Jumatatu, 19 Agosti 2019

WAZIRI NDALICHAKO AWAASA WANAFUNZI WALIOPATA UFADHILI WA MASOMO YA ELIMU YA JUU NCHINI CHINA KUWA MABALOZI WAZURI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amewaasa wanafunzi waliopata ufadhili wa masomo ya Elimu ya juu nchini China kuwa mabalozi wazuri wa Tanzania nchini humo.


Waziri Ndalichako amesema hayo Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi hao iliyofanyika katika ofisi za ubalozi wa China nchini.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi waliopata ufadhili wa masomo nchini China. Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Ubalozi wa China Jijini Dar es Salaam.
Jumla ya wanafanzi 61 wamepata ufadhili wa masomo kwa Shahada za  Uzamili na Uzamivu katika fani za Afya, Uhandisi, Utabibu , TEHAMA na Mazingira.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na baadhi ya wanafunzi waliopata ufadhili wa masomo nchini China wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi hao iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiteta jambo na Balozi wa China nchini Wang Ke.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi Balozi wa China nchini Wang Ke zawadi ya picha inayoonesha baadhi ya wanyama wanaopatikana katika hifadhi za Tanzania.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa China nchini Tanzania pamoja na wanafunzi waliopata ufadhili wa masomo nchini China.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni