Jumatano, 6 Juni 2018

OLE NASHA: SERIKALI YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA DFID


Serikali imehaidi kuendelea kushirikiana na wadau wa Sekta ya Elimu katika kuhakikisha watoto wa kitanzania wanapata Elimu iliyo bora ili kufikia malengo ya mkakati wa kuwa na uchumi wa viwanda.

 Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mheshimiwa Wiliam Ole Nasha jijini Dar es Salaam katika kikao cha pamoja kilichowakutanisha Wadau wa Elimu walio chini ya Shirika la  Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID

Naibu Waziri Ole Nasha amesema ushirikiano wa serikali ambao umekuwepo kwa muda mrefu na wadau hao wa Elimu umechangia katika kuhakikisha mtoto wa Kitanzania anapata Elimu iliyo bora.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akizungumza na wajumbe katika kikao kilichoandaliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID. Kikao hicho kimewashirikisha wadau wa Elimu kutoka EQUIP –T, EP4R, HDIF,GPE, British Council, GPE, na RISE
“Elimu bora kwa kila mtoto wa kitanzania ndiyo msimamo wa Serikali, katika kutekeleza hilo sera ya Elimu bila malipo imekuwa  na baadhi ya chagamoto  na katika kukabiliana nazo ndiyo maana wamekuwepo wadau wa Elimu ambapo sasa wanafanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ili kutimiza malengo yanayokusudiwa, kwani hatuwezi kuboresha Elimu kama kila mtu atafanya kazi peke yake, Umoja ni Nguvu.”amesema Mheshimiwa Ole Nasha.

Ole Nasha amesema mpaka sasa wadau hao wa Elimu kupitia Mpango wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) wameshatoa  kiasi cha zaidi ya bilioni 200 ambazo zimekusudiwa kufanya uboreshaji wa Miundombinu ya shule za msingi na Sekondari, pamoja na kukarabati na kujenga vyuo vya Ualimu.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akishiriki katika moja ya majadiliano ya pamoja katika kikao kilichoandaliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID kikao ambacho kimefanyika jijini Dar es salaam.

Naye Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza-DFID Jane Miller ameishukuru serikali ya Tanzania kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakiupata katika kuhakikisha fedha zinazotolewa zinatumika kama zilivyokusdiwa. Kikao hicho kimewashirikisha wadau wa Elimu kutoka EQUIP –T, EP4R,HDIF,GPE, British Council, GPE, na RISE

Jumanne, 29 Mei 2018

PROFESA MDOE ASHIRIKI KONGAMANO LA SAYANSI NA TEKNOLOJIA NCHINI ISRAEL


Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe yuko mjini Jerusalem nchini Israel, kwa ajili ya kushiriki kongamano la Mawaziri la kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia katika kuhudumia wanadamu.

Mkutano huo ulioanza jana ulifungukiwa rasmi na Waziri Mkuu wa Israel ambapo Mada kuu ya mkutano huo ni “kufikiria nje ya boksi”.
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Israel wakati wa kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia.

Kongamano hilo la siku 4 linawashirikisha Mawaziri, Naibu Mawaziri na viongozi mbalimbali.
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wengine wa kongamano la Mawaziri la kuadhimisha miaka 70 ya Sayansi na Teknolojia katika kuhudumia wanadamu nchini Israel.

Jumatatu, 28 Mei 2018


To all Heads of Secondary Schools,

RE:  GUIDELINE FOR EAST AFRICAN ESSAY WRITING COMPETITION FOR SECONDARY SCHOOLS 2018

The East African Community Secretariat (EAC) has organized the EAC students essay writing competition for the year 2018.  The Essay writing competition is intended to broaden knowledge of the school going population on EAC activities.  The competition is open to students from Form I to Form IV who are required to write essays between 1000 – 1500 words.  The students are required to begin researching on the topic prior to writing and submitting to their Heads of Schools by 30th July, 2018. 

The topic for the year 2018 in English is:
How can Science and Technology be used to improve the lives of the citizens of the East African Community?”

In Kiswahili
Ni kwa namna gani Sayansi na Teknolojia inaweza kutumika kuimarisha maisha ya wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki?”

In French
"Comment pouvons-nous utiliser la Science et la Technologie pour ameliorer la vie des Peuples de la Communauté Est Africaine?”

The Heads of Schools will then be expected to constitute a marking panel which will choose best essays of the school.  The panel should go through the essays (Please do not mark the essays) and choose three essay to be submitted to Permanent Secretary Ministry of Education, Science and Technology by 15th August, 2018.

