Jumatano, 13 Februari 2019


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY


Tender No. ME-024/2018-19/HQ/G/05


For

SUPPLY OF SPECIAL NEEDS MATERIALS (TESP)

Invitation for Tender

Date: 13th February, 2019
1.       This Invitation for Tenders follows the General Procurement Notice (GPN) which appeared on PPRA website online on 02nd October, 2018.

2.       The Ministry of Education, Science & Technology has received a grant from the Global Affairs Canada (GAC) towards the cost of Teacher Education Support Project, and it intends to apply part of the proceeds of this grant to cover eligible payments under the contract for Supply of Special Needs Materials.

3.       Tendering will be conducted through the National Competitive Tendering procedures specified in the Public Procurement Regulations, 2013 – Government Notice No. 446 as amended in 2016 and are open to all Tenderers as defined in the Regulations.
4.       Interested eligible Tenders may obtain further information from and inspect the Tendering Documents at the office of the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 1040479Dodoma, Office number 320 from 0900 to 1500 hours on Mondays to Fridays inclusive except on public holidays.

5.       A complete set of Tendering Document (s) in English and additional sets may be   purchased by interested Tenderers on the submission of a written application to the address given under paragraph 4 above and upon payment of a non-refundable fee of Tzs. 100,000/= (Tanzania Shillings: One hundred Thousand Only), Payment should be done through Government e-Payment Gateway (Gepg) where the tenderer should get Control number at Ministry of Education, Science and Technology, Room No. 327.

6.       All Tenders must be accompanied by a Tender Security in an acceptable form in the amount of TZS. 5,000,000.00 (Tanzanian shillings Five million) be in the form of a Bank Guarantee in the format provided in section IX.

7.       All tenders in one original plus two copies properly filled in, and enclosed in plain envelopes must be delivered to the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 - 40479Dodoma, Room 320 at or before 10:30HRS, on 22nd February, 2019. Tenders will be opened at 10:45 hrs in public and in the presence of Tenderers’ representatives who choose to attend in the opening at the Conference Room, Ground Floor, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 40479Dodoma.

8.       Late Tenders, Portion of Tenders, Electronic Tenders, Tenders not received, Tenders not opened and not read out in public at the tender opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.


PERMANENT SECRETARY,
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE & TECHNOLOGY
University of Dodoma (UDOM), Block No. 10, P.O. Box 10   40479 DODOMA.


WAZIRI NDALICHAKO AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI ALIYEKUWA MKUU WA CHUO CHA UALIMU ILONGO NA WATUMISHI WENGINE WAWILI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Leonard Akwilapo kumvua madaraka na kumsimamisha kazi Benjamini Mwilapwa aliyekuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Ilonga kabla ya kuhamishiwa Chuo cha Ualimu Mpwapwa  kwa kushindwa kusimamia ukarabati  Chuoni hapo.

Waziri Ndalichako pia amemuagiza Dkt. Akwilapo kuwasimamisha kazi watumishi wengine akiwemo afisa manunuzi na ugavi Ally Masanja na Muhasibu Godlove Yona ambao ni watumishi wa chuo hicho ili kupisha uchunguzi kwa kile kinachodaiwa kufanya manunuzi yasiyofuata taratibu na kulipa fedha kwa kazi ambazo hazijakamilika.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akikagua miundombinu ya ujenzi wa mabweni katika Chuo cha Ualimu Ilonga kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Waziri Ndalichako ametoa maagizo hayo  mkoani Morogoro  alipofanya ziara chuoni hapo ya kukagua maendeleo ya ujenzi, na uboreshaji wa miundombinu inayofanywa na Wizara hiyo.

Amesema ukarabati uliofanyika hauridhishi huku aliyekuwa Mkuu wa Chuo hicho ambae ndie  alikuwa mwenyekiti wa kamati za ujenzi na manunuzi  chuoni hapo kuwa  mtoa maamuzi ya mwisho bila kujali kufuata  sheria ya manunuzi inayoelekeza unapotumia Force Akaunti unatakiwa kuwa na kamati aina gani na majukumu yake ni yapi. 

