Jumamosi, 25 Januari 2020

SHORT TRAINING COURSES SCHOLARSHIP TENABLE IN INDIA FOR THE ACADEMIC YEAR 2019/2020


Call for Application
The General Public is hereby informed that the Government of India through the Indian Technical and Economic Cooperation (ITEC), has granted a full funded scholarship to eligible Tanzanian to pursue Short courses at Indian Public Institutions for the academic year 2019/2020.

A directory of Host Training Institutions and the Training Calendar is available on the website of ITEC through www.itecgoi.in/stream_list.php. Containing a complete list of the Indian Public Institutions as well as specific information about them, including the conditions of access, the course and the duration of the studies. For more information about the programme visit the following link www.itecgoi.in/about.php.

How to apply
1.    Applicants are advised to apply for the current courses as indicated in ITEC training Calendar of 2019/2020;
2.    The applicants after applying online are required to forward the applications to the Embassy/High Commission of India in Tanzania  concurrently accredited for nomination; and
3.    Further, the applicants may later check the status of their applications by logging-in at www.itecgoi.in.

Eligibility
1.    Academic qualifications as laid down by the Institute for the course concerned;
2.    Officials in Government, Public  and Private sectors, Universities,
 Chambers of Commerce and industry, progressive farmers and Research;
3.    Candidate should possess adequate working experience on the related field;
4.    Age limit between 25 to 45 years; and
5.    Medically fit to undertake the training.

Issued by
Permanent Secretary,     
Ministry of Education, Science and Technology,
Mtumba Block,
Afya Street,
P.O.BOX 10,
40479 DODOMA.

Jumanne, 21 Januari 2020

TANGAZO LA KUJIUNGA NA VYUO VYA MAENDELEO YA WANANCHI


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatangaza nafasi za kujiunga katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) kwa mwaka 2020.
Sifa za Mwombaji ni mwananchi yeyote mwenye nia ya kupata ujuzi na maarifa mbalimbali.
Aina ya Mafunzo yanayotolewa ni:
1. MAFUNZO YA UFUNDI STADI- NGAZI YA I, II &III
  1. Ufundi Umeme wa Magari : (Ifakara, Katumba, Nzovwe, Rubondo, Same, Sofi, Kisangwa, Mto wa Mbu,Chala,Handeni, Ikwiriri, Karumo, Kilosa, Katumba, Kibondo, Kilwa Masoko, Kihiga, Mamtukuna, Malampaka, Kiwanda,Malya).
  1. Ufundi Mekanika, (Vyuo vyote vinavyofundisha Ufundi Magari).
  1. Ufundi Umeme wa Majumbani, (Vyuo vyote vinafundisha kozi hii).
  1. Ufundi  Magari : (Bigwa, Chala, Chilala, Handeni, Ifakara, Ikwiririri, Karumo, Kilosa, Kisarawe, Katumba, Kibondo, Kilwa Masoko, Kisangwa, Kihinga, Singida Mamtukuna, Malampaka, Malya, Masasi, Mbinga, Msinga, Mtawanya, Musoma, Mwanhala, Mwanva, Mto wa Mbu, Munguri, Nandembo, Newala, Ngara, Njombe, Nzega, Nzovwe, Rubondo, Same, Sengerema, Sofi, Urambo).
  1. Useremala: (Bariadi, Mtawanya, Chala, Chilala, Chisala, Handeni, Ifakara, Ilula, Ulembwe, Kiwanda).
  1. Uashi: (Vyuo vyote vinavyofundisha Uashi isipokuwa Mtowambu, Nzega, Ikwiriri, Buhangija, Kiwanda, Chilala, Bigwa na Sikonge).
  1. Ushonaji: (Vyuo vyote vinafundisha ushonaji isipokuwa, Arnatouglu, Handeni, Sofi).
  1. Upishi: (Urambo, Sofi, Singida, Same, Nzovw, Nzega, Njombe, Mto wa Mbu, Mwanhala, Mtawanya, Msanginya, Masasi, Mamtukuna, Kiwanda, Kisarawe, Kilosa, Ilula, Ikwiriri, Ifakara, Handeni, Arnatouglu, Bigwa na Bariadi).
  1. Uchomeleaji: (Gera, Ifakara, Karumo, Kisarawe, Kisangwa, Kiwanda, Malya, Mtawanya, Mwanhala, Munguri, Newala, Njombe, Nzovwe, Sikonge, Nzega, Sengerema, Sikonge, Sofi, Ulembwe na Urambo).
  1. Kompyuta: vyuo vyote vinafundisha isipokuwa, (Sofi, Sikonge, Same, Newala, Nandembo, Munguri, Mto wa Mbu, Musoma, Mtawanya, Msingi, Msanginya, Muhukuru, Masasi, Mamtukuna, Kiwanda, Kisangwa, Kisarawe, Ifakara, Handeni, Gera, Chilala na Arnatouglo).
  1. Kilimo na Ufugaji: (Chisalu, Gera, Kiwanda, Handeni, Ifakara, Ikwiriri, Kilosa, Kilwa Masoko, Kisangwa, Mamtukuna, Malampaka, Mamtukuna Malampaka, Malya, Muhukuru, Msanginya, Msingi, Mwanhala, Njombe, Nzovwe, Same, Singida, Bigwa, Tango, Urambo).
  1.  Utunzaji wa watoto (Day care): (Nzovwe, Bigwa, Mtawanya, Msingi, Mtawanya, Msinga, Masasi, Katumba, Chisalu).
  1. Elimu haina mwisho (Sekondari nje ya mfumo rasmi kwa wasichana tu): (Chilala, Ilula, Karumo, Katumba, Malya, Masasi, Muhukuru, Msanginya, Msinga, Msingi, Mtawanya, Mwanva, Mputa, Mto wa Mbu, Ngara, Njombe, Nzega, Nzovwe, Bigwa, Rubondo, Sengerema).
  1. Mpira fursa kwa Wanafunzi wa kike tu: (Sengerema, Nzovwe, Mputa, Masasi, Katumba, Bigwa na Nzega).
  1. Uongozaji Watalii: (Kilwa Masoko, na Ngara).
  1. Udereva: (Tarime, Kiwanda, Tango, Sofi, Sikonge, Rubodo, Nzega, Malya, Kilwa Masoko, Ikwiriri, Chala).
  1. Ufundi Bomba: (Kiwanda).

2. MAFUNZO MAALUM
    Muda hulingana na Mahitaji ya Wahusika
                i.                 Elimu ya Sekondari Nje ya Mfumo Rasmi (Elimu haina Mwisho)
              ii.                  Utunzaji wa Watoto Wadogo (Day Care)
            iii.Mpira fursa (Michezo)

3. MAFUNZO YA MUDA MFUPI
Mafunzo haya hutolewa kwa wananchi mbalimbali sambamba na vikundi mbalimbali kulingana na mahitaji yao.

Aidha, pamoja na mafunzo haya yaliyoainishwa hapo juu, washiriki watajifunza masomo yafuatayo ya Uelewa kulingana na mahitaji ya wahusika. Masomo hayo ni pamoja na: Kiingereza, Uraia, Uchumi, Hifadhi ya Mazingira, Ujasiriamali na Afya ya Jamii.

GHARAMA YA WASHIRIKI
Gharama kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi na Mafunzo Maalum kwa mwanachuo wa Bweni na Kutwa malipo ni kama ifuatavyo:-
a)     Gharama kwa Wanachuo wa Bweni ni shs. 250,000/=

    1. Ada ya Mafunzo                     -TShs.  100,000/=
    2. Gharama nyingine                   -TShs. 150,000/=
Jumla                                        TShs. 250,000/=

NB: Gharama nyingine inajumuisha:

i)   Kitambulisho                                  -TShs      5,000/=
ii)  Fedha ya ukarabati             -TShs.   25,000/=
iii) T-shirt (sare)                      - TShs.   15,000/=
iv) Godoro                               - TShs.     5,000/=
v)  Vifaa vya mafunzo             - TShs    100,000/=


b)    Gharama kwa Wanachuo wa Kutwa ni shs. 245,000/=;

a)     Ada ya Mafunzo                 -TShs.  100, 000/=
b)    Gharama nyingine              -TShs.  145,000
       Jumla                                     -TShs- 245,000/=

NB: Gharama nyingine inajumuisha:

i)   Kitambulisho                    - TShs    5,000/=
ii)  Fedha ya ukarabati            -TShs.  25,000/=
iii) T-shirt (sare)                     - TShs. 15,000/=
iv) Vifaa vya mafunzo           - TShs 100,000/=
                                   - TShs 145,000/=

c)                       Kwa mafunzo ya Muda Mfupi ni Tshs 20,000/= kwa mshiriki kwa mwezi.

N.B - Ada kiasi cha Tshs. 100,000/- ilipwe kwenye mfumo wa Serikali na mwanafunzi atalazimika kupata Namba ya Malipo (Control Number) toka chuoni ili afanye malipo na gharama nyingine zilipwe kwenye akaunti ya Chuo na zitakatiwa risiti ya Chuo.  Ada inaweza kulipwa kwa awamu mbili (2) tu.

Imetolewa na:


KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Jumatatu, 20 Januari 2020

MKUTANO WA KIMATAIFA WA ELIMU JIJINI LONDON UINGEREZA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako na baadhi ya wataalamu wa elimu kutoka Tanzania  wakiwemo kutoka  Washirika wa Maendeleo kutoka "DFID" Tanzania na British Council Tanzania wanashiriki Mkutano wa Kimataifa wa Elimu jijini London, Uingereza ambapo ajenda kuu ya mkutano huo ni nini kifanyike kuboresha Elimu ndani ya kizazi kimoja "One Generation."


Mkutano huo unawaleta pamoja Mawaziri wenye dhamana ya Elimu na wataalamu katika Sekta ya Elimu kutoka nchi 120 ambapo pia watajadili kuhusu mfumo sahihi wa upimaji uelewa wa wanafunzi na iwapo matokeo ya mwanafunzi yanatokana na mwanafunzi mwenyewe, Mfumo, Walimu au Mitaala.


Mengine yatakayojadiliwa katika Mkutano huo ni pamoja na uboreshaji Mazingira  ya utoaji elimu kwa ajili ujifunzaji, uboreshaji Elimu jumuishi, uimarishaji Elimu ya Ufundi katika kuongeza Vijana wenye ujuzi, umuhimu wa vipaumbele vya elimu katika ngazi zote za elimu  kuwiana, maendeleo ya Teknolojia  yanavyochagiza na kutumika katika ujifunzaji na ufundishaji, umuhimu wa  kuwa na takwimu sahihi za Kitaifa za Sekta na pia umuhimu wa uwekezaji katika elimu ya awali katika ujifunzaji.