Alhamisi, 17 Mei 2018

KKK IMEONDOA WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA


·   EP4R IMEONDOA ADHA YA VYOO ILIYOKUWA INAIKABILI SHULE YAMBAWALA 

Mkuu wa shule ya Ufundi Mtwara Paul Kaji amepongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo na hivyo kuondoa kabisa changamoto mbalimbali zilizoKuwa kikwazo kwa wanafunzi na walimu shuleni hapo.

Kaji ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na timu ya wanahabari waliofika shuleni hapo kwa lengo la kuangalia ukarabati wa miundombinu ya shule hiyo ambapo zaidi ya bilioni moja imetumika kukarabati vyumba vya madarsa, ofisi za walimu, mabweni, Bwalo la chakula, sehemu za kuandalia chakula (majiko), kukarabati njia Maalumu za wanafunzi wenye ulemavu, kurejesha miundombinu ya umeme na Maji katika hali ya kawaida.

Pia baadhi ya wanafunzi waliohojiwa wameelezea kufurahishwa na ukarabati huo na hivyo kuwafanya kuwa katika mazingira mazuri ya kusomea.
“Tunaishukuru Serikali kwa kutuboreshea miundombinu ya shule siyo tu shule yetu imependeza bali hata sisi tuna uwezo wa kusoma muda wowote kwa kuwa umeme upo, tunawasilisha shukrani na hivyo tunaahidi tutasoma kwa bidii ili tufaulu vizuri” anasema David Andrew mmoja wa wanafunzi wa kidato cha pili katika shule hiyo ambaye anasomea fani ya ujenzi.

Muonekano wa darasa linaloongea KKK katika Shule ya Msingi Msijute iliyopo Mkoani Mtwara


Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mbawala Ali Haroun amesema licha ya kujenga madarasa mapya lakini jambo ambalo limeleta heshima kwao ni ujenzi wa matundu ya vyoo.

Alisema katika fedha hizo wamejenga matundu ya vyoo 10 na kufanya jumla ya matundu ya vyoo kuwa 16 na madarasa 8 jambo ambalo limesaidia kuongeza wanafunzi na kila darasa kukaa wanafunzi kulingana na ukubwa wa darasa.
Hata hivyo aliongeza kuwa matundu ya vyoo yamewasaidia katika kuhakikisha walimu wanakaa shuleni muda wote kuliko hapo zamani ambapo ilikuwa ni lazima kwenda kujisaidia majumbani kwao.

‘’Hapo awali kulikuwa na shida kabisa kwani walimu walikuwa wanafika shuleni wakijisikia kubanwa na haja wanakimbilia nyumbani na kuwafanya kuchukua muda mwingi hadi wa vipindi ndipo wanarejea shuleni kwa ajili ya kuendelea na masomo,’’

‘’ Programu hii ni mkombozi kwetu kwani hata wanafunzi waliokuwa wakikaa katika madarasa kwa kubebana sasa wanakaa kwa nafasi na mpaka chumba kimoja kimebaki kwa kukosa wanafunzi,’’aliongeza mwalimu Ally.
Mwalimu wa darasa la awali katika Shule ya Msingi Msijute Mariamu Milanzi akifundisha kwa kutumia zana zilizowekwa katika darasa darasa la awali. Matumizi ya Zana za kufundishia unasaidia watoto kuelewa kwa urahisi kupenda shule na kupunguza utoro.

Naye mwalimu, Isabela Mwambona alisema mradi huo umewarahisishia kazi kutokana na kufundisha kwa nafasi na hata kuwafikia wanafunzi  mmoja baada ya mwingine kwa ufundishaji.

Katika hatua nyingine programu ya Kusoma, Kuandika na  Kuhesabu (KKK) imezaa matunda katika shule mbalimbali za Mkoa wa Lindi na Mtwara.
Isabela alisema tangu wapeate mafunzo ya ufundishaji wa KKK kwa kutumia vitendo na michoro kwa sasa wamefanikiwa kupunguza idadi ya wasiojua Kusoma na Kuandika shuleni hapo.
Wanafunzi wa Darasa la Awali katika shule ya Msingi Msijute wakiwa darasani tayari kwa kuanza masomo. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni