Alhamisi, 7 Aprili 2016

TAARIFA KWA UMAA


YAH: TAARIFA ZA UZUSHI KUHUSU WALIMU KUSHONEWA SARE INAYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII
 

Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi inakanusha taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari “NDALICHAKO NA WALIMU TZ”.

Taarifa hiyo inadai kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa walimu wanaandaliwa sare  watakazo vaa wakati wa kazi.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa Taarifa hizi si za kweli. Aidha, Wizara inawataka watu wanaoeneza taarifa za kizushi za aina hii waache kufanya hivyo ili kuepusha usumbufu unaojitokeza. Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kuanzisha na kueneza uzushi huu.

 

IMETOLEWA NA

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

07/04/2016

Jumanne, 5 Aprili 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi atembelewa na Mabalozi wa Ireland na Finland Ofisini kwake

 
 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akiongea na Balazoi wa Ireland Bi Fionnuala Gilsenan aliyefika ofisini kwake leo asubuhi kwa ajili ya kujadili miradi mbalimbali ya elimu inayoendeshwa nchini.





 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akiongea na Balazoi wa Finland Bw. Pelleka Hakka aliyefika ofisini kwake leo asubuhi kwa ajili ya kujadili miradi mbalimbali ya elim inayoendeshwa nchini pamoja nao ni Oskar Kass na Mkurugenzi wa Kitengo cha Uratibu wa masuala ya elimu Kikanda na Kimataifa 
 
 
 
 
 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi afanya ziara shule za Msingi za Diamond na Olympio



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akipokelewa na viongozi wa shule za Msingi Diamond na Olympio wakati wa ziara yake.





Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akitembelea mazingira ya shule ya Msingi Olympio



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akiongea na wanafunzi wa  shule ya Msingi Olympio




Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akiwa darasani na wanafunzi.



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akizungumza na walimu wa shule za Msingi Olympio na Diamond

Jumanne, 29 Machi 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi atembelea na kuona maendeleo ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akisikiliza  maelezo kuhusu hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila kutoka kwa wasimamizi wa ujenzi


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akikagua maeneo  mbalimbali ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila


 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi akikaangalia ramani ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila kinachoendelea kujengwa.


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi akizungumza na viongozi wa Chuo Kikuu  cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili pamoja na Wakandarasi (Hawapo Pichani)  kuhusu  ujenzi wa Kampasi ya Mloganzila alipotembelea ili kuonea maendeleo ya ujenzi huo.


 
Moja ya Jengo la  Chuo Kikuu  cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila linaloendelea kujengwa

 



Alhamisi, 24 Machi 2016

Serikali yatoa zawadi kwa Halmashauri zilizotekeleza mipango ya kuboresha Elimu


Serikali kwa kushirikiana na wafadhili wa maendeleo wanatekeleza programu inayojulikana kama Lipa Kulingana na Matokeo ambayo inalenga kutoa zawadi kwa Serikali kuu na Halmashauri kulingana na utekelezaji ambapo kwa kuanzia vigezo vifuatavyo vimewekwa kwa ajili ya kupima utendaji wa Halmashauri. Vigezo vilivyowekwa viliangalia Eneo la Ruzuku zinazopelekwa shuleni.  Katika eneo hili Halmashauri 167 zilipimwa kwa kanuni ya kuchukua fedha iliyopelekwa shuleni.

Eneo lingine lililoangaliwa ni upatikanaji wa  Takwimu. Eneo hili liliangalia idadi ya shule zilizopo kwenye Halmashauri ambazo takwimu zake zimekusanywa na kuwekwa mtandaoni.  

Aidha, eneo lingine lililoangaliwa ni Uwiano wa Mwalimu kwa Mwanafunzi: Halmashauri zilipimwa kwa idadi ya shule ambazo zilikuwa na walimu wachache na zimeongezewa walimu. Hii ni kwa sababu Halmashauri zinapimwa uwezo wake wa kupunguza walimu kwenye shule zenye walimu wengi kupeleka kwenye shule zenye walimu wachache na pia kupanga walimu wapya kwenye shule zenye uhaba wa walimu.

