Jumanne, 21 Januari 2020

TANGAZO LA KUJIUNGA NA VYUO VYA MAENDELEO YA WANANCHI


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatangaza nafasi za kujiunga katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) kwa mwaka 2020.
Sifa za Mwombaji ni mwananchi yeyote mwenye nia ya kupata ujuzi na maarifa mbalimbali.
Aina ya Mafunzo yanayotolewa ni:
1. MAFUNZO YA UFUNDI STADI- NGAZI YA I, II &III
  1. Ufundi Umeme wa Magari : (Ifakara, Katumba, Nzovwe, Rubondo, Same, Sofi, Kisangwa, Mto wa Mbu,Chala,Handeni, Ikwiriri, Karumo, Kilosa, Katumba, Kibondo, Kilwa Masoko, Kihiga, Mamtukuna, Malampaka, Kiwanda,Malya).
  1. Ufundi Mekanika, (Vyuo vyote vinavyofundisha Ufundi Magari).
  1. Ufundi Umeme wa Majumbani, (Vyuo vyote vinafundisha kozi hii).
  1. Ufundi  Magari : (Bigwa, Chala, Chilala, Handeni, Ifakara, Ikwiririri, Karumo, Kilosa, Kisarawe, Katumba, Kibondo, Kilwa Masoko, Kisangwa, Kihinga, Singida Mamtukuna, Malampaka, Malya, Masasi, Mbinga, Msinga, Mtawanya, Musoma, Mwanhala, Mwanva, Mto wa Mbu, Munguri, Nandembo, Newala, Ngara, Njombe, Nzega, Nzovwe, Rubondo, Same, Sengerema, Sofi, Urambo).
  1. Useremala: (Bariadi, Mtawanya, Chala, Chilala, Chisala, Handeni, Ifakara, Ilula, Ulembwe, Kiwanda).
  1. Uashi: (Vyuo vyote vinavyofundisha Uashi isipokuwa Mtowambu, Nzega, Ikwiriri, Buhangija, Kiwanda, Chilala, Bigwa na Sikonge).
  1. Ushonaji: (Vyuo vyote vinafundisha ushonaji isipokuwa, Arnatouglu, Handeni, Sofi).
  1. Upishi: (Urambo, Sofi, Singida, Same, Nzovw, Nzega, Njombe, Mto wa Mbu, Mwanhala, Mtawanya, Msanginya, Masasi, Mamtukuna, Kiwanda, Kisarawe, Kilosa, Ilula, Ikwiriri, Ifakara, Handeni, Arnatouglu, Bigwa na Bariadi).
  1. Uchomeleaji: (Gera, Ifakara, Karumo, Kisarawe, Kisangwa, Kiwanda, Malya, Mtawanya, Mwanhala, Munguri, Newala, Njombe, Nzovwe, Sikonge, Nzega, Sengerema, Sikonge, Sofi, Ulembwe na Urambo).
  1. Kompyuta: vyuo vyote vinafundisha isipokuwa, (Sofi, Sikonge, Same, Newala, Nandembo, Munguri, Mto wa Mbu, Musoma, Mtawanya, Msingi, Msanginya, Muhukuru, Masasi, Mamtukuna, Kiwanda, Kisangwa, Kisarawe, Ifakara, Handeni, Gera, Chilala na Arnatouglo).
  1. Kilimo na Ufugaji: (Chisalu, Gera, Kiwanda, Handeni, Ifakara, Ikwiriri, Kilosa, Kilwa Masoko, Kisangwa, Mamtukuna, Malampaka, Mamtukuna Malampaka, Malya, Muhukuru, Msanginya, Msingi, Mwanhala, Njombe, Nzovwe, Same, Singida, Bigwa, Tango, Urambo).
  1.  Utunzaji wa watoto (Day care): (Nzovwe, Bigwa, Mtawanya, Msingi, Mtawanya, Msinga, Masasi, Katumba, Chisalu).
  1. Elimu haina mwisho (Sekondari nje ya mfumo rasmi kwa wasichana tu): (Chilala, Ilula, Karumo, Katumba, Malya, Masasi, Muhukuru, Msanginya, Msinga, Msingi, Mtawanya, Mwanva, Mputa, Mto wa Mbu, Ngara, Njombe, Nzega, Nzovwe, Bigwa, Rubondo, Sengerema).
  1. Mpira fursa kwa Wanafunzi wa kike tu: (Sengerema, Nzovwe, Mputa, Masasi, Katumba, Bigwa na Nzega).
  1. Uongozaji Watalii: (Kilwa Masoko, na Ngara).
  1. Udereva: (Tarime, Kiwanda, Tango, Sofi, Sikonge, Rubodo, Nzega, Malya, Kilwa Masoko, Ikwiriri, Chala).
  1. Ufundi Bomba: (Kiwanda).

