Jumamosi, 13 Juni 2020

WATUMISHI WIZARA YA ELIMU WAPATIWA MAFUNZO JUU YA MAGONJWA SUGU

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa James Mdoe amesema afya ya mtumishi ni nguzo kubwa na muhimu ya uendeshaji wa shughuli za taasisi yeyote. 

Akizungumza Jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi wa Wizara hiyo kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU), Ukimwi na Magonjwa Sugu yasiyoambukizwa, Profesa Mdoe amesema watumishi wasipopewa mafunzo ya uelewa juu ya magonjwa hayo kuna uwezekano wa Taifa kupoteza nguvu kazi. 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa James Mdoe akiongea na watumishi wa Wizara ya Elimu kabla ya kuanza mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU), Ukimwi na Magonjwa Sugu yasiyoambukizwa.

Naibu Katibu Mkuu Mdoe amesema magonjwa hayo yanaweza kupoteza maisha ya watumishi ama kusababisha utendaji kazi wa watumishi kushuka kutokana na kuugua mara kwa mara na kuwa na afya dhoofu. 

“Watumishi ni muhimu katika taasisi yoyote, hivyo afya zao ni muhimu sana kwa taasisi. Katika utumishi wa umma kuna miongozo iliyotolewa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma na Utawala Bora ambayo inaelekeza namna bora ya kutoa huduma kwa watumishi,” amesema Naibu Katibu Mkuu. 

Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU), Ukimwi na Magonjwa Sugu yasiyoambukizwa.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Moshi Kabengwe akiongea na watumishi wa Wizara ya Elimu kabla ya kuanza mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU), Ukimwi na Magonjwa Sugu yasiyoambukizwa 

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Moshi Kabengwe akizungumza katika mafunzo hayo amesema Wizara imeamua kutoa mafunzo hayo ili kuwawezesha watumishi kupata uelewa na mbinu za kukabiliana na magonjwa hayo.

Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Elimu wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uelewa kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU), Ukimwi na Magonjwa Sugu yasiyoambukizwa.

Ijumaa, 22 Mei 2020

WAZIRI NDALICHAKO ATANGAZA TAREHE ZA MITIHANI KWA KIDATO CHA SITA NA VYUO VYA UALIMU

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako amezitaka  shule zote zenye wanafunzi wa kidato cha sita kuanza maandalizi ya kupokea wanafunzi hao ili waanze masomo Juni 1 2020 kama ilivyoelekezwa.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo Jijini Dodoma wakati alipoongea na waandishi wa habari ambapo amesema ni vizuri kwa shule za bweni zikaanza kupokea wanafunzi hao Mei 30, 2020 ili waanze masomo katika muda uliopangwa.
 
Amesema wakati shule za bweni zikipokea wanafunzi Mei 30, 2020 shule za kutwa nazo zianze maandalizi huku akilitaka Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) kusambaza ratiba za mtihani mapema kwa ajili ya maandalizi.

"Mitihani ya Kidato cha sita na Vyuo vya Ualimu inaanza Juni 29, 2020 na kukamilika Julai 16, 2020 hivyo NECTA sambazeni ratiba za mtihani mapema ili shule  na vyuo vianze maandalizi na kumbukeni mtapaswa kutoa  matokeo ya mtihani huo kabla ya Agosti 30, 2020,"alisema Wziri Ndalichako.

Kwa upande wa Vyuo vikuu na Vyuo vya Kati waziri   Ndalichako ameyataka mabaraza pamoja na Seneti ya Vyuo kupanga ratiba za masomo kwa lengo la kufidia muda wa masomo ambao wanafunzi wamepoteza wakiwa nyumbani na kuwasilisha ratiba hizo Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania(TCU) ili mwaka huu wa masomo ukamilike bila kuathiri ratiba za masomo kwa nwakali 2020/2021

Pia amevitaka vyuo hivyo kuwasilisha nyaraka muhimu zinazohitajika Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu ili Mikopo kwa wanafunzi na ada zao ziweze kutolewa mapema kwa kuwa tayari Serikali imeshatoa jumla ya sh Bilioni 122.8  kwa ajili hiyo.

Itakumbukwa kwamba Mei 21 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati akihutubia wananchi kupitia Vyombo vya habari alitangaza kufungua vyuo vya elimu ya Juu, Kati na Masomo kwa wanafunzi wa kidato cha sita.

WAZIRI NDALICHAKO ATANGAZA TAREHE ZA MITIHANI KWA KIDATO CHA SITA NA VYU...

Jumatano, 13 Mei 2020

TAARIFA KWA UMMA

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY


STUDY OPPORTUNITIES TENABLE AT THE HELWAN UNIVERSITY IN THE ARAB REPUBLIC OF EGYPT FOR 2020/2021 ACADEMIC YEAR

1.0  Call for Application

The general public is hereby informed that, Helwan University has granted scholarship opportunities to eligible Tanzanian nationals to pursue Undergraduate and Postgraduate studies for the academic year 2020/2021.

 

2.0  Application Requirements

Applicants should submit the following documents in PDF form;

1.      A recommendation letter;

2.      A statement of purpose describing reasons for selecting the relevant program;

3.      Certified photocopies of academic certificates, transcripts and birth certificate;

4.      A certificate of English Language Proficiency;

5.      A detailed Curriculum Vitae;

6.      A copy of the information page of the passport; and

7.  Applicants for Masters and Doctorate degrees should include their research proposal.

NB: Incomplete application forms and application documents will not be considered.

For details on application procedures, an application form and required application documents visit:

http://www.helwan.edu.eg/InternationalStudents/wp-content/uploads/2013/01/HU-IASSP-2020.pdf

 

3.0  Scholarship Coverage

This is a partial scholarship which covers only tuition fee. It does NOT cover accommodation expenses, monthly stipend, travel expenses, healthcare or any category of insurance, stationery or visa costs.  

 

4.0  Submission

A filled application form and the corresponding application documents should be submitted to the following email: hisb-scholarships@hq.helwan.edu.eg not later than 31th May, 2020.

 

Issued by

Permanent Secretary,

Ministry of Education, Science and Technology,

Government City,

Mtumba Area,

Afya Street,

P. O. Box 10,

40479 DODOMA.