“Inaonekana Mkuu wa Chuo alipora madaraka, ninafahamu kuwa amehamishiwa Chuo cha Ualimu Mpwampwa  sasa namuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia amrudishe na avuliwe madaraka mara moja, haiwezekani mtu akapandishwa cheo wakati Chuo hiki ambacho ni kidogo kilimshinda kusimamia ukarabati”, alisisitiza Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiangalia sakafu ya moja ya bweni lililokarabatiwa lakini bado imeonesha kuchakaa kwa muda mfupi.

Aliongeza kuwa kazi zilizofanyika za ukarabati chuoni hapo niza ubabaishaji na kwamba zimefanyika chini ya kiwango, akitolea mfano sakafu kwenye majengo yote kuonesha nyufa, huku nyongeza ya gharama za ukarabati zikiwa kubwa.

Pia Waziri Ndalichako amemtaka Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) Profesa Joseph Msambichaka kufika katika Chuo Cha Ualimu Ilonga  siku ya  kesho , February 13, 2019 kuona namna wataalamu wa taasisi hiyo  walivyoshindwa kusimamia kazi waliyokabidhiwa kwao ambao ni  washauri elekezi.

Pia amemtaka Katibu Mkuu kuvisimamia kwa karibu vyuo vya ualimu kwa  kuwa sasa vimeanza kuwa kama vichaka ambapo michango haifuati utaratibu ikiwa  ni pamoja na kuitaka timu  ya wakaguzi wa wizara  waliofika chuoni hapo kufanya uchunguzi wa kina   kwa sababu inaelekea kuna mahali pengine nyaraka zilikuwa zinaghushiwa.
Muonekano wa Jengo la Utawala lililokarabatiwa katika Chuo cha Ualimu Ilonga kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameiomba wizara kama iliyo katika miradi  mingine inayotekelezwa na Serikali katika Wilaya hiyo kuhakikisha wanawahirikishwa kwa karibu ili waweze kusimamia kile kinachotekelezwa katika eneo husika.
Zaidi ya Shilingi bilioni moja zimetolewa na Serikali kukarabati Chuo cha Ualimu Ilonga kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.

Jumatatu, 11 Februari 2019


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

STUDY OPPORTUNITY TENABLE IN THE UNITED STATE OF AMERICA FOR ACADEMIC YEAR 2019

1.0 Call for Application
The general Public is hereby informed that, the United States Embassy Public Affairs’ Section  is now accepting application for 2020 Fulbright Foreign Student Programme  to pursue Master`s and Doctorates Degrees offered in the US Universities for the academic year 2019.

U.S. Embassy encourages candidates with disabilities to apply as special accommodations are available.

2.0 Mode of Application
Applications must be submitted online using the Embark Visiting Scholar system, accessible at https://apply.iie.org/ffsp2020The submission deadline for applications is April 5, 2019. For more information, please email drs_exchanges@state.gov.

Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business Studies and Law,
Universities of Dodoma (UDOM) Building No. 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.

Alhamisi, 7 Februari 2019

DKT. AKWILAPO AZINDUA DIRISHA LA SOMO LA KIFARANSA KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amezindua dirisha la taarifa za kimasomo katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam litakalowapa fursa wanafunzi na wadau hasa wa somo la lugha ya kifaransa kupata taarifa mbalimbali kuhusiana na fursa za masomo zinazopatikana nchini Ufaransa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akijadiliana jambo na Balozi wa Ufaransa Mhe. Frederic Clavier wakati wa hafla ya uzinduzi wa dirisha la taarifa za kimasomo katika Chuo Kikuu Cha Dar es salaam litakalowapa fursa wanafunzi na wadau hasa wa somo la lugha ya kifaransa kupata taarifa kuhusiana na fursa za masomo nchini Ufaransa.

Kituo hicho kitawawezesha wanafunzi na wadau wengine kuingia katika mfumo wa kompyuta na kupata taarifa hizo hasa za kimasomo, aina za kozi, na vyuo vilivyopo nchini humo kwa ajili ya kujiunga.

“Ufaransa wanataka kuwa moja ya mataifa yanayoongoza kwa kukaribisha wanafunzi wengi wa kigeni nchini mwao, kwa sasa wanashika nafasi ya nne ili kufikia lengo la kushika nafasi ya kwanza wameanzisha kampeni inaitwa STUDY in FRANCE ambapo ifikapo 2027 wanatarajia kuwa na idadi ya wanafunzi wa kigeni laki 5 wanaotoka katika nchi mbalimbali,” alisema Dkt. Akwilapo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa dirisha la taarifa za fursa za kimasomo zinazopatikana nchini Ufaransa. Dirisha hilo limezinduliwa katika Chuo Kikuu Cha Dar es salaam jijini Dar es Salaam.

