Jumatatu, 19 Novemba 2018

SERIKALI YAJENGA SEKONDARI YA MFANO KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI ARUSHA


Serikali inajenga  Shule ya Sekondari Maalum ya mfano kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Chuo cha Ualimu Patandi kilichopo mkoani Arusha yenye uwezo wa kudahili wanafunzi 600 kwa mara moja ikiwa ni mkakati wake wa kuongeza fursa za udahili kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kwa Mkoa wa Kilimanjaro, ambapo amesema Serikali imekarabati miundombinu kwenye shule kongwe ya Moshi Ufundi inayopokea wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimpongeza mwanafunzi mwenye mahitaji maalum baada ya kufanya vizuri katika maonyesho ya mavazi katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kwa Mkoa wa Kilimanjaro

 “Serikali inaendelea kutekeleza mipango mbalimbali inayolenga kuongeza upatikanaji wa fursa na kuimarisha ubora wa elimu inayotolewa katika ngazi zote kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambapo tayari serikali imekarabati miundombinu ya shule kongwe ya Moshi Ufundi ambayo inapokea wanafunzi wenye mahitaji maalumu”. Alisisitiza Prof. Ndalichako.

Waziri Ndalichako amesema watu wenye mahitaji maalum wana fursa sawa ya kushiriki katika michezo na kufanya hivyo kunasaidia kuondoa kasoro za kimwili na kiakili na baadhi ya ulemavu unaweza kurekebishwa kwa kushiriki katika michezo na burudani.
Prof Ndalichako amesisitiza kuwa ushiriki katika michezo, hususan kwa watoto wenye mahitaji maalum ni muhimu sana kama ilivyowekwa bayana katika kifungu cha 52 cha Sheria ya Watu wenye Ulemavu Namba 9 ya mwaka 2010 kinachosisitiza umuhimu wa Watu wenye ulemavu kushiriki katika michezo, starehe na burudani.

Akizungumza katika Bonanza hilo Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Walemavu) Stella Ikupa amewataka wanafunzi wenye mahitaji maalum kuunga mkono juhudi za serikali ya Awamu ya Tano kwa kuendelea kujitambua, kujikubali na kujituma ili kujikwamua katika changamoto wanazokutana nazo katika masomo yao.
Waziri Ikupa amewataka wanafunzi hao pia kujiunga na vyuo vya ufundi ambavyo vitawawezesha kupata satadi ambazo watazitumia kwa ajili ya  kujiari wenyewe badala ya kuwa tegemezi.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akibadilishana mawazo na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Walemavu) katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kwa Mkoa wa Kilimanjaro

Naye Mratibu wa Bonaza hilo ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (Vyuo Vikuu) Esther Mmasi amesema wakati wa  maandalizi ya Bonanza hilo amebaini kuwepo kwa uhaba wa viwanja vya michezo katika shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambapo ameiomba serikali kuhakikisha inaboresha miundominu ili kuwajengea uwezo wanafunzi hao.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na wadau wa Elimu pamoja na wanafunzi wenye mahitaji maalum ( Hawapo Pichani) katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro.





Ijumaa, 16 Novemba 2018


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY



THE STIPENDIUM HUNGARICUM SCHOLARSHIP PROGRAMME FOR THE ACADEMIC YEAR 2019/2020

1.0 Call for Application

The General Public is hereby informed that, the Government of Hungary has opened the new Stipendium Hungaricum Call for Applications for studies starting in the academic year 2019/2020. Interested candidates are highly encouraged to apply.

2.0 Mode of Application 


The online application system can be reached through the following link:  https://apply.stipendiumhungaricum.hu/

Further details on the eligible study Programmes can be accessed through the following link: http://studyinhungary.hu/study-in-hungary/menu/stipendium-hungaricum-scholarship-programme/call-for-applications-2019-2020.html

NB: The deadline for submission of online Applications is 15th January, 2019

Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business and Law,
University of Dodoma,
P. O. Box. 10,
40479 DODOMA.


MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY
 


   
ME-024/2018-2019/HQ/G/03

For

SUPPLY OF REFERENCE BOOKS FOR TEACHERS’ COLLEGES


Invitation for Tenders


                                                                                                            Date: 16th November, 2018
1.       This Invitation for Tenders follows the General Procurement Notice (GPN) which appeared on PPRA website online on 02nd October, 2018.


2.       The Ministry of Education, Science & Technology has received a grant from the Global Affairs Canada (GAC) towards the cost of Teacher Education Support Project, and it intends to apply part of the proceeds of this grant to cover eligible payments under the contract for Supply of Reference Books for Teachers’ Colleges.

3.       The Ministry of Education, Science & Technology now invites sealed Tenders from eligible National Suppliers of Reference Books for Teachers’ Colleges.

  1. Tendering will be conducted through the National Competitive Bidding (NCB) procedures specified in the Public Procurement Regulations– Government Notice No. 446 of 2013 and are open to all Tenderers as defined in the Regulations.
5.       Interested eligible Tenderers may obtain further information from and inspect the Tendering Documents at the office of the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O. Box 10- 40479 Dodoma, Office number 320 from 0900 to 1530 hours on Monday to Friday inclusive except on public holidays.

6.       A complete set of Tendering Documents in English and additional sets may be purchased by interested Tenderers on the submission of a written application to the address given under paragraph 5 above and upon payment of a non-refundable fee of TZS. 100,000.00 (Tanzanian shillings hundred thousand) only. Payment should either be by Cash.

7.       All Tenders must be accompanied by a Tender Security in an acceptable form in the amount of TZS. 20,000,000.00 (Tanzanian shillings Twenty Million) or freely convertible currencies.

  1. All Tenders in one original plus two copies, properly filled in, and enclosed in plain envelopes must be delivered to the address Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O. Box 10- 4079, Dodoma, Room 320 at or before 10:30 local hours on Tuesday 04th December, 2018. Tenders will be opened promptly thereafter in public and in the presence of Tenderers’ representatives who choose to attend in the opening at the Conference Room, Ground Floor, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10- 40479Dodoma.

9.       Late Tenders, portion of Tenders, electronic Tenders, Tenders not received, Tenders not opened and not read out in public at the Tender opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.





PERMANENT SECRETARY,
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE & TECHNOLOGY
University of Dodoma (UDOM), Block No. 10, P.O.Box10,
40479- DODOMA.

 


Alhamisi, 15 Novemba 2018

DKT. AKWILAPO AZITAKA TAASISI ZA ELIMU YA JUU KUFANYA TAFITI ZA KITAALAMU


Serikali imezitaka Taasisi za Elimu ya Juu nchini kutimiza wajibu wake wa kufanya tafiti za kitaalamu kwa kushirikiana na wadau ili kuongeza ufahamu kwa jamii na kuisaidia serikali kwenye kutunga na kusimamia sera utungaji na usimamizi wa sera mbalimbali za nchi.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Katibu MkuuWizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo kwenye ufunguzi wa mkutano wa mwaka waWadau wa Tafiti kwa Maendeleo shirikishi uliyofanyika jijini Dar es Salaam ambapo amezitaka Taasisi zinazohusiana na Tafiti kutafuta namna ya kufikisha matokeo ya tafiti hizo kwenye jamii kwa lengo la kuwaletea wananchi Mabadiliko na Maendeleo.


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza na wadau waElimu kwenye ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa mwaka wa wadau wa tafiti kwa maendeleo shirikishi uliyofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo amezita kataasisi za elimu ya juu kufanya tafiti ili kuisaidia serikali  kutunga sera.



“Hakuna asiyefahamu kuwa Elimu ni chombo muhimu kwa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii, na kuwakupitia Elimu ndiyo njia pekee inayoweza kutoawataalamu wenye ujuzi wa kusaidia jamii kwenye kilanyanja, hivyo ni wakati muafaka kwa Taasisi za Elimu kulitambua hilo na kujua nyakati za sasa zinahitaji pia ufahamu wa masuala ya kidijitali,”alisistiza Dkt. Akwilapo.

Kwa upande wake Balozi wa Sweden nchini Tanzania,Anders Sjoberg, amesema Shirika la Maendeleo la Kimatiafa (SIDA) litaendelea kuisaidia Tanzania kujikwamua kiuchumi hususani kwenye viwanda kupitiakazi za kitaaluma kupitia Shirika hilo.

Akizungumza katika mkutano huo wa mwaka wa Wadau wa Tafiti kwa Maendeleo shirikishi Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Cuthbert Kimambo amesema ni dhahiri kuwa nchi ya Sweden imekuwa na mshusiano na ushirikiano mzuri na Tanzania katika sekta ya Elimu, na kupitiamradi huo unaojumuisha UDSM, ni hatua nzuri yakuisaidia serikali na wananchi kwa ujumla kufanyashughuli zao kitaalamu na kufikia Tanzania ya viwanda ifikapo 2025.


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Leonard Akwilapo akiangalia na kupata maelezo kuhusu ufugaji wa samaki mara baada ya kufungua mkutono wa Kwanza wa mwaka wa wadau wa tafiti kwa maendeleo shirikishi uliofanyika jijini Dar esSalaam.

Mkutano huo wa siku mbili unaofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) unawashirikishawatunga sera, wadau kutoka sekta ya umma na binafsi.


Jumatano, 14 Novemba 2018

WAZIRI NDALICHAKO AZINDUA MWONGOZO NA MASHINDANO YA UBUNIFU


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako leo amezindua mwongozo na mashindano ya ubunifu kitaifa mkoani Dodoma.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi Waziri Ndalichako amesema lengo la mashindano hayo ni kutambua na kuendeleza fikra za wabunifu kwa lengo la kuongeza ajira.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge na Huduma za Maendeleo ya Jamii Peter Serukamba Mwongozo wa ubunifu mara baada ya kuuzindua leo Jijini Dodoma.



Prof. Ndalichako amesema katika kuimarisha uchumi wa viwanda lazima matumizi ya Sayansi, Teknolojia na ubunifu yaimarishwe kwa lengo la kuongeza tija viwandani na kwenye biashara.

“Kutoka na umuhimu wa mashindano haya naielekeza Idara ya Sayansi, Teknolojia na ubunifu kuhakikisha mashindano haya yanafanyika kila mwaka, ili kukuza ujuzi, wabunifu kwa maendeleo ya viwanda,” alisisitiza Waziri Ndalichako.
Waziri Wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge na Huduma ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba wakionesho mwongozo wa Ubunifu mara baada ya Kuzinduliwa leo Jijini Dodoma.

Mashindano hayo yameshirikisha Makundi mbalimbali ya kijamii zikiwemo Shule za Sekondari, Vyuo vya Ufundi Stadi, Sekta isiyo rasmi, Vyuo vya ufundi wa Kati, Vyuo vya Elimu ya Juu na Taasisi za utafiti na Maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa kuzinduliwa kwa mwongozo huo ni jambo kubwa na la kihistoria ikizingatiwa kuwa nchi inaelekea kwenye uchumi wa viwanda.
 Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakifurahia mara baada ya Mwongozo na Mashindano ya Ubunifu Kuzinduliwa leo Jijini Dodoma.


Serukamba amesema bila Sayansi, Teknolojia na ubunifu nchi haiwezi kufanikisha malengo yake, hivyo ameiomba Serikali ihakikishe inawekeza fedha nyingi.

“Kama hatutawekeza fedha za kutosha kwenye Sayansi, Teknolojia na Ubunifu hatuwezi kufanya kitu, hivyo tuwekeze fedha za kutosha ili tujiletee Maendeleo kwa haraka,” amesema Mhe. Serukamba.

Kauli mbiu ya mashindano hayo ni “Kukuza Ujuzi na Ubunifu kwa Uchumi wa Viwanda.”
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi mmoja wa Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Dodoma Mwongozo wa Ubunifu mara baada ya kuuzindua leo Jijini Dodoma.

Jumamosi, 10 Novemba 2018

WAZIRI NDALICHAKO AVITAKA VYUO KUFUATA MIONGOZO KATIKA KUTOA ELIMU



Serikali imevitaka vyuo vyote vya Elimu ya Juu nchini kuzingatia kanuni na miongozo  inayotolewa na Baraza la Taifa la Ufundi (NACTE) na Tume ya vyuo  Vikuu Nchini (TCU) katika kutoa elimu ili kuepuka  kufungiwa au kufutiwa udahili.

Kauli hiyo ya serikali   imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi naTeknolojia Prof. Joyce Ndalichako katika mahafali ya 53 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam, ambapo amesema serikali kupitia TCU na NACTE itaendelea kusimamia ubora wa Elimu na kuvifungia vyuo vyote vinavyotoa elimu chini ya kiwango.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika maandamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam.

Waziri Ndalichako amesema kuna baadhi ya Vyuo ambavyo vimekuwa havifuati taratibu na miongozo inayotolewa na TCU na NACTE na kusababisha usumbufu kwa wanafunzi pale vinapotakiwa kufungiwa, na kusisitiza kuwa hatua zinazochukuliwa na Taasisi hizo  ni endelevu na kuwa lengo ni kuhakikisha wahitimu wanapata Elimu bora itakayowawezesha kujiajiri ama kuajiriwa.

 Waziri Ndalichako pia amewataka Wahadhiri wenye tabia yakuficha matokeo ya wanafunzi kwa madai ya kukosa maslahi yao kutoka kwa mwajiri  kuacha mara moja tabia hiyo kwani imekuwa ikiwasumbua wanafunzi ambao hawana hatia.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na wahitimu katika mahafali ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam amewataka kuwa wanafunzi kuwa mabalozi wazuri na wazalendo katika kazi zao baada  ya kuajiriwa ama kujiajiri.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha CBE Prof. Emanuel Mjema amesema chuo hicho kinakabiliwa na changamoto ya uvhakavu wa miundombinu kutokana na Chuo hicho kuwa  cha muda mrefu,  hivyo Marion a serikali kukipatia udhamini ili kiweze kukopa katika Taasisi za fedha ili kuboresha miundombinu hiyo.




Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimbalisha  mmoja wahitimu wa Shahada ya Uzamili ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Maendeleo katika mahafali ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam.

Ijumaa, 2 Novemba 2018

SERIKALI KUTOA MWONGOZO WA USAMBAZAJI KOMPYUTA SHULENI


Serikali imesema inatarajia kutoa mwongozo wa utaratibu wa kusambaza kompyuta na vifaa vyake katika shule za msingi na sekondari ili kuwezesha vifaa hivyo kutambuliwa ikiwa ni pamoja na kuwa na takwimu sahihi  kwa shule ambazo  zitakuwa zimepatiwa vifaa hivyo.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe jijini Dar es Salaam wakati akifunga mafunzo ya TEHAMA yaliyofadhiliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) ambapo amesema kwa sasa ni vigumu kwa serikali kujua ni shule ngapi zenye kompyuta ama taasisi zinazotoa misaada ya kompyuta shuleni.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akizungumza na washiriki wa mafunzo ya TEHAMA (hawapo Pichani) wakati wa kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam ambapo amewataka washiriki hao kutumia maarifawaliyoyapata katika kuboresha Elimu
“Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itakaa pamoja na Ofisi ya Rais Tawalaza Mikoa na Serikali za Mitaa ili tuweze kuweka mwongozo ambao utawezesha serikali kutambua taasisi zote zinazojishughulisha na usambazaji wa kompyu takatika shule pamoja na kutambua shule zilizo na kompyuta ili iwe rahisi kuziratibu”amesema Prof. Mdoe.

Akizungumza na Walimu walioshiriki mafunzo hayo amewataka kuhakikisha wanatumia  maarifa waliyoyapata katika kuboresha elimu na kuimarisha utendaji  wa kazi  ili kuinua Ubora wa Elimu hapa nchini.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Pius Joseph amesema mfuko wa Mawasiliano kwa wote ina jukumu la  kuhakikisha ina ziunganisha shule zote za msingi na sekondari katika mtandao wa inteneti, pamoja na kutoa vifaa na mafunzo kwa walimu wanaofundisha masomo ya TEHAMA .

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akimkabidhi cheti cha kumaliza mafunzo ya TEHAMA mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

 Mfuko  huo wa Mawasiliano tayari umetoa  mafunzo yaTEHAMA kwa  walimu 578 kutoka mikoa yote ya Tanzania pia umetoa kompyuta 425 kwa shule za msingi,  komputa 1250 kwa shule za sekondari  na kuwa vifaa hivyo vimetolewa katika  kipindi cha mwaka 2015 hadi 2018.