2. MAFUNZO MAALUM
    Muda hulingana na Mahitaji ya Wahusika
                i.                 Elimu ya Sekondari Nje ya Mfumo Rasmi (Elimu haina Mwisho)
              ii.                  Utunzaji wa Watoto Wadogo (Day Care)
            iii.Mpira fursa (Michezo)

3. MAFUNZO YA MUDA MFUPI
Mafunzo haya hutolewa kwa wananchi mbalimbali sambamba na vikundi mbalimbali kulingana na mahitaji yao.

Aidha, pamoja na mafunzo haya yaliyoainishwa hapo juu, washiriki watajifunza masomo yafuatayo ya Uelewa kulingana na mahitaji ya wahusika. Masomo hayo ni pamoja na: Kiingereza, Uraia, Uchumi, Hifadhi ya Mazingira, Ujasiriamali na Afya ya Jamii.

GHARAMA YA WASHIRIKI
Gharama kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi na Mafunzo Maalum kwa mwanachuo wa Bweni na Kutwa malipo ni kama ifuatavyo:-
a)     Gharama kwa Wanachuo wa Bweni ni shs. 250,000/=

    1. Ada ya Mafunzo                     -TShs.  100,000/=
    2. Gharama nyingine                   -TShs. 150,000/=
Jumla                                        TShs. 250,000/=

NB: Gharama nyingine inajumuisha:

i)   Kitambulisho                                  -TShs      5,000/=
ii)  Fedha ya ukarabati             -TShs.   25,000/=
iii) T-shirt (sare)                      - TShs.   15,000/=
iv) Godoro                               - TShs.     5,000/=
v)  Vifaa vya mafunzo             - TShs    100,000/=


b)    Gharama kwa Wanachuo wa Kutwa ni shs. 245,000/=;

a)     Ada ya Mafunzo                 -TShs.  100, 000/=
b)    Gharama nyingine              -TShs.  145,000
       Jumla                                     -TShs- 245,000/=

NB: Gharama nyingine inajumuisha:

i)   Kitambulisho                    - TShs    5,000/=
ii)  Fedha ya ukarabati            -TShs.  25,000/=
iii) T-shirt (sare)                     - TShs. 15,000/=
iv) Vifaa vya mafunzo           - TShs 100,000/=
                                   - TShs 145,000/=

c)                       Kwa mafunzo ya Muda Mfupi ni Tshs 20,000/= kwa mshiriki kwa mwezi.

N.B - Ada kiasi cha Tshs. 100,000/- ilipwe kwenye mfumo wa Serikali na mwanafunzi atalazimika kupata Namba ya Malipo (Control Number) toka chuoni ili afanye malipo na gharama nyingine zilipwe kwenye akaunti ya Chuo na zitakatiwa risiti ya Chuo.  Ada inaweza kulipwa kwa awamu mbili (2) tu.

Imetolewa na:


KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Maoni 2 :

  1. I was reading your article and wondered if you had considered creating an ebook on this subject. Your writing would sell it fast. You have a lot of writing talent. خبير سيو

    مسك كلمات في جوجل

    خبير سيو
    محترف سيو
    خدمات سيو
    حجر هاشمي
    رأفت ربيع

    JibuFuta
  2. Nina D2 na C1 naeza jiunga na chuo

    JibuFuta