Jumatano, 27 Februari 2019

WAZIRI NDALICHAKO ARIDHISHWA NA HATUA ZA UJENZI OFISI ZA WIZARA YA ELIMU KATIKA MJI WA SERIKALI IHUMWA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako leo ametembelea na kukagua hatua ya ujenzi wa ofisi mpya za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zinazojengwa kwenye Mji wa serikali Ihumwa, mkoani Dodoma na kusema kuwa ameridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikagua ujenzi wa ofisi za wizara anayoiongoza zinazojengwa katika mji wa serikali uliopo eneo la Ihumwa jijini Dodoma.

Waziri Ndalichako amesema kukamilika kwa ofisi hizo utasaidia utendaji kazi kuimarika kwa kuwa mazingira ya kufanyia kazi yanakuwa ni mazuri zaidi.

“Ofisi kwa ujumla ni nzuri zimejengwa vizuri naamini hata watumishi watakuwa na ari ya kufanya kazi kwa kuwa mazingira yatakuwa bora zaidi.” alisema  Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipata taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi za wizara kutoka kwa Msimamizi wa Ujenzi, Kamishna Msaidizi Aron Lunyungu kutoka Shirika la Magereza.

Waziri Ndalichako pia  amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Leonard Akwilapo kuhakikisha anasimamia kwa ukaribu ujenzi wa jengo pacha la wizara ili liweze kukamilika kwa wakati.

Naye Msimamizi wa ujenzi huo Kamishna Msaidizi Aron Lunyungu kutoka Shirika la Magereza amesema ujenzi umefikia katika hatua ya ukamilishaji na kwamba wanatarajia kukabidhi Jengo la Wizara baada ya wiki mbili kuanzi leo.

Ujenzi wa jengo la Ofisi za Wizara ya Elimu, Sayansi naTeknolojia katika mji mpya wa serikali ulianza Desemba 10, 2018.
 
Muonekano wa hatua ya ujenzi wa ofisi za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zinazojengwa katika mji wa Serikali uliopo eneo la Ihumwa jijini Dodoma.

SERIKALI YA TANZANIA NA ILE YA SUDAN KUSINI KUSHIRIKIANA KATIKA ELIMU

Serikali ya Tanzania na ile ya Sudan Kusini zimetiliana saini makubaliano ya ushirikiano katika sekta ya elimu ambapo wanafunzi wa Sudan Kusini watajifunza lugha ya Kiswahili lakini pia nchi ya Tanzania itapeleka walimu wa lugha ya Kiswahili Sudan Kusini pamoja na kubadilishana uzoefu na ujuzi kati ya nchi hizi mbili.

Makubaliano hayo yamefanyika mkoani Dodoma ambapo kwa upande wa Tanzania Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ndiye aliyetia saini makubaliano hayo huku nchi ya Sudan Kusini ikiwakilishwa na Waziri wa Elimu wa nchi hiyo Deng Deng Hoc Yai.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako (Tanzania) na Waziri wa Elimu Deng Deng Hoc (Sudan Kusini) wakitiliana saini makubaliano ya kushirikiana katika masuala mbalimbali yahusuyo Elimu katika nchi hizi mbili. 

Waziri Ndalichako amesema makubaliano yanalenga kufungua fursa katika nchi hizo mbili, na kuwa Tanzania iko tayari kuhakikisha inaisaidia nchi ya Sudan Kusini kufikia malengo waliyojiwekea.

“Tukio hili ni muhimu, ambapo nchi ya Sudan Kusini wameomba ushirikiano katika sekta ya Elimu na kuwa Tanzania tunaihakikishia nchi  hiyo ushirikiano kwa kuchapisha vitabu vya somo la Kiswahili, Tanzania pia iko tayari  kwa walimu wa Kiswahili kwenda Sudan kufundisha somo hilo pia nchi hizo mbili zitaweza kubadilishana uzoefu katika eneo la mafunzo ya ufundi stadi," alisema Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako (Tanzania) na Waziri wa Elimu (Sudan Kusini) Deng Deng Hoc wakionesha mkataba wa makubaliano unaohusu ushirikiano katika sekta ya elimu ambapo wote kwa pamoja wamekubaliana kuendelea kudumisha umoja na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu wa Sudan Kusini Deng Deng Hoc Yai ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kudumisha umoja na ushirikiano kati ya nchi hizi mbili huku akisisitiza kuwa Tanzania ni nyumbani.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa hafla ya utilianaji saini wa makubaliano ya mashirikiano katika masuala mbalimbali yahusuyo elimu. Amesema makubaliano hayo yanalenga kufungua fursa kwenye sekta ya elimu katika nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu na ujuzi.

Waziri Deng Deng amesema kwa sasa Kiswahili ni miongoni mwa lugha zinazoweza kushindanishwa na lugha nyingine za kimataifa kama vile Kingereza na  Kiarabu hivyo nchi hiyo imeona umuhimu kwa shule zao kuanza kufundisha lugha ya kiswahili shuleni.

Waziri wa Elimu Tanzania na Waziri wa Elimu Sudan Kusini wakifurahia jambo baada ya  kutiliana saini makubaliano ya ushirikiano katika masuala mbalimbali  kwenye sekta ya elimu.

Ijumaa, 15 Februari 2019

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI YA KUZUIA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI

Serikali imesema inaendelea na mkakati wa kujenga mabweni katika shule mbalimbali za Sekondari hapa nchini ambazo ni za kutwa ili kuepusha watoto wa kike kupata mimba pamoja na kuzuia ndoa za utotoni.

Kauli ya Serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania wenye lengo la kuzuia ndoa za utotoni uliofanyika Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Wiliam Ole Nasha akizungumza na wadau wa Elimu (Hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania wenye lengo la kuzuia ndoa za utotoni Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri huyo amesema tatizo la ndoa za utotoni ni kubwa katika nchi nyingi hali ambayo inasababisha watoto wa kike kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu na kusababisha Taifa  kukosa wataalamu.

“Ndoa za utotoni zinafanya mtoto wa kike asisonge mbele katika safari yake ya elimu  na ndio maana serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali   kuhakikisha tunazuia ndoa za utotoni na kuweka mazingira wezeshi ya kuwafanya watoto wa kike waendelee kubaki shuleni kupata elimu,” alisema Mhe. Ole Nasha.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi wa wadau wa elimu waliohudhuria mkutano wa mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania.

Akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu zinashirikiana kuhakikisha shule za msingi na sekondari zinakuwa na Walimu ambao watasaidia kutoa ushauri nasaha kwa wanafunzi kufahamu namna ya kujizuia kuingia katika  ndoa na mimba za utotoni.

Mradi wa Girls Inspire Tanzania una lenga kuzuia ndoa za utotoni unatekelezwa katika nchi za Tanzania, Msumbiji, Bangladesh, India na Pakistani na kufadhiliwa na na serikali za Canada na Australia ambapo kwa Tanzania umatekelezwa na Taasisi ya Elimu ya Watu wazima na Shirika lisolo la Serikali Kiota Women Health and Development, (KIHOWEDE).

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akiwa na  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Balozi wa Canada O’Donnell na Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Tanzania Dkt. Naomi Katunzi wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wa katika mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania.

WAZIRI NDALICHAKO AAHIDI USHIRIKIANO MAANDALIZI YA ZANZIBAR JAMBO REE


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ambaye pia ndiye  Rais wa Skauti Profesa Joyce Ndalichako amewaahidi ushirikiano Viongozi wa Chama cha Skauti Tanzania katika kufanya maandalizi ya sherehe za  Zanzibar Jambo Ree inayotarajiwa kufanyika mwezi wa sita mwaka huu Visiwani Zanzibar..

Waziri Ndalichako amesema hayo wakati alipokutana na kuzungumza na Viongozi wa  Juu wa Skauti Tanzania kwa lengo la kumuelezea  Waziri hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya sherehe hizo.

Waziri Ndalichako amewaambia viongozi hao wa skauti kuwa ni vyema wakaliangalia kwa makini pendekezo lao la kutaka kupeleka washiriki 24 Visiwani Zanzibar kutoka kila mkoa wa Tanzania bara kwani namba hiyo itakuwa ni kubwa, na kuzifanya sherehe hizo kuonekana ni za Bara badala ya Zanzibar.


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Skauti Mkuu Mwantumu Mahizi na Kamishana Mkuu Grace Joseph jijini Dar es salaam ambapo Waziri amewaahidi viongozi wa skauti ushirikiano katika maaandalizi ya Sherehe za Jambo Ree zinazotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar.



 “Ninawashauri kuangalia kwa undani na makini suala la idadi ya washiriki kutoka Bara kwa kila mkoa washiriki 24, idadi hii ni kubwa na tutawazidi kwa kuwa Zanzibar  ina mikoa michache kuliko sisi na sherehe hizi zitaonekana kuwa ni za Bara na si Zanzibar,” alisema Waziri.

Skauti Mkuu Mwantumu Mahiza alimwelezea Waziri kuwa Chama cha Skauti Tanzania kinatekeleza agizo la Makamu wa Rais alilolitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Skauti Dunia na Maadhimisho ya miaka mia moja ya Skauti hapa nchini ya kukitaka chama hicho kufanya sherehe  hizo Visiwani Zanzibar.

Mahiza pia alimtambulisha Kamishna Mkuu mpya Grace Joseph Kado aliyeteuliwa hivi karibuni na kueleza kuwa sasa safu ya uongozi  kwa sasa imekamilika.
Skauti Mkuu Mwantumu Mahizi akisisitiza jambo kwa Rais wa Skauti Tanzania ambaye pia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa kujadiliana kuhusu maandalizi ya sherehe za Jambo Ree zinazotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar.

Jumatano, 13 Februari 2019


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

STUDY OPPORTUNITY TENABLE IN THE REPUBLIC OF KOREA FOR ACADEMIC YEAR 2019-2021
1.0 Call for Application
The general Public is hereby informed that, the National Institute for International Education (NIIED) under the Ministry of Education of the Republic of Korea is offering Graduate study opportunity to a Tanzanian citizen for  the academic year 2019 Global Korea Scholarship: Korean Government Scholarship Program for International Students for a Graduate Degree (2019 Graduate GKS).

2.0 Mode of Application
All applicants are required to complete application form and attach all requested documents. Instructions for this Scholarship are obtained in the following website http://www.studyinkorea.go.kr.

Application forms and attached documents should be submitted to the Korean Embassy not later than 7th March, 2019
PHYSICAL ADDRESS
19TH Floor Golden Jubilee Tower,
Ohio Street, City Centre,
P. O. Box 1154,
DAR ES SALAAM.




Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business Studies and Law,
University of Dodoma (UDOM) Building No. 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

STUDY OPPORTUNITY TENABLE IN THE THAILAND FOR ACADEMIC YEAR 2019-2020
1.0 Call for Application
The general Public is hereby informed that, the Thailand International Cooperation Agency (TICA) announces scholarships for Master’s degree under the Thailand International Postgraduate Programme (TIPP) for the academic year 2019.

2.0 Mode of Application
The application and the corresponding application documents should be submitted to application receiving agency, the Permanent Secretary, Ministry of Education, Science and Technology. For more information, please visit the following link: http://tica.thaigov.net/main/en/  and an application form is found in the following link: http://www.tica.thaigov.net/main/en/relation/75500-TIPP-Application-form.html

Eligibility criteria for candidates and required documents are as per the applied programme. For more information please visit the following link: http://tica.thaigov.net/main/en/relation/99237-TIPP-2019.html.

Note that: late or incomplete applications/documents will not be considered.

Deadline for receiving application forms is on 15th March, 2019.


Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business Studies and Law,
University of Dodoma (UDOM) Building No. 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.