Jumanne, 12 Aprili 2016

Profesa Ndalichako: Wekeni malengo katika utendaji kazi


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia  na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amewataka Watumishi wa Wizara hiyo kujiwekea malengo katika utendaji kazi wao ili waweze kutimiza malengo makubwa ya sekta ya elimu.


Profesa Ndalichako aliyasema hayo wakati  akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo kutoka Makao Makuu katika ukumbi wa Mikutano wa Karimjee ikiwa ni mara ya kwanza kukutana nao tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi lengo likiwa ni kuwasikiliza lakini pia kujadiliana nao namna bora zaidi ya kuboresha utendaji kazi katika wizara hiyo.

Waziri Ndalichako aliwataka wafanyakazi kufanya kazi  kujituma, kutoa huduma bora kwa wakati kwa kuwa  ni watumishi wa umma na maana ya mtumishi wa umma ni kuwa na  wajibu wa kuwatumikia wananchi ili wapate haki yao kwa wakati kwani haki iliyocheleweshwa ni sawa na haki iliyoptea.

Amewataka watumishi hao kuipende kazi yao,  kwa maana mtumishi anayependa kazi yake  uifahamu kwa undani wake na inakuwa rahisi kuwatyumika wananchi bila ya kuwa na wasiwasi na kujiamini zaidi

 “kila mfanyakazi ni lazima kujivika joho la Wizara kwa maana ya kuijua Wizara vizuri, misingi yake, dira pamoja na sera zinazotuongoza katika utendaji kazi wetu ili tuweze kufikia malengo ya kuinua ubora wa elimu” alisisitza Ndalichako.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi Omary Mkali alimshukuru Waziri kwa kukutana na watumishi na kuahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri ili kuweze kufikia lengo kwa pamoja la kuinua ubora wa Elimu nchini.


1   Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akiingia katika ukumbi wa Karimjee kuongea na wafanyakazi wa Wizara.


1      Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Maimuna Tarishi akimkaribisha Waziri wa Elimu kuongea na wafanyakazi.


1   waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akiongea na wafanyakazi wa Wizara.



1     wafanyakazi wa Wizara ya Elimu Sayansi Teknolojia na Ufundi wakimsikiliza Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako.



Alhamisi, 7 Aprili 2016

TAARIFA KWA UMAA


YAH: TAARIFA ZA UZUSHI KUHUSU WALIMU KUSHONEWA SARE INAYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII
 

Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi inakanusha taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari “NDALICHAKO NA WALIMU TZ”.

Taarifa hiyo inadai kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa walimu wanaandaliwa sare  watakazo vaa wakati wa kazi.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa Taarifa hizi si za kweli. Aidha, Wizara inawataka watu wanaoeneza taarifa za kizushi za aina hii waache kufanya hivyo ili kuepusha usumbufu unaojitokeza. Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kuanzisha na kueneza uzushi huu.

 

IMETOLEWA NA

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

07/04/2016

Jumanne, 5 Aprili 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi atembelewa na Mabalozi wa Ireland na Finland Ofisini kwake

 
 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akiongea na Balazoi wa Ireland Bi Fionnuala Gilsenan aliyefika ofisini kwake leo asubuhi kwa ajili ya kujadili miradi mbalimbali ya elimu inayoendeshwa nchini.





 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akiongea na Balazoi wa Finland Bw. Pelleka Hakka aliyefika ofisini kwake leo asubuhi kwa ajili ya kujadili miradi mbalimbali ya elim inayoendeshwa nchini pamoja nao ni Oskar Kass na Mkurugenzi wa Kitengo cha Uratibu wa masuala ya elimu Kikanda na Kimataifa 
 
 
 
 
 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi afanya ziara shule za Msingi za Diamond na Olympio



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akipokelewa na viongozi wa shule za Msingi Diamond na Olympio wakati wa ziara yake.





Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akitembelea mazingira ya shule ya Msingi Olympio



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akiongea na wanafunzi wa  shule ya Msingi Olympio




Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akiwa darasani na wanafunzi.



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akizungumza na walimu wa shule za Msingi Olympio na Diamond

Jumanne, 29 Machi 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi atembelea na kuona maendeleo ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akisikiliza  maelezo kuhusu hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila kutoka kwa wasimamizi wa ujenzi


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akikagua maeneo  mbalimbali ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila


 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi akikaangalia ramani ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila kinachoendelea kujengwa.


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi akizungumza na viongozi wa Chuo Kikuu  cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili pamoja na Wakandarasi (Hawapo Pichani)  kuhusu  ujenzi wa Kampasi ya Mloganzila alipotembelea ili kuonea maendeleo ya ujenzi huo.


 
Moja ya Jengo la  Chuo Kikuu  cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila linaloendelea kujengwa

 



Alhamisi, 24 Machi 2016

Serikali yatoa zawadi kwa Halmashauri zilizotekeleza mipango ya kuboresha Elimu


Serikali kwa kushirikiana na wafadhili wa maendeleo wanatekeleza programu inayojulikana kama Lipa Kulingana na Matokeo ambayo inalenga kutoa zawadi kwa Serikali kuu na Halmashauri kulingana na utekelezaji ambapo kwa kuanzia vigezo vifuatavyo vimewekwa kwa ajili ya kupima utendaji wa Halmashauri. Vigezo vilivyowekwa viliangalia Eneo la Ruzuku zinazopelekwa shuleni.  Katika eneo hili Halmashauri 167 zilipimwa kwa kanuni ya kuchukua fedha iliyopelekwa shuleni.

