Ijumaa, 26 Aprili 2019

WAZIRI NDALICHAKO AIPONGEZA CHINA KWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameipongeza Jamhuri ya Watu wa China kwa kuimarisha ushirikiano  na  Tanzania hususan katika sekta za Elimu, Biashara na Ujenzi wa miundombinu.

Waziri Ndalichako ametoa pongezi hizo wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na China ambapo amesema kuwa mahusiano kati ya nchi hizo mbili ni ya muda mrefu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza katika sherehe za kuadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Watu wa China na Jamhri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Prof. Ndalichako amesema mchango wa nchi hiyo kwenye maendeleo ya Tanzania ni dhahiri akitolea mfano  wa ujenzi wa Reli ya TAZARA pamoja na ujenzi wa viwanda mbalimbali vya nguo nchini.

Prof. Ndalichako amesema pia China imeendelea kushirikiana na Tanzania kwenye Sekta ya Afya kwa kubadilishana uzoefu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China, Wag Ke (Hayupo pichani) katika sherehe za kuadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya China na Tanzania.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo  Pinda, Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bw. Caesar Waitara, na viongozi mbalimbali kutoka Taasisi  za umma na binafsi nchini. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni