Jumanne, 27 Novemba 2018

RAIS MAGUFULI AZINDUA MAKTBA YA KISASA KATIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI.

Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli leo amezindua Maktaba ya kisasa kwa ukanda wa Afrika Mashariki iliyopo katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) iliyojengwa kwa thamani ya dola milioni 41 Sawa na fedha za Kitanzania shilingi bilioni 90.

Akizungumza jijini Dar es salam wakati wa hafla ya kuzindua Maktaba hiyo iliyojengwa kwa msaada wa Serikali ya China Rais Magufuli amempongeza mkandarasi alyojenga Maktaba hiyo kwa kukamilisha mradi kwa wakati na kwa kiwango Cha juu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli akizindua jengo la Maktaba ya kisasa katika Chuo kikuu cha Dar es salaam ambapo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako na balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Wang Ke walishiriki uzinduzi huo.

Rais Magufuli pia ameishukuru serikali ya China kwa kuwa marafiki wa kweli kwa nchi ya Tanzania Kwa kutoa  msaada wa ujenzi wa maktaba hiyo pamoja na misaada mingine ya Maendeleo bila masharti yeyote.

“Tutaendelea kuenzi mahusiano mazuri yaliyoanzishwa na waasisi wa serikali hizi mbili ambazo ni Tanzania na China, na kuwa kuwepo kwa mahusiano kumekuwa na tija katika Kujiletea Maendeleo na kuwa misaada imekuwa ikitokewa bila masharti yoyote,” alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli katika hotuba yake amekitaka Chuo Kikuu kuendelea kusimamia maadili, heshima ya Chuo kikuu na kuhakikisha Elimu inayotolewa ni ya  viwango ili kulinda hadhi ya Chuo hicho.

Rais John Magufuli akikabidhiwa mfano wa ufunguo na balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Wang Ke kwa ajili ya kufungulia maktaba ya kisasa ambayo amezindua leo katika Chuo kikuu cha Dar es salaam, jijini Dar es salaam.

Rais Magufuli pia amewataka  wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na wale wa nje ya Chuo kuhakikisha wanaitunza maktaba hiyo ili idumu na iweze kutumiwa na vizazi vijavyo.

Akizungumza katika uzinduzi huo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amezitaka Taasisi za Elimu ya Juu kuacha kutumika kama vichaka vya kuvunja sheria na kufanya ubadhirifu wa fedha za Umma.

“Tunazitaka  Taasisi zote za Elimu ya Juu kuhakikisha zinakuwa ni  mfano wa kuigwa na siyo kuwa mstari wa mbele katika kushiriki vitendo vya ubadhirifu, na kuwa watumishi wa Taasisi hizo  ni watumishi wa Umma na kama walivyo watumishi wengine na kuwa yeyeote atakyekwenda kinyume Sheria itachukua Mkondo wake,” alisisitiza Waziri Ndalichako.
Viongozi waandamizi wa Serikali kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za serikali wakifuatilia uzinduzi wa maktaba ya Kisasa ya UDSM jijini Dar es salaam, maktaba hiyo imejengwa kwa msaada wa Serikali ya china kwa gharama ya shilingi bilioni 90.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu hicho Prof. William Anangisye amesema Maktaba ni chombo muhimu katika kujiendeleza na kuwa maktaba hiyo ya kisasa itatumiwa na wafunzi pamoja na watafiti mbalimbali katika kujiongezea maarifa.

Rais John Magufuli akimshukuru balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Wang Ke kwa kufanikisha ujenzi wa maktaba ya kisasa iliyojengwa katika Chuo kikuu cha Dar es salaam

Jumatatu, 26 Novemba 2018

TANZANIA NA CHINA ZATILIANA SAINI KUANZA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA


Serikali ya Tanzania na ile ya Jamuhuri ya watu wa China leo zimetiliana  saini makubaliano ya kuanza kwa ujenzi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) ambacho kinatarajiwa kujengwa mkoani Kagera na kuwa ujenzi huo unatarajiwa  kukamilika mwaka 2020

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leornald Akwilapo ndiye aliyesaini mkataba huo kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na  kwa upande wa China mkataba huo umesainiwa na Mwakilishi wa Uchumi na Biashara nchini Tanzania Yuan Lin na kuwa tukio hilo limefanyikia jijini Dar es salaam.


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leornald Akwilapo pamoja na Mwakilishi wa Uchumi na Biashara nchini Tanzania Yuan Lin wakitia saini  mkataba wa makubaliano wa ujenzi wa chuo cha VETA kinachotarajiwa kujengwa mkoani Kagera na ujenzi wake  unatarajiwa kukamilika mwaka 2020.

Mara baada ya kusaini mkataba huo Dkt. Akwilapo amesema kuwa Chuo hicho kitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 400 wa kozi za muda mrefu na wanafunzi  1000 wa kozi za muda.

Miundombinu itakayojengwa katika chuo hicho ni pamoja na vyumba vya madarasa, Karakana za Kufundishia, Majengo ya Utawala, mabweni  na Viwanja vya michezo na kuwa mpaka kukamilika kitagharimu zaidi ya shilingi bilioni 22.

 Dkt. Akwilapo amewataka wakandarasi  wanaopewa mikataba ya ujenzi na Wizara yake kuhakikisha wanatekeleza makubaliana ya mikataba hiyo kwa wakati  na kwamba serikali haitasita kuvunja mkataba wowote ambao unatekelezwa kinyume na makubalino ikiwa ni pamoja na  kuchukulia hatua za kisheria kwa kwenda kinyume na mikataba hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leornald Akwilapo pamoja na Mwakilishi wa Uchumi na Biashara nchini Tanzania Yuan Lin wakibadilisha hati za mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa chuo cha VETA kinachotarajiwa kujengwa mkoani Kagera.



Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu amesema Chuo hicho kitasaidia kuongeza udahili wa wanafunzi katika fani mbalimbali za VETA kutokana na ukweli kwamba mkoa huo ni mkubwa na kuwa hapo awali ulikuwa na chuo cha VETA kimoja kinachojulikana kama Rwamishenye ambacho kilikuwa kidogo.

Naye Mwakilishi wa China anayeshughulikia masuala ya Uchumi na Biashara nchini Tanzania Yuan Lin amesema Serikali ya Tanzania na China zimekuwa marafiki kwa muda mrefu na ndio maana China imeona umuhimu wa kusaidia ujenzi wa chuo hicho ikiwa ni hatua ya kuunga mkono Juhudi za Serikali ya awamu ya Tano ya kuwa nchi ya uchumi wa viwanda hadi ifikapo mwaka 2020.

Katibu Mkuu Waizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leornald Akwilapo akisoma mkataba wa makubaliano wa ujenzi wa chuo cha VETA kinachotarajiwa kujengwa mkoani Kagera.

Jumamosi, 24 Novemba 2018

WAZIRI NDALICHAKO ASEMA AFRIKA ITAENDELEZWA NA WAAFRIKA WENYEWE


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema wajibu wa kuiendeleza Afrika uko mikononi mwa Waafrika wenyewe huku jukumu la wadau wengine wa Maendeleo ni  kusaidia kukua kwa Maendeleo hayo.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo Leo katika Mahafali ya Programu za ESAMI yaliyofanyika katika Makao Makuu ya ESAMI jijini Arusha ambapo amesisitiza kuwa  Waafrika wanapaswa kujisimamia wenyewe katika nyanja za Kijamii na Kiuchumi  kwa lengo la kutimiza malengo ya bara hilo.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu wa kozi za ESAMI katika Mahafali yaliyofanyika jijini Arusha

“ Ili Afrika iweze kuendelea lazima ijisimamie yenyewe katika masuala ya kijamii na kiuchumi na hii itawezekana tu kupitia   vijana ambao wameandaliwa  vyema na wakawa tayari kuhakikisha wanaliendeleza bara la Afrika kwa ujasiri bila kuhofia changamoto watakazokutana nazo,” alisisitiza Waziri Ndalichako

Kiongozi huyo amesema bara la Afrika linahitaji Viongozi wenye ujasiri, ambao wapo tayari kuhakikisha Afrika inakwenda mbele kiuchumi na Kijamii.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika maandamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya Programu za ESAMI yaliyofanyika katika Makao Makuu ya ESAMI jijini Arusha

Akizungumza katika mahafali hayo Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI Prof. Bonard  Mwape amesema wahitimu wote wameandaliwa vyema kwenda kuleta Mabadiliko  na Maendeleo katika nchi zao pamoja na kuhakikisha  bara la Afrika linakuwa  lenye maendeleo.

Mahafali hayo yamejumuisha zaidi ya wahitimu 360 kutoka nchi za Afrika ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Namibia, Mali, Malawi DR- Congo, Burundi, Zimbambwe na wenyeji Tanzania.

Baadhi ya wahitimu wa kozi mbalimbali wakimsikiliza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia (Hayupo Pichani) wakati wa mahafali wakati wa mahafali ya Programu za ESAMI yaliyofanyika katika Makao Makuu ya ESAMI jijini Arusha

Ijumaa, 23 Novemba 2018


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY


Tender No. ME-024/2016-17/HQ/G/36

For

SUPPLY OF VARIOUS GOODS FOR EDUCATION SUPPORT RESOURCE AND ASSESSMENT CENTRE (RETENDERED)

Invitation for Tender

Date: 26th November, 2018
  1. This Invitation for Tender follows the General Procurement Notice for this Project which appeared in Daily News and Procurement Journal Issue no. 1768 dated 16th October, 2016.

  1. The Government of Tanzania through Ministry of Education, Science & Technology has received a Grant from the Global Partnership for Education (GPE) towards the cost of Literacy & Numeracy Education Support (LANES) and it intends to apply part of the proceeds of this Grant to cover eligible payments under the contract for the supply of various goods for Education Support Resource and Assessment Centre.

  1. The Permanent Secretary, Ministry of Education, Science & Technology now invites sealed tenders from eligible suppliers as tabulated below:

Lot
Description of Items
Qty
Delivery Period (after contract signing)
1
Office equipment
Various
Within 12 weeks
2
Intellectual- Toys (Teaching Materials)
Various
Within 12 weeks
3
Stationery & related Supplies
Various
Within 4 weeks
4
Specialized Equipment( Intellectual and Hearing Equipment)
Various
Within 12 weeks
5
Cleaning Materials
Various
Within 4 weeks
6
Visual Impairment Items
Various
Within 4 weeks

       Tenderers are required to quote for one lot or combination of two, three, four, five or all lots but in any case Tenderers are required to quote for all items and quantities specified in each lot.  Tenderers who do not quote for all items and quantities will be considered non responsive and rejected in evaluation.

  1. Tendering will be conducted through the National Competitive Tendering procedures specified in the Public Procurement Regulations, 2013 – Government Notice No. 446 and are open to all Tenderers as defined in the Regulations.
  2. Interested eligible Tenderers may obtain further information from and inspect the Tendering Documents at the office of the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 40479Dodoma, Office number 320 from 0900 to 1500 hours on Mondays to Fridays inclusive except on public holidays.

  1. A complete set of Tendering Document (s) in English and additional sets may be   purchased by interested Tenderers on the submission of a written application to the address given under paragraph 5 above and upon payment of a non-refundable fee of Tzs. 100,000/= (Tanzania Shillings: One hundred Thousand Only), Payment should be done through Government e- Payment Gateway (Gepg) where the tenderer should get Control number at office No. 327, at Ministry of Education, Science and Technology.

7.       Tenders for Lots 1, 2 & 4 must be accompanied by a Tender Security in an acceptable form in the amount of TZS. 20,000,000.00 (Tanzanian shillings Twenty million).

8.       Tenders for Lots 3, 5 & 6 must be accompanied by a Tender Securing Declaration in a format provided.

  1. All tenders in one original plus two copies properly filled in, and enclosed in plain envelopes must be delivered to the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 – 40479 Dodoma, Room 320 at or before 10:30am local hours on Tuesday, 11th December, 2018. Tenders will be opened promptly thereafter in public and in the presence of Tenderers’ representatives who choose to attend in the opening at the Conference Room, Ground Floor, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 40479Dodoma.

10.   late Tenders, Portion of Tenders, Electronic Tenders, Tenders not received, Tenders not opened and not read out in public at the tender opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.





PERMANENT SECRETARY,
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE & TECHNOLOG
University of Dodoma (UDOM), Block No. 10, P.O. Box 10 40479 DODOMA



OLE NASHA: SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA WAHISANI KATIKA SEKTA YA ELIMU


Serikali imesema inatambua mchango wa wahisani na wadau wa Elimu katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya Tano katika kuendelea kuchangia ujenzi wa mabweni ya Wanafunzi wa kike, ujenzi wa vyumba vya madarasa, ununuzi wa vifaa vya TEHAMA pamoja na ununuzi wa vifaa vya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.William Ole Nasha wakati akitunuku hati za utambuzi kwa Wahisani na Wadau ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuchangia Miradi ya Elimu kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwenye hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akimkabidhi hati ya utambuzi kwa mchangiaji wa Miradi ya Elimu Kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo Naibu Waziri Ole Nasha amewahakikishia wahisani hao usalama wa fedha zao na kuwa zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo.

“Niwahakikishie kuwa Serikali inatambua mchango wenu katika kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuchangia Elimu, ikiwa ni pamoja na kuchangia ujenzi wa mabweni ya Wanafunzi wa kike, ujenzi wa vyumba vya madarasa, ununuzi wa vifaa vya TEHAMA pamoja na ununuzi wa vifaa vya wanafunzi wenye mahitaji maalum,”

“Pia fedha zilizotolewa na Taasisi zenu zitatumika kama zilivyokusudiwa na si vinginevyo na endapo itabainika kuwepo kwa matumizi ambayo siyo sahihi basi Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria kwa wale wote watakaobanika kwenda kinyume na maelekezo”alisisitiza Naibu Waziri Ole Nasha.
Wachangiaji wa Miradi ya Elimu kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknlojia Mhe. William Ole Nasha  mara baada ya wahisani hao kutunukiwa hati za utambuzi.

Jumla ya Taasisi 18 za ndani na nje ya nchi zilitunukiwa hati baada ya kuchangia takribani Shilingi  bilioni 11  ambazo zimetumika kuboresha Miundombinu mbalimbali ya Elimu.

Alhamisi, 22 Novemba 2018


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Anuani ya simu “ELIMU”
Simu: 026 296 35 33
Baruapepe:info@moe.go.tz
Tovuti: www.moe.go.tz


  
Chuo cha Masomo ya Biashara na Sheria,
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Jengo Na. 10,
S. L. P. 10,
40479 DODOMA.           

TAARIFA KWA UMMA

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inaufahamisha umma kuwa taarifa zinazosambazwa na Mtandao wa Programu ya Wanafunzi Tanzania (TSNP) kwenye mitandao ya kijamii zinazoelezea kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Semina ya Kuwajengea Uwezo Viongozi wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania siyo sahihi.

Kwa mujibu wa taarifa inayosambaa semina hiyo imepangwa kufanyika Desemba 1, 2018 katika ukumbi wa Kisenga uliopo katika Jengo la LAPF Kijitonyama, Jijini Dar es salaam.

Mhe. Waziri hajapokea mwaliko rasmi kutoka kwenye Mtandao huo hivyo hatarajii kushiriki semina hiyo, pia katika tarehe tajwa atakuwa na majukumu mengine kwa mujibu wa ratiba yake.

Wizara haina taarifa ya mwaliko au ushiriki wa kiongozi mwingine yeyote wa ngazi ya Wizara.
Imetolewa na;
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
22/11/2018

Jumatatu, 19 Novemba 2018

SERIKALI YAJENGA SEKONDARI YA MFANO KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI ARUSHA


Serikali inajenga  Shule ya Sekondari Maalum ya mfano kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Chuo cha Ualimu Patandi kilichopo mkoani Arusha yenye uwezo wa kudahili wanafunzi 600 kwa mara moja ikiwa ni mkakati wake wa kuongeza fursa za udahili kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kwa Mkoa wa Kilimanjaro, ambapo amesema Serikali imekarabati miundombinu kwenye shule kongwe ya Moshi Ufundi inayopokea wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimpongeza mwanafunzi mwenye mahitaji maalum baada ya kufanya vizuri katika maonyesho ya mavazi katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kwa Mkoa wa Kilimanjaro

 “Serikali inaendelea kutekeleza mipango mbalimbali inayolenga kuongeza upatikanaji wa fursa na kuimarisha ubora wa elimu inayotolewa katika ngazi zote kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambapo tayari serikali imekarabati miundombinu ya shule kongwe ya Moshi Ufundi ambayo inapokea wanafunzi wenye mahitaji maalumu”. Alisisitiza Prof. Ndalichako.

Waziri Ndalichako amesema watu wenye mahitaji maalum wana fursa sawa ya kushiriki katika michezo na kufanya hivyo kunasaidia kuondoa kasoro za kimwili na kiakili na baadhi ya ulemavu unaweza kurekebishwa kwa kushiriki katika michezo na burudani.
Prof Ndalichako amesisitiza kuwa ushiriki katika michezo, hususan kwa watoto wenye mahitaji maalum ni muhimu sana kama ilivyowekwa bayana katika kifungu cha 52 cha Sheria ya Watu wenye Ulemavu Namba 9 ya mwaka 2010 kinachosisitiza umuhimu wa Watu wenye ulemavu kushiriki katika michezo, starehe na burudani.

Akizungumza katika Bonanza hilo Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Walemavu) Stella Ikupa amewataka wanafunzi wenye mahitaji maalum kuunga mkono juhudi za serikali ya Awamu ya Tano kwa kuendelea kujitambua, kujikubali na kujituma ili kujikwamua katika changamoto wanazokutana nazo katika masomo yao.
Waziri Ikupa amewataka wanafunzi hao pia kujiunga na vyuo vya ufundi ambavyo vitawawezesha kupata satadi ambazo watazitumia kwa ajili ya  kujiari wenyewe badala ya kuwa tegemezi.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akibadilishana mawazo na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Walemavu) katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kwa Mkoa wa Kilimanjaro

Naye Mratibu wa Bonaza hilo ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (Vyuo Vikuu) Esther Mmasi amesema wakati wa  maandalizi ya Bonanza hilo amebaini kuwepo kwa uhaba wa viwanja vya michezo katika shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambapo ameiomba serikali kuhakikisha inaboresha miundominu ili kuwajengea uwezo wanafunzi hao.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na wadau wa Elimu pamoja na wanafunzi wenye mahitaji maalum ( Hawapo Pichani) katika ufunguzi wa Bonanza la Kilimanjaro Committee for Sports iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro.