Ijumaa, 4 Mei 2018


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Anuani ya simu “ELIMU”
Simu: 026  296 35 33
Baruapepe:  info@moe.go.tz
Tovuti: www.moe.go.tz




  
Chuo cha Masomo ya  Biashara na Sheria,
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Jengo Na. 10,
S. L. P. 10,
40479 DODOMA          

Tarehe:  4 Mei, 2018

TAARIFA KWA UMMA
Kumekuwa na taarifa za upotoshaji ambazo zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii, ambazo zinaonesha dosari na makosa katika vitabu. Mojawapo ni picha inayoelezea viungo vya mwili wa mwanadamu na nyingine iko katika Kitabu cha Kiingereza chenye maneno yanayosomeka “The Big City of Tanzania”.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa kitabu kinachosambazwa kinachoelezea viungo vya mwili wa mwanadamu si chapisho la Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na wala si miongoni mwa vitabu ambavyo vimesambazwa kwenye shule. Kitabu hicho hakina uhusiano wowote na wala hakifanani na vitabu ambavyo vimechapishwa hivi karibuni na TET.
Aidha, kuhusu kitabu cha Kiingereza, hilo ni chapisho la mwaka 2016 ambalo limefanyiwa marekebisho katika chapisho la mwaka 2018.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inawasihi watanzania kupuuza taarifa hizo ambazo siyo za kweli na zina nia ya kupotosha na kuleta usumbufu kwa jamii. Wizara pia inatumia fursa hii kuwakumbusha wananchi kuzingatia Sheria za Matumizi ya Mitandao na kutambua kuwa kutoa taarifa za uongo ni kosa la jinai.
                                                  Imetolewa na:      
Mwasu Sware
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
04/05/2018

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni