Jumanne, 12 Mei 2015

Waziri Mkuu afungua Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Kitaifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Peter Pinda amewataka wazazi na jamii kutambua umuhimu wa watoto kupata elimu na kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanaandikishwa na wanahudhuria bila kukosa hadi kuhitimu elimu ya msingi. Aidha almewataka walimu kufundisha ipasavyo ili elimu itolewayo iwe bora kwa maendeleo ya Taifa.

Waziri Mkuu alisema hayo wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya elimu kitaifa yanayofanyika kwa mara ya pili nchini katika uwanja wa Jamhuri, Mjini Dodoma. Maadhimsho haya yaliyoanza tarehe Mei 11 yanakwenda sambamba na maonesho ya wadau mbalimbali wa Elimu na  yanatarajiwa kuhitimishwa siku ya Ijuma tarehe Mei 15 na Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Aidha, katika ufunguzi huu Mhe. Waziri Mkuu ametoa tuzo kwa Shule, Mikoa na Halmashauri zenye ufaulu uliotukuka na zilizoongeza ufaulu kwa kiwango cha juu katika mitihani 2014 ikilinganisha na matokeo ya 2013. Sambamba na utoaji wa tuzo pia alitoa pikipiki kwa Waratibu Elimu Kata sita waliowakirisha Waratibu Elimu Kata wa nchi nzima

 
 
 



 
 
 
 
 









 

Jumanne, 5 Mei 2015

AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA KKK - CHUO KIKUU CHA DODOMA

Awamu ya pili ya mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu wa shule za Msingi wanaofundisha darasa la I na II yakiendelea katika Chuo Kikuu cha Dodoma ambapo walimu wengine zaidi ya elfu nne wameshiriki kutoka mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Kagera, Katavi, Geita na Mwanza

 Katika awamu ya kwanza mikoa iliyoshiriki ni pamoja na Arusha, Dar es Salaam, Morogoro, Pwani, Rukwa, Ruvuma, Tanga na Singida







.

Jumatano, 29 Aprili 2015



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI




MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU MWAKA 2015

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inawatangazia wabunifu wote wa namna ya kutoa elimu kwa njia mbalimbali kuwasilisha andiko la ubunifu wao, ili waweze kushiriki katika maonesho yatakayokwenda sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Elimu itakayoanza tarehe 11- 15 Mei 2015 katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Andiko la ubunifu liwe limewasilishwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo, 7 Mtaa wa Magogoni, 11479 DAR ES SALAAM siku ya Jumamosi tarehe 02/05/2015.



Elimu Msingi ni Haki ya Kila Mtoto kwa Maendeleo ya Taifa


IMETOLEWA NA:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi





JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI




MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU MWAKA 2015

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inawatangazia wadau wa Elimu na wananchi wote kwa ujumla kuwa Maadhimisho ya Wiki ya Elimu kwa mwaka 2015 yatafanyika kuanzia mwezi April 2015 hadi Mei 2015.
Maadhimisho haya yatafanyika kwa mara ya Pili kitaifa mwaka huu 2015.

Maadhimisho ya Wiki ya Elimu yataanzia katika  ngazi za Halmashauri, Mikoa na baadaye kuhitimishwa kitaifa. Uzinduzi wa maadhimisho hayo kitaifa utafanyika tarehe 11/05/2015 katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma ambapo mgeni Rasmi atakuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda. Kilele cha Maadhimisho kitafanyika tarehe 15/05/2015 katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma ambapo mgeni Rasmi atakuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pamoja na kuongea na wananchi atatoa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi, shule, mikoa na Halmashauri zilizofanya vizuri na zilizoongeza ufaulu kwa kiasi cha Juu katika Mitihani   ya Taifa Darasa la Saba na Kidato cha Nne mwaka 2014.

Maadhimisho ya kitaifa yataenda sambamba na maonesho ya wadau mbalimbali wa elimu yatakayofanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma kuanzia tarehe 11-15/05/2015.
Ili kufanikisha maonesho hayo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inakaribisha wadau wote wa Elimu na Mafunzo kushiriki katika Maadhimisho hayo katika ngazi za Halmashauri, Mikoa na Taifa.

.
Elimu Msingi ni Haki ya Kila Mtoto kwa Maendeleo ya Taifa


IMETOLEWA NA:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
7 Mtaa wa Magogoni,
11479  DAR ES SALAAM.
Tovuti: www.moe.go.tz
19/04/2015