Eneo lingine lililoangaliwa ni upatikanaji wa  Takwimu. Eneo hili liliangalia idadi ya shule zilizopo kwenye Halmashauri ambazo takwimu zake zimekusanywa na kuwekwa mtandaoni.  

Aidha, eneo lingine lililoangaliwa ni Uwiano wa Mwalimu kwa Mwanafunzi: Halmashauri zilipimwa kwa idadi ya shule ambazo zilikuwa na walimu wachache na zimeongezewa walimu. Hii ni kwa sababu Halmashauri zinapimwa uwezo wake wa kupunguza walimu kwenye shule zenye walimu wengi kupeleka kwenye shule zenye walimu wachache na pia kupanga walimu wapya kwenye shule zenye uhaba wa walimu.

 Jumla ya Kila Halmashauri ilitakiwa ipate dola za kimarekani 7,000. Katika hili Serikali kuu pia inapimwa katika uwezo wake wa kupeleka walimu kwenye Halmashauri na kwa tawkimu zilizokusanywa mwaka 2014 wakati wa kusambaza walimu. Halmashauri 112 zilikuwa na uwiano wa kati ya 1:35 -1:50, Halmashauri 25 zilikuwa na uwiano zaidi ya 1:50 na Halmashauri 27 zilikuwa na uwiano wa chini ya 1:35.


Halmashauri ya zilizofanya vizuri na kupata zawadi ni Mbinga iliyopata shilingi 331,234,275.00, Chato 302,637,899.56, Busega 282,677,815.00, Lushoto 267,403,689.33 Nkasi 262,991,890.00, Liwale 260,836,890.00,  Sikonge 244,679,555.61,  Mbarali 216,749,648.88, Mpanda 213,341,853.60 na Tabora 185,191,379.60








Ijumaa, 4 Desemba 2015



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
 
Coat of arms of Tanzania.png

KATAZO LA KUONGEZA ADA KWA SHULE ZISIZO ZA SERIKALI KWA MWAKA WA MASOMO 2016
 
Waraka wa Elimu Na. 4 wa Mwaka 2008 uliweka viwango vya ada vinavyotozwa katika shule za Msingi na Sekondari za Serikali na zile zisizo za serikali. Ada iliyowekwa kwa shule za kutwa zisizo za serikali ni Tsh. 150,000/= na shule za bweni Tsh. 380,000/= kwa mwaka kwa kila mwanafunzi. Aidha waraka huo ulielekeza kwamba ongezeko lolote la ada lazima lipate kibali cha Kamishna wa Elimu kabla ya kuanza kutumika.  
Hata hivyo imegundulika kuna baadhi ya shule zisizo za serikali zimekuwa zikiongeza ada kila mwaka pasipo kupata kibali cha Kamishna wa Elimu. Utamaduni huu wa kuongeza ada kila ifikapo mwishoni mwa mwaka umekuwa ukisababisha usumbufu mkubwa kwa wazazi/walezi na hata baadhi yao kushindwa kuendelea kusomesha vijana wao katika baadhi ya shule.
Kwa tangazo hili wamiliki wote wa shule zisizo za serikali wanaagizwa kufanya yafuatayo:
1.      Kutokuongeza gharama za uendeshaji wa shule zikiwemo ada kwa mwaka wa masomo unaoanzia mwezi Januari mwaka 2016 mpaka watakapopata maelekezo kutoka kwa Kamishna wa Elimu; wale ambao tayari wameongeza gharama na ada kwa mwaka wa masomo wa 2016 bila kibali cha Kamishna wa Elimu, Wizara haitambui ongezeko hilo kwa kuwa ni batili na hivyo zimefutwa.
2.      Ada zote kwa shule zisizo za serikali zitabaki kama zilivyokuwa zimeidhinishwa na Kamishna wa Elimu.
3.      Kuwasilisha taarifa kwa Msajili wa Shule aliyepo Idara ya Ithibati ya Shule inayoeleza kiasi cha ada na gharama  kinachotozwa kwa sasa (kabla ya mwaka wa masomo 2016) na tarehe shule ilipopata kibali kutoka kwa Kamishna wa Elimu kutoza kiwango hicho cha ada.  Taarifa hiyo ifike ndani ya wiki mbili kuanzia tarehe ya tangazo hili.
Wathibiti ubora wa shule waliopo sehemu mbalimbali nchini wanaagizwa kulifuatilia suala hili kwa karibu ili kila shule itekeleze agizo hili na kutoa taarifa zilizoelekezwa katika tangazo hili. Hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa wamiliki ambao hawatatekeleza maagizo haya.  
Aidha Wizara iko katika hatua za mwisho za utafiti na kuandaa mfumo wa kielektroniki wa kutambua gharama za kumsomesha mwanafunzi katika elimumsingi (elimu ya awali, msingi na sekondari) na hivyo wadau mbalimbali watoe ushirikiano kwa timu za wataalamu wanaofanya kazi hii ili kusaidia katika kuukamilisha mfumo na hatimaye kuwa na ada elekezi katika maeneo mbalimbali.
 
     
IMETOLEWA NA KATIBU MKUU