 Jumla ya Kila Halmashauri ilitakiwa ipate dola za kimarekani 7,000. Katika hili Serikali kuu pia inapimwa katika uwezo wake wa kupeleka walimu kwenye Halmashauri na kwa tawkimu zilizokusanywa mwaka 2014 wakati wa kusambaza walimu. Halmashauri 112 zilikuwa na uwiano wa kati ya 1:35 -1:50, Halmashauri 25 zilikuwa na uwiano zaidi ya 1:50 na Halmashauri 27 zilikuwa na uwiano wa chini ya 1:35.


Halmashauri ya zilizofanya vizuri na kupata zawadi ni Mbinga iliyopata shilingi 331,234,275.00, Chato 302,637,899.56, Busega 282,677,815.00, Lushoto 267,403,689.33 Nkasi 262,991,890.00, Liwale 260,836,890.00,  Sikonge 244,679,555.61,  Mbarali 216,749,648.88, Mpanda 213,341,853.60 na Tabora 185,191,379.60








Ijumaa, 4 Desemba 2015



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
 
Coat of arms of Tanzania.png

KATAZO LA KUONGEZA ADA KWA SHULE ZISIZO ZA SERIKALI KWA MWAKA WA MASOMO 2016
 
Waraka wa Elimu Na. 4 wa Mwaka 2008 uliweka viwango vya ada vinavyotozwa katika shule za Msingi na Sekondari za Serikali na zile zisizo za serikali. Ada iliyowekwa kwa shule za kutwa zisizo za serikali ni Tsh. 150,000/= na shule za bweni Tsh. 380,000/= kwa mwaka kwa kila mwanafunzi. Aidha waraka huo ulielekeza kwamba ongezeko lolote la ada lazima lipate kibali cha Kamishna wa Elimu kabla ya kuanza kutumika.  
Hata hivyo imegundulika kuna baadhi ya shule zisizo za serikali zimekuwa zikiongeza ada kila mwaka pasipo kupata kibali cha Kamishna wa Elimu. Utamaduni huu wa kuongeza ada kila ifikapo mwishoni mwa mwaka umekuwa ukisababisha usumbufu mkubwa kwa wazazi/walezi na hata baadhi yao kushindwa kuendelea kusomesha vijana wao katika baadhi ya shule.
Kwa tangazo hili wamiliki wote wa shule zisizo za serikali wanaagizwa kufanya yafuatayo:
1.      Kutokuongeza gharama za uendeshaji wa shule zikiwemo ada kwa mwaka wa masomo unaoanzia mwezi Januari mwaka 2016 mpaka watakapopata maelekezo kutoka kwa Kamishna wa Elimu; wale ambao tayari wameongeza gharama na ada kwa mwaka wa masomo wa 2016 bila kibali cha Kamishna wa Elimu, Wizara haitambui ongezeko hilo kwa kuwa ni batili na hivyo zimefutwa.
2.      Ada zote kwa shule zisizo za serikali zitabaki kama zilivyokuwa zimeidhinishwa na Kamishna wa Elimu.
3.      Kuwasilisha taarifa kwa Msajili wa Shule aliyepo Idara ya Ithibati ya Shule inayoeleza kiasi cha ada na gharama  kinachotozwa kwa sasa (kabla ya mwaka wa masomo 2016) na tarehe shule ilipopata kibali kutoka kwa Kamishna wa Elimu kutoza kiwango hicho cha ada.  Taarifa hiyo ifike ndani ya wiki mbili kuanzia tarehe ya tangazo hili.
Wathibiti ubora wa shule waliopo sehemu mbalimbali nchini wanaagizwa kulifuatilia suala hili kwa karibu ili kila shule itekeleze agizo hili na kutoa taarifa zilizoelekezwa katika tangazo hili. Hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa wamiliki ambao hawatatekeleza maagizo haya.  
Aidha Wizara iko katika hatua za mwisho za utafiti na kuandaa mfumo wa kielektroniki wa kutambua gharama za kumsomesha mwanafunzi katika elimumsingi (elimu ya awali, msingi na sekondari) na hivyo wadau mbalimbali watoe ushirikiano kwa timu za wataalamu wanaofanya kazi hii ili kusaidia katika kuukamilisha mfumo na hatimaye kuwa na ada elekezi katika maeneo mbalimbali.
 
     
IMETOLEWA NA KATIBU MKUU
 
 
 




 
 

Jumatatu, 9 Novemba 2015

USHAURI WANGU KWA SERIKALI JUU YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU.


Josias Charles.

Baada ya mchakato mzima wa Kampeni kukamilisha na hatimaye Serikali kuundwa na Chama cha Mapinduzi kupitia kwa aliyekua mgombea wake wa Urais Mh. Dkt. John Pombe Magufuli tunapaswa kuungana wote na kutoa mawazo yenye lengo la kujenga uchumi wa Nchi Yetu.

Kumekuwepo na tatizo sugu la ukosefu ama kuwa na miundombinu mibovu mbalimbali ya Elimu Kama Madarasa, Maktaba, Mabweni, Maabara, Madawati nk. Ukosefu wa miundombinu hii umekwamisha ama kudumaza utoaji wa Elimu nchini.

Binafsi napenda kuishauri Serikali ya awamu ya Tano kuwekeza katika kuimarisha Elimu ya ufundi (VETA) na kuweka sera madhubuti itakayowabana wahitimu wa vyuo vya ufundi kujitolea kama sehemu yao ya mafunzo lakini pia ikiwa kama sehemu ya Kujitolea kujenga Taifa.


Mitaala ya Elimu ya ufundi Kama itatolewa kwa kipindi cha miaka miwili basi mwaka mmoja utumike kwa mafunzo darasani na mwaka mmoja kwa mafunzo kwa vitendo yaani( FIELD). Wanachuo wote wa VETA hata kama watasoma bure lakini wakatakiwa kufanya field kwa mwaka mzima watakua wameshiriki kwa kiwango kikubwa katika Ujenzi wa Taifa letu.

Mfano wanafunzi 10,000 wakichukua mafunzo ya ufundi kwa mwaka kwa uwiano tuu wa mafundi uashi 5000 na mafundi seremala 5000 kisha baada ya masomo ya mwaka mmoja wakaenda field kwa Mwaka mmoja kujenga Shule, hospitali, vituo vya afya, kutengeneza samani za ofisi tutapunguza gharama kiasi gani?

Nchi Yetu tuna raslimali nyingi ikiwemo raslimali watu lakini hatujaweza kuiendeleza. Naomba tuwekeze katika  kuendeleza raslimali tulizo nazo kwa manufaa ya Taifa letu.

Baada ya kuhitimu mafunzo ya miaka miwili tunao uwezo wa kuwatengenezea ajira vijana hawa na kuwawezesha mitaji inayotokana na shughuri zao katika jamii kwa kujitolea kwa mwaka mzima.

Hebu fikiria Serikali inaagiza samani za ofisi kiasi gani kwa mwaka? Pesa kiasi gani inatumika? Vipi kama vijana waliohitimu VETA mafunzo ya miaka miwili tena kwa kujitolea kujenga Taifa kwa mwaka mzima wakisajiriwa na  kampuni na kupata soko la uhakika toka Serikali na kuachana na uagizwaji wa samani za kichina tutapunguza tatizo la ajira kwa kiwango gani?

Vipi kama vijana walio soma ufundi uashi na kujitolea kujenga Taifa kwa mwaka mzima  wakapewa mikataba ya kujenga nyumba kama za NHC na Majengo mengine mengi tutapunguza tatizo la ajira kwa kiwango gani?

Tuna amini Serikali ya awamu ya Tano ipo makini na inalenga kila MTU afanye kazi kutimiza kauli mbiu ya "HAPA KAZI TU"

Mawaziri, Wabunge, na viongozi wote wa Serikali onyesheni ubunifu kulifanya Taifa letu lisonge mbele.

Kwa Leo inatosha.

HapaKaziTu