The following are the guidelines for essay competition:
·  The length of the essay should be between 1,000 and 1,500 words,
·  The essay can be written in English, French or Kiswahili,
·  The essay should be in their own hand writing,
·  Students information such as name, sex, class, school address, region, Country and title of the essay should be written on the cover page,
·  The essay should be written on white A4 lined/ruled papers (Similar to the draft pads),
·  Written only on one side of the paper,
·  Students should draw double margin in each paper,
·  The Head of Schools to certify that the essay is student’s own work. (signature and stamp),
·                 Students to show the reference materials they have used in writing the essay.



Moshi J. Kabengwe
ACTING PERMANENT SECRETARY



Jumapili, 27 Mei 2018

ZAIDI YA BILIONI NNE KUTUMIKA KWENYE MIRADI YA UTAFITI.


·         WAZIRI NDALICHAKO ASISITIZA KUWA ZISITUMIKE VINGINEVYO

Serikali imetoa zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya Taasisi na Watafiti walioshinda maandiko ya miradi 8 ya utafiti ambayo itaanza kufadhiliwa mwaka huu wa fedha.

Akizungumza jijini Dar es Salaam kabla ya kukabidhi hundi kwa Taasisi zilizoshinda fedha hizo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa. Joyce Ndalichako amesema miradi yote iliyopata fedha ni ile ambayo ina malengo madhubuti ya kuimarisha uchumi wa viwanda hadi ifikapo 2025.

Waziri Ndalichako amesema kufadhiliwa kwa miradi hiyo nane kutaleta mchango mkubwa wa uzalishaji wa dawa nchini na kupunguza uagizwaji wa dawa kutoka nje, uboreshaji wa maabara za uhandishi jeni, kuongeza ushindani wa bidhaa, kuongeza uzalishaji wa mazao, uzalishaji wa mimea, pamoja na kuchangia katika uanzishwaji wa viwanda.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikabidhi hundi kwa Taasisi na Watafiti walioshinda maandiko ya Miradi ya utafiti unaosimamiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)

Waziri Ndalichako amezitaka taasisi zilizopata fedha hizo kuzitumia kwa uadilifu na kwa malengo yaliyokusudiwa na siyo vinginevyo.

Miradi hiyo nane ni pamoja na ule wa umaliziaji wa kiwanda cha uzalishaji wa dawa na maabara ya utafiti ya mabibo, uimarishaji wa miundombinu ya utafiti na ugunduzi wa dawa katika chuo kikuu cha tiba (MUHAS), Muhimbili, ununuzi wa vifaa na uboreshaji wa maabara ya uhandisi jeni ya Taasisi ya Mifugo TALIRI kwa ajili ya kuongeza kasi ya uzalishaji wa mifugo, Uboreshaji wa maabara ya Chanjo ya Taasisi ya Taifa Kibaha.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipokelewa na baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kuwasili katika Taasisi hiyo jijini Dar Es Salaam. 

Miradi mingine ni Uboreshaji wa maabara ya udongo, ili kuimarisha Afya ya Udongo kwa ajili ya kilimo endelevu kwa lengo la kuimarisha uchumi wa viwanda, Uboreshaji wa maabara ya kisasa ya utafiti wa mbogamboga na matunda kaskazini mwa Tanzania (HORTI Tengeru), Ukarabati wa mtambo wa utafiti wa kutengeneza mvinyo  katika taasisi ya utafiti wa kilimo, Makutopora na uboreshaji wa usimamizi wa maabara za uchakataji wa mazao ya taasisi ya utafiti wa viwanda TIRDO. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH Dk. Amosi Nungu akizungumza na washiriki wa Mkutano wa utoaji wa hundi kwa washindi wa maandiko ya miradi

Jumatatu, 21 Mei 2018

EP4R IMEIFANYA SHULE YA SEKONDARI WASICHANA SONGEA KUWA MPYA


Mkuu wa shule ya Sekondari wasichana Songea Tupoke Ndwala amesema shule yake ilipokea zaidi ya milioni Mia mbili kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknlojia kwa ajili ya ukarabati wa mabweni na tayari wamekwisha karabati bweni moja ambalo Lina uwezo wa kuchukua wanafunzi wa kike 115.

Akizungumza na waandishi wa habari Ndwala amesema kabla ya kupokea Fedha hizo kwa ajili ya ukarabati hali ilikuwa mbaya, ikizingatiwa kuwa shule hiyo ni miongoni mwa shule kongwe hapa nchini na hivyo ilikuwa haijafanyiwa ukarabati.

“Kwa kweli naipongeza sana Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukarabati huu ambao kwa kweli sasa hivi muonekano wa shule na mabweni umeifanya shule iwe mpya, mandhari ya shule ni nzuri, walimu na wanafunzi ambao ndiyo watumiaji wakubwa wa miundombinu hii kwa kweli wanafurahia pia wanajifunza na kufundisha kwa Amani”, anasema Ndwala ambaye ni Mkuu wa shule hiyo ya Sekondari wasichana Songea.
BWENI la MPUTA ni moja ya BWENI lililokarabatiwa katika shule ya sekondari wasichana Songea, (Songea Girls Secondary School) iliyopo manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wameelezea kufurahishwa na ukarabati huo na kusema kuwa hivi sasa mabweni yanapendeza hata ukitaka kupiga kumbukumbu ya picha kuonyesha kuwa nilisoma hapa inavutia tofauti na ilivyokuwa awali mabweni yalikuwa  hayavutii. 

