Ijumaa, 4 Novemba 2016

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yakabidhiwa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Mkinga akimkabidhi  Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish  baadhi ya nyaraka mbalimbali zinazohusu Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ambavyo sasa vitakuwa vikiendeshwa na kusimamiwa  na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na anayeshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Saimon Msanjila.


Katibu Mkuu Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akizungumza na watendaji wa Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia na Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  wakati wa  makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa wizara.



Makatibu wakuu wa Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa wizara hizo  mara baada ya makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii.

Alhamisi, 3 Novemba 2016

Wizara yakabidhi ramani ya michoro ya shule ya sekondari Nyakato


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akiwa ameshika ramani ya michoro inayokwenda kujengwa katika shule ya sekondari Nyakato iliyopo Mkoani Kagera. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Bukoba Vijijini Mwantumu Dau na Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mansoor induries Ltd Sharif Hirani ambaye yeye pamoja na wadau wengine wamejitolea kusaidia kukarabati baadhi ya miundombinu ya shule hiyo.  Shule hiyo  ni miongoni mwa shule ambazo ziliharibiwa na tetemeko


Mkurugenzi Mkuu Wakala wa Majengo Tanzania Elius Mwakibinga akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish ramani ya michoro inayokwenda kujengwa katika shule ya sekondari Nyakato iliyopo Mkoani Kagera, huku Mkurugenzi Mkuu wa Mansoor induries Ltd Sharif Hirani akishuhudia. Shule hiyo  ni miongoni mwa shule ambazo ziliharibiwa na tetemeko



  Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akimkabidhi Mkurugenzi wa Bukoba Vijijini Mwantumu Dau ramani ya michoro inayokwenda kujengwa katika shule ya sekondari Nyakato iliyopo Mkoani Kagera. Shule hiyo  ni miongoni mwa shule ambazo ziliharibiwa na tetemeko



Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Mansoor induries Ltd Sharif Hirani ramani ya michoro inayokwenda kujengwa katika shule ya sekondari Nyakato iliyopo Mkoani Kagera. Shule hiyo  ni miongoni mwa shule ambazo ziliharibiwa na tetemeko