Jumanne, 6 Septemba 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dr. John Pombe Maghufuli afanya ziara kukagua ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo ya awali kutoka kwa Profesa Florens Luoga (Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma) kuhusu ujenzi wa mabweni ya chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati alipotembelea eneo la mradi huu muda mfupi kabla ya Rais kuwasili.Kushoto ni Katibu Mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish.



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Magufuli wakati alipotembelea Mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).





Katibu Mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish akisalimiana na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli wakati alipotembelea Mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
 


 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli  akipata maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa TBA Aktecti (Arch) Elius A.. Mwakalinga kuhusu mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Mradi huo chuoni hapo. Kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako.
 










Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli akikagua mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Mradi huo. Kushoto ni Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako.





 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako akimshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli  kwa uamuzi wa kujenga mabweni katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni hatua katika kuleta ubora wa elimu.


  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Magufuli akizungumza na wanajumuiya ya Chuo Kikuu pamoja na Wafanyakazi wa Mradi huo mara baada ya kufanya ukaguzi wa ujenzi wa mabweni hayo.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.

Jumatano, 31 Agosti 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Ndalichako afunga Mafunzo ya Vijana kwa Mujibu wa sheria Ruvu JKT

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akisalimiana na baadhi ya Maafisa wa JKT Ruvu  alipohudhuria sherehe za kufunga mafunzo ya vijana wa mujibu wa sharia Operesheni Magufuli zilizofanyika Ruvu JKT Mlandizi

 Mkurugenzi wa ElimuMsingi Nicholaus Burreta kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  akisalimiana na baadhi ya Maafisa wa JKT Ruvu  alipohudhuria sherehe za kufunga mafunzo ya vijana wa mujibu wa sharia Operesheni Magufuli zilizofanyika Ruvu JKT Mlandizi


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akiangalia mazoezi yanayofanywa na vijana (hawapo pichani) waliohitimu mafunzo alipohudhuria sherehe za kufunga mafunzo ya vijana wa mujibu wa sharia Operesheni Magufuli zilizofanyika Ruvu JKT Mlandizi

Baadhi ya vijana wa JKT waliokuwa katika mafunzo kwa mujibu wa sharia wakimuonyesha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia mazoezi ambayo wamejifunza kwa kipindi chote cha mafunzo yao katika Kambi ya Ruvu JKT



                                     
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akipokea salam kutoka kwa vijana waliohudhuria mafunzo kwa mujibu wa sharia wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo hayo katika kambi ya JKT Ruvu


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akikagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake kutoka kwa vijana waliohudhuria mafunzo kwa mujibu wa sharia wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo hayo katika kambi ya JKT Ruvu
Baadhi ya wananchi walioshiriki katika sherehe ya kufunga mafunzo ya vijana wa mujibu wa sharia operation Magufuli zilizofanyika katika kambi ya JKT Ruvu

Jumatano, 24 Agosti 2016


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA



WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA


TAARIFA KWA UMMA



Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST), kwa mujibu wa Waraka Namba 4 wa mwaka 2014, imeipa Taasisi ya Elimu Tanzania mamlaka ya kufanya  uthibiti wa ubora wa vitabu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Itakumbukwa kuwa kabla ya mwaka 2014, ithibati kwa vitabu na vifaa vya kielimu ilikuwa inatolewa na Kamati ya Ithibati ya Vitabu na Vifaa vya Kielimu (EMAC), ambayo ilivunjwa mwaka 2013.


Kwa muktadha huo, Wizara inawaagiza wachapishaji wote wa vitabu vya Darasa la Nne hadi Darasa la Saba ambavyo vina ithibati ya EMAC kuviwasilisha Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa ajili ya kufanyiwa tathmini. Ili kufanikisha zoezi hili nakala nne (4) za kila chapisho ziwasilishwe kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania kabla ya tarehe 30 septemba, 2016. Baada ya muda huo kupita, vitabu vyote ambavyo havitakuwa vimewasilishwa na kuhakikiwa na Taasisi hiyo vitafutwa katika orodha ya vitabu vyenye ithibati.

Baada ya zoezi la uhakiki kukamilika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na OR – TAMISEMI, itafanya ufuatiliaji kwenye shule na maduka ya vitabu ili kuhakiki utekelezaji wa agizo hili.

Aidha, hatua stahiki zitachukuliwa kwa wauzaji/wachapishaji watakaoendelea kuuza vitabu vitakavyokuwa vimefutwa.



Imetolewa na:



Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia akabidhi Chuo cha Ualimu Kitangali kwa Wakandarasi


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akiingia katika Chuo cha Ualimu Kitangali alipokwenda kukabidhi Chuo hicho kwa wakandarasi wa ujenzi kwa ajili ya kufanya ujenzi majengo mapya ya chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni chuoni hapo.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akipata maelezo kutoka kwa mkandarasi (hayupo pichani) juu ya ujenzi wa  Chuo cha Ualimu Kitangali alipokwenda kukabidhi Chuo hicho kwa wakandarasi wa ujenzi kwa ajili ya kufanya ujenzi majengo mapya ya chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni chuoni hapo.



Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akifanya ukaguzi kwenye ya jiko linatumika kwa jili ya kupikia chakula cha wanafunzi alipokwenda kukabidhi Chuo hicho kwa wakandarasi wa ujenzi kwa ajili ya kufanya ujenzi majengo mapya ya chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni chuoni hapo.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akikabidhi mkataba pamoja na michoro kwa mmoja wa wakandarasi watakaofanya kazi ya ujenzi ya miundombinu ya Chuo cha Ualimu Kitangali alipokwenda kukabidhi Chuo hicho kwa wakandarasi wa ujenzi kwa ajili ya kufanya ujenzi majengo mapya ya chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni chuoni hapo.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akikabidhi mkataba pamoja na michoro kwa mmoja wa wakandarasi watakaofanya kazi ya ujenzi ya miundombinu ya Chuo cha Ualimu Kitangali alipokwenda kukabidhi Chuo hicho kwa wakandarasi wa ujenzi kwa ajili ya kufanya ujenzi majengo mapya ya chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni chuoni hapo.


Jumanne, 23 Agosti 2016

Serikali yawasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma Kuandika na Kuhesabu


 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akiongea na Wawakilishi kutoka kamati ya Global Partnership for Education  wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji ya  Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara 



 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akiongea na Wawakilishi kutoka kamati ya Global Partnership for Education  wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji ya  Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara



Kaimu  Mkurugenzi wa Sera na Mipango  wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Gerald Mweli akiongea na Wawakilishi kutoka kamati ya Global Partnership for Education  wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji ya  Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara




 Baadhi ya wajumbe wa kikao wakifuatilia kwa makini maelezo yanayotolewa na wasimamizi wa Mradi huo wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji ya  Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara


Baadhi ya wajumbe wa kikao wakifuatilia kwa makini maelezo yanayotolewa na wasimamizi wa Mradi huo wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji ya  Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara