Alhamisi, 8 Septemba 2016

Kaimu Kamisha Afungua Maadhimisho ya Siku ya Kisoma Duniani



Kaimu Kamishna wa Elimu, Nicholaus  Bureta akifungua   maadhimisho  ya siku ya Kisomo Duniani (International Literacy Day)Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish, katika ukumbi wa makumbusho ya Taifa. Maadhimisho haya yalienda sambamba na ufunguzi wa ripoti ya Kimataifa ya Ufuatiliaji wa Elimu.
 



Mwakilishi wa UNESCO nchini Bi.Zulmira Rodriguez akimkabidhi Kaimu kamishna wa Elimu ripoti ya Kimataifa ya Ufuatiliaji wa Elimu wakati wa maadhimisho ya siku ya kisomo duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa.
 




Kaimu Kamishna wa Elimu Nicholaus Bureta akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa  wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, mashirika ya Kimataifa ya maendeleo pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali wakionyesha ripoti ya Kimataifa ya Ufuatiliaji wa Elimu mara baada ya uzinduzi wake rasmi. Kushoto mwanzoni ni Mwakilishi wa UNESCO nchini Bi.Zulmira Rodriguez.


Kaimu Kamishna wa Elimu Nicholaus Bureta akiwakabidhi ripoti ya Kimataifa ya Ufuatiliaji wa Elimu baadhi ya walimu wakuu wa shule za Msingi nchini mara baada ya uzinduzi rasmi wa ripoti hiyo wakati wa maadhimisho ya siku ya kisomo duniani yaliyofanyika  katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa.

Jumatano, 7 Septemba 2016

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia afungua Kikao cha Maandalizi ya Makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya jamii

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarishi akifungua kikao cha maandalizi ya makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga

Ofisa wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, akisoma historia fupi ya vyuo vya maendeleo ya jamii wakati wa kikao cha maandalizi ya makabidhiano ya vyuo hivyo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.


Katibu Mkuu wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akimfafanulia jambo Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarishi kwenye kikao cha maandalizi ya makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Jumanne, 6 Septemba 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dr. John Pombe Maghufuli afanya ziara kukagua ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo ya awali kutoka kwa Profesa Florens Luoga (Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma) kuhusu ujenzi wa mabweni ya chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati alipotembelea eneo la mradi huu muda mfupi kabla ya Rais kuwasili.Kushoto ni Katibu Mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish.



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Magufuli wakati alipotembelea Mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).





Katibu Mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish akisalimiana na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli wakati alipotembelea Mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
 


 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli  akipata maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa TBA Aktecti (Arch) Elius A.. Mwakalinga kuhusu mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Mradi huo chuoni hapo. Kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako.
 










Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli akikagua mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Mradi huo. Kushoto ni Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako.





 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako akimshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli  kwa uamuzi wa kujenga mabweni katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni hatua katika kuleta ubora wa elimu.


  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Magufuli akizungumza na wanajumuiya ya Chuo Kikuu pamoja na Wafanyakazi wa Mradi huo mara baada ya kufanya ukaguzi wa ujenzi wa mabweni hayo.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr.John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.  Profesa Joyce Ndalichako na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.