Kwa sasa nchi ya Ufaransa ina wafunzi wasiozidi elfu 25,000 hivyo kupitia dirisha hilo kutasaidia wadau kupata  taarifa kwa haraka zaidi  kupitia dirisha hilo la kuaminika.

Kwa maelezo zaidi kuhusu namna ya kujiunga na masomo nchini Ufaransa fika katika Ofisi zao zilizopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akisalimiana na Viongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na wawakilishai kutoka ubalozi wa Ufaransa wakati alipowasili chuo hapo kuzindua dirisha la taarifa za fursa za kimasomo zinazopatikana nchini Ufaransa.

Jumatano, 6 Februari 2019

KITENGO CHA MANUNUZI WIZARA YA ELIMU CHATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUFUATA SHERIA NA KANUNI ILI KUEPUKA HOJA ZA MKAGUZI MKUU

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe amekitaka Kitengo cha Manunuzi na Ugavi cha Wizara hiyo kuhakikisha kinafanya kazi zake kwa kufuata sheria na kanuni za manunuzi ili kukwepa hoja za ukaguzi ambazo zimekuwa zikiripotiwa na ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali   (CAG).

Prof. Mdoe ametoa agizo hilo mkoani Morogoro wakati wa  ufunguzi wa kikao kazi kinachowahusisha wajumbe wa bodi ya manunuzi, Idara ya   manunuzi , kitengo cha ukaguzi wa ndani  na kitengo Cha sheria kutoka Wizara hiyo  lengo likiwa ni kuimarisha Kitengo cha manunuzi kuondokana na hoja za wakaguzi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Dkt. Leonard Akwilapo, Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe na Mkurugenzi wa Idara ya Manunuzi na  Ugavi Hirtudice Jisenge wakifuatilia mada inayotolewa wakati wa Kikao Kazi cha wajumbe wa bodi ya manunuzi, maafisa manunuzi, kitengo Cha wakaguzi wa ndani na kitengo Cha Sheria cha kuwajengea uwezo kuhusu kanuni na sheria za manunuzi.


Naibu Katibu Mkuu huyo amewaeleza washiriki wa mafunzo hayo kuwa Kitengo hicho kimekuwa na shughuli za manunuzi ambazo zinatumia kiasi kikubwa cha fedha za serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa miundombinu ya vyuo na shule, hivyo ni muhimu kuimarisha shughuli za manunuzi ili kuokoa fedha ambazo zinaweza kupotea kwa kutofuatwa kwa taratibu.

"Wizara imekuwa na miradi mbalimbali ambayo inachukuakaribu asilimia 75 ya bajeti ya Wizara, hivyo mafunzo haya yanalenga kuwajengea uwezo washiriki ili waweze kutoa maamuzi sahihi manunuzi, pia  kuwakumbusha wajibu wao wa kufuata sheria na kanuni za manunuzi,”amesema Profesa Mdoe.
Washiriki wa kikao kazi Cha mafunzo ya Sheria za manunuzi wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi. Kikao kazi hicho kinafanyika mkoani Morogoro.

Akizungumzia umuhimu wa kikao kazi hicho,  Mkurugenzi wa Kitengo cha Manunuzi  wa Wizara hiyo Hirtudice Jisenge amesema mafunzo hayo yatawezesha Kitengo hicho kujipanga na  kufanya kazi kwa ufanisi.

Jumatatu, 4 Februari 2019

WAZIRI NDALICHAKO AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI WATUMISHI 6 CHUO CHA UALIMU PATANDI.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Leonard Akwilapo kuwasimamisha kazi watumishi 6 wa Chuo cha Ualimu Patandi kutokana na kushindwa kusimamia vyema ujenzi wa shule ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu inayojengwa Wilayani Arumeru mkoani ARUSHA.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Ave Maria Semakafu na watendaji wengine wakikagua hali ya ujenzi wa shule ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu inayojengwa katika Chuo Cha Ualimu Patandi mkoani ARUSHA.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo baada ya kukagua hali ya ujenzi unaoendelea wa vyumba vya madarasa, jengo la Utawala, na bwalo la chakula na kisha kuwa na kikao cha pamoja na watendaji wa Chuo hicho kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali ambayo yameripotiwa na Mkaguzi Mkuu wa ndani wa Wizara hiyo baada ya kufanyika ukaguzi wa mradi huo wa ujenzi.


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akimuonesha Waziri wa Elimu Prof. Ndalichako hatua za ujenzi wa shule ya wanafunzi wenye mahitaji Maalumu inayojengwa Patandi, shule hiyo ikikamilika itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 640.

Kufuatia hali hiyo, Waziri aliagiza kusimamiashwa kazi kwa  Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Issac Myovela, Afisa manunuzi Charles Njarabi, Mhasibu Rose Kijaka, M/Kiti wa kamati ya  mapokezi Peter Mosha na  Msimamizi wa ujenzi huo Israel Mayage.

Wengine ni aliyekuwa Afisa manunuzi wa Chuo hicho Henry Matei ambaye alihamishiwa Chuo cha Ualimu Monduli na kuwa Waziri ameelekeza arudishwe chuoni hapo na asimamishwe kazi mara moja.


Muonekano wa Jengo la Utawala la Shule ya Wanafunzi wenye mahitaji maalumu inayojengwa katika Chuo cha Ualimu Patandi.

Pia Waziri amemuagiza Katibu Mkuu Dkt. Akwilapo kumpunguzia majukumu ya kazi Mkuu wa Chuo cha Patandi Lyana Mbaji kutokana na kuwa ni mgonjwa na badala yake ateuliwe Mkuu mwingine aweze kuendelea na majukumu katika Chuo hicho.

Mpaka sasa tayari Wizara imekwishatoa kiasi cha shilingi Bilioni 2.3, mradi utakapokamika kiasi ha sh. 2.56 zitakuwa zimetumika.
Muonekano wa Bwalo la Wanafunzi wenye mahitaji maalumu linalojengwa katika Shule ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Chuo cha Ualimu Patandi, Arumeru mkoani Arusha.

DKT. AKWILAPO AMEWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA KUZNGATIA KANUNI, TARATIBU NA SHERIA ZA KAZI


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amewataka watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria za kazi pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Dkt. Akwilapo ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati wa mkutano wa pamoja na watumishi wa Wizara hiyo wenye lengo la kupitia utendaji kazi wa wizara kwa mwaka 2018 na kuweka malengo ya utekelezaji wa majukumu kwa mwaka 2019.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo (hawapo pichani), wakati akifungua mkutano wa pamoja uliofanyika Jijini Dodoma leo, ambao amewataka watumishi kufuata kanuni, taratibu na sheria za kazi pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa katika utekelezaji wa majukumu yao. 


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  kutoka  Idara na Vitengo wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Dkt. Leonard Akwilapo wakati wa mkutano wa pamoja wa Watumishi wa Wizara hiyo, mkutano huo umefanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu huyo pia amewataka watendaji wa Wizara hiyo kuendelea kuwahudumia wateja kwa lugha nzuri na kuhakikisha huduma zinatolewa katika muda muafaka kwa lengo la kuepusha malalamiko.

“Nichukue fursa hii kupitia mkutano wa wafanyakazi wote kuwataka kutekeleza majukumu yenu kwa kufuata taratibu na sheria za kazi pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa ili nchi iweze kufikia malengo ambayo imejiwekea. Kila mmoja atomize wajibu wake katika eneo lake naamini kwa kufanya hivyo tutafanikiwa,” alisisitiza Dkt. Akwilapo.

Watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Makao Makuu) wakiwa katika Mkutano wa pamoja ambapo Katibu Mkuu ameelekeza watumishi kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja na zitolewe katika muda muafaka.

Mkutano   wa pamoja wa Wafanyakazi wa Wizara hiyo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kujitathmini katika utekelezaji wa majukumu ambayo Wizara inakuwa imejiwekea.

Mkutano wa pamoja wa Viongozi na watumishi wa Wizara wenye lengo la kupitia utendaji kazi wa Wizara kwa mwaka 2018 na kuweka malengo ya utekelezaji kwa mwaka 2019.