Ijumaa, 3 Machi 2017

WAZIRI WA ELIMU AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA WANANCHI (FDCs).

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amewataka wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya wananchi kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wafanye kazi Kwa uadilifu, ubunifu, na weledi wa hali ya juu ili vijana wanamaliza kwenye vyuo hivyo wawe na ujuzi na uwezo wa kujiajiri wenyewe.

MAMBO YA MSINGI AMBAYO WAKUU WA VYUO  VYA FDCs WAMETAKIWA KUZINGATIA;
1-KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA
2- WAMETAKIWA KUWA WABUNIFU
3- WAMETAKIWA KUFANYA KAZI KWA MSHIKOMANO
4- WAMETAKIWA KUWA WAADILIFU
5- WAMETAKIWA KUTUMIA NA KUTHAMINI RASILIMALI 






WAZIRI WA ELIMU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA DFID.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako jana amekutana na kufanya mazungumzo na  washirika wa Maendeleo kutoka nchini Uingereza (DFID)  mjini Dodoma ambapo Kwa pamoja wamekubaliana kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kuboresha Miundombinu katika sekta ya Elimu
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akifurahia jambo na wageni wake ambao ni washirika wa Maendeleo kutoka nchini Uingereza, DFID waliofika katika ofisi za wizara hiyo mkoani Dodoma


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na washirika wa Maendeleo DFID wa nchini Uingereza kwenye ofisi za wizara ya Elimu mkoani Dodoma ambapo Kwa pamoja wamekubaliana kuboresha miundombinu ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu

Waziri wa Elimu akisalimia na wageni wake kabla ya kuanza Kwa mazungumzo yao ambayo yalijikita zaidi katika masuala mbalimbali ya sekta ya Elimu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mabweni ya wasichana Kwa wanafunzi wa vijijini  ili kuwaondolea adha wanafunzi kutembea umbali mref.



Jumatano, 1 Machi 2017

Wizara ya Elimu yahamia Dodoma


Waziri wa Elimu  sayansi na teknolojia profesa Joyce ndalichako leo ametanga za  kuwa wizara hiyo imehamia rasmi Dodoma. Viongozi wakuu wote akiwemo mhe.waziri, mhe.naibu waziri, katibu mkuu, naibu Makatibu Wakuu wote tayari wamesharipoti Dodoma katika awamu hii ya kwanza.

Mawasiliano yote yafanyike kupitia anuani ifuatayo:
Katibu mkuu
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
S.L.P. 10
DODOMA

Namba ya simu: 026- 2963633
Tovuti: www.moe.go.tz

Barua pepe: info@moe.go.tz

viongozi wa juu wa wizara wakiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa taasisi, idara na vitengo vilivyochini ya wizara hiyo

Waziri wa Elimu profesa joyce ndalichako akitangaza kuhamia rasmi makao makuu ya nchi, Dodoma.

viongozi wa wizara, wakuu wa taasisi, idara na vitengo vya wizara ya Elimu wakifuatilia maelekezo kutoka Kwa waziri wa Elimu.

Viongozi wa wizara wakikagua majengo ya ofs za wizara ya Elimu.





Jumatatu, 20 Februari 2017

Serikali za Tanzania na China zatia saini ujenzi wa Chuo cha VETA Kagera



 
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Maimuna Tarishi na Mwakilishi wa Masuala  ya Uchumi na Biashara ya Jamhuri ya watu wa China nchini Tanzania Lin Zhiyong wametiliana saini makubaliano ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA kitakachojengwa  Gera mkoani kagera


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Maimuna Tarishi akibadilishana hati za makubaliano (MOU) na Mwakilishi wa Masuala  ya Uchumi na Biashara wa Jamhuri ya watu wa China nchini Tanzania Lin Zhiyong mara baada ya kutiliana saini.

Alhamisi, 16 Februari 2017

Mkutano wa SDGs4 unaendelea leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini DSM nchini Tanzania

Mawaziri kutoka nchi Kumi tatu, wawakilishi, mabalozi na wabunge wakifuatilia kwa makini hotuba ya waziri wa elimu katika mkutano wan chi za Ukanda wa Afrika Mashariki wa akuaanisha changamoto zinazofanana katika mfumo wa  elimu ili kubadilishana uzoefu ili kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo. Mkutano huo unatarajiwa kuitimishwa leo jioni.







Mawaziri kutoka nchi Kumi tatu, wawakilishi, mabalozi na wabunge wakifuatilia kwa makini hotuba ya waziri wa elimu katika mkutano wan chi za Ukanda wa Afrika Mashariki wa akuaanisha changamoto zinazofanana katika mfumo wa  elimu ili kubadilishana uzoefu ili kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo. Mkutano huo unatarajiwa kuitimishwa leo jioni.







MKUTANO WA NCHI 13 ZA UKANDA WA A. MASHARIKI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MALENGO YA MAENDFELEO ENDELEVU SDGs4 YA ELIMU 2030

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akifungua mkutano wa nchi kumi na tatu za ukanda wa Afrika Mashariki kuhusu utekelezaji wa Malengo yaMaendeo Endelevu SDGs4 ya elimu 2030 ambao unafanyika tarehe 15/02/2017 hadi tarehe 16/02/2017 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.





Waziri wa Elimu amebainisha malengo ya mkutano huo kuainisha changamoto zinazofanana na kubadilishana uzoefu wa namna wa kukabiliana na changamoto hizo, ambapo kwa pamoja wanahitaji  uwepo kwa elimu jumuishi yenye usawa bila kujali wanakotoka.





Jumatatu, 6 Februari 2017

Waziri wa Elimu atoa vyeti kwa Halmashauri zilizofanya vizuri katika sekta ya Elimu nchini.


    Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akikabidhi hundi ya Shilingi Milioni Mia Saba na Nne, Mia Sita Ishirini na Saba Elfu na Mia Nane Hamsini Na Sita (704,627,856/=) kwa Halmashauri ya kwanza ya Kaliua Kati Ya Halmashauri zote Nchini zilizoshindanishwa katika utekelezaji wa Mpango wa Lipa Kulingana na Matokeo [ (P4r).




      Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akikabidhi cheti cha ushindi kwa Halmashauri ya Kaliua iliyopata ushindi wa kwanza Kati ya Halmashauri zote Nchini zilizoshindanishwa katika utekelezaji wa Mpango wa Lipa Kulingana na Matokeo [ (P4r).