Mary Komba anasema awali mabweni kwa maana ya Dari, Sakafu, Vitanda, makabati  na hata rangi iliyokuwa imepigwa ukutani ilikuwa mbaya lakini sasa hivi tumerejea kwenye hali ya nzuri na tunafurahia mno.

“Kwa kweli tunaipongeza sana Serikali ya awamu ya Tano kwa kutuboreshea miundombinu hii ya shule, sasa hivi mabweni yetu ni mazuri na yanapendeza sana hivyo tunaahidi na sisi tutasoma kwa bidii na kufaulu kwa kuwa miundombinu ni mizuri ya kujifunzia”, anasema Mary Komba mmoja wa wanafunzi wa kidato Cha Tano katika shule hiyo.
Muonekano wa sasa wa BWENI la MPUTA baada ya Kufanyiwa ukarabati na fedha zilizotolewa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia kupitia programu yake ya lipa kulingana na Matokeo, EP4R.

Katika hatua nyingine timu  ya Maafisa kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na na wanahabari walifika katika shule ya Msingi Tembo Mashujaa na kufurahishwa na namna mwalimu wa darasa la pili alivyokuwa akitumia mbinu za kufundishia za kuimbaa , kucheza na wanafunzi wake kwa lengo la kuwafundisha wanafunzi hao.

Mwalimu Assumpta Banda ambaye anafundisha wanafunzi wa darasa la pili  anasema ualimu ni Wito, nidhamu, uadilifu na upendo kwa wale unaowafundisha na kuwa hayo ndiyo yamekuwa maisha yake na anaipenda sana kazi yake.

“ Mwezi ujao ninastaafu, kazi ya Ualimu ni wito. Madarasa haya ya chini ndiyo Msingi wa Elimu hivyo naishukuru sana Serikali kwa kutupatia mafunzo ya KKK ambapo hivi sasa tunatumia zana na mbinu za kufundishia hali ambayo inarahisisha mwanafunzi kuelewa kwa wepesi na pia watoto wanaoenda shule”, anasema Ndwala.
Ukarabati ukiwa unaendelea katika mabweni mengine katika shule ya sekondari wasichana Songea. Shule hiyo ipo kwenye manispaa ya Songea mkoani Ruvuma

Jumamosi, 19 Mei 2018

WANAFUNZI WA CHIDYA WAIPONGEZA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MAJI.


Wanafunzi wa shule ya Sekondari Chidya iliyopo Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara wameipongeza serikali kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo pamoja na kuchimba kisima ambacho kimewapungizia adha ya upatikanaji wa Maji kwa urahisi.

Wanafunzi hao wametoa kauli hiyo wakati walipofanya mahojiano na waandishi wa habari kufuatia ziara ya ufuatiliaji wa uboreshaji wa miundombinu ya shule na ujifunzaji na ufundishaji wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu - KKK.

 Wanafunzi hao wamesema mwanzoni miundombinu ilikuwa imechakaa pia walikuwa wanafuata Maji umbali takribani kilometa moja na pia iliwalazimu kila siku kuamka alfajiri ili kufuatilia Maji hivyo iliwafanya wachoke na hata kupunguza morali ya kusoma.

 Jengo la Utawala lililokarabatiwa katika Shule ya Sekondari Chidya Wilayani Masasi Mkoani Mtwara.

“Kwa kweli hili la Maji wanafunzi lilikuwa linakera sana maana inatulazimu kuamka kila siku alfajiri kufuatilia maji na kisha kujindaa kuelekea shuleni kwa ajili ya masomo, kwa kweli hii ilikuwa inatuchosha na pia ilikuwa ni hatari kwa sababu tulikuwa tunakutana na wadudu wabaya kama vile nyoka,” anasema mmoja wa wanafunzi hao Saidi Mnguvu.

 “Nakumbuka tulikuwa tunatolewa darasani kwa ajili ya kuafuatilia maji, hata vipindi wakati mwingine vilikuwa vinakatishwa ili tuweze kwenda kufuata Maji sasa adha hii ya Maji kwa kweli imeisha na sasa tunaishi kwa raha na tunapata Maji muda wote,” anasema Mnguvu.
Muonekano wa vyumba vya madarasa vilivyojengwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) katika Shule ya Sekondari Chidya iliyopo Wilayani Masasi Mkoani Mtwara. 


 Mkuu wa shule hiyo ya Sekondari ya Chidya Zawadi Mdimbe ali
sema shule hiyo ilipokea zaidi ya milioni Mia mbili kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa kulingana na matokeo yaani (EP4R) ambazo zimetumika kukarabati Miundombinu ya vyumba vya madarasa, ujenzi wa Nyumba za walimu, kuboresha miundombinu ya Maji, bwalo, Jiko pamoja na kukarabati ofisi za walimu za shule hiyo.
Muonekano wa majengo mawili yenye vyumba vya madarasa vilivyokarabatiwa katika Shule ya Sekondari Chidya Wilayani Masasi Mkoani Mtwara.

Alhamisi, 17 Mei 2018

KKK IMEONDOA WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA


·   EP4R IMEONDOA ADHA YA VYOO ILIYOKUWA INAIKABILI SHULE YAMBAWALA 

Mkuu wa shule ya Ufundi Mtwara Paul Kaji amepongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo na hivyo kuondoa kabisa changamoto mbalimbali zilizoKuwa kikwazo kwa wanafunzi na walimu shuleni hapo.

Kaji ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na timu ya wanahabari waliofika shuleni hapo kwa lengo la kuangalia ukarabati wa miundombinu ya shule hiyo ambapo zaidi ya bilioni moja imetumika kukarabati vyumba vya madarsa, ofisi za walimu, mabweni, Bwalo la chakula, sehemu za kuandalia chakula (majiko), kukarabati njia Maalumu za wanafunzi wenye ulemavu, kurejesha miundombinu ya umeme na Maji katika hali ya kawaida.

Pia baadhi ya wanafunzi waliohojiwa wameelezea kufurahishwa na ukarabati huo na hivyo kuwafanya kuwa katika mazingira mazuri ya kusomea.
“Tunaishukuru Serikali kwa kutuboreshea miundombinu ya shule siyo tu shule yetu imependeza bali hata sisi tuna uwezo wa kusoma muda wowote kwa kuwa umeme upo, tunawasilisha shukrani na hivyo tunaahidi tutasoma kwa bidii ili tufaulu vizuri” anasema David Andrew mmoja wa wanafunzi wa kidato cha pili katika shule hiyo ambaye anasomea fani ya ujenzi.

Muonekano wa darasa linaloongea KKK katika Shule ya Msingi Msijute iliyopo Mkoani Mtwara


Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mbawala Ali Haroun amesema licha ya kujenga madarasa mapya lakini jambo ambalo limeleta heshima kwao ni ujenzi wa matundu ya vyoo.

Alisema katika fedha hizo wamejenga matundu ya vyoo 10 na kufanya jumla ya matundu ya vyoo kuwa 16 na madarasa 8 jambo ambalo limesaidia kuongeza wanafunzi na kila darasa kukaa wanafunzi kulingana na ukubwa wa darasa.
Hata hivyo aliongeza kuwa matundu ya vyoo yamewasaidia katika kuhakikisha walimu wanakaa shuleni muda wote kuliko hapo zamani ambapo ilikuwa ni lazima kwenda kujisaidia majumbani kwao.

‘’Hapo awali kulikuwa na shida kabisa kwani walimu walikuwa wanafika shuleni wakijisikia kubanwa na haja wanakimbilia nyumbani na kuwafanya kuchukua muda mwingi hadi wa vipindi ndipo wanarejea shuleni kwa ajili ya kuendelea na masomo,’’

‘’ Programu hii ni mkombozi kwetu kwani hata wanafunzi waliokuwa wakikaa katika madarasa kwa kubebana sasa wanakaa kwa nafasi na mpaka chumba kimoja kimebaki kwa kukosa wanafunzi,’’aliongeza mwalimu Ally.
Mwalimu wa darasa la awali katika Shule ya Msingi Msijute Mariamu Milanzi akifundisha kwa kutumia zana zilizowekwa katika darasa darasa la awali. Matumizi ya Zana za kufundishia unasaidia watoto kuelewa kwa urahisi kupenda shule na kupunguza utoro.

Naye mwalimu, Isabela Mwambona alisema mradi huo umewarahisishia kazi kutokana na kufundisha kwa nafasi na hata kuwafikia wanafunzi  mmoja baada ya mwingine kwa ufundishaji.

Katika hatua nyingine programu ya Kusoma, Kuandika na  Kuhesabu (KKK) imezaa matunda katika shule mbalimbali za Mkoa wa Lindi na Mtwara.
Isabela alisema tangu wapeate mafunzo ya ufundishaji wa KKK kwa kutumia vitendo na michoro kwa sasa wamefanikiwa kupunguza idadi ya wasiojua Kusoma na Kuandika shuleni hapo.
Wanafunzi wa Darasa la Awali katika shule ya Msingi Msijute wakiwa darasani tayari kwa kuanza masomo.