo leo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi ambalo linahusisha ujenzi wa Jengo la utawala, bwalo la chakula, hosteli za wanafunzi, jengo maalum la kupokelea umeme na ujenzi wa mifumo ya maji na umeme.  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni