Jumatatu, 20 Januari 2020

MKUTANO WA KIMATAIFA WA ELIMU JIJINI LONDON UINGEREZA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako na baadhi ya wataalamu wa elimu kutoka Tanzania  wakiwemo kutoka  Washirika wa Maendeleo kutoka "DFID" Tanzania na British Council Tanzania wanashiriki Mkutano wa Kimataifa wa Elimu jijini London, Uingereza ambapo ajenda kuu ya mkutano huo ni nini kifanyike kuboresha Elimu ndani ya kizazi kimoja "One Generation."


Mkutano huo unawaleta pamoja Mawaziri wenye dhamana ya Elimu na wataalamu katika Sekta ya Elimu kutoka nchi 120 ambapo pia watajadili kuhusu mfumo sahihi wa upimaji uelewa wa wanafunzi na iwapo matokeo ya mwanafunzi yanatokana na mwanafunzi mwenyewe, Mfumo, Walimu au Mitaala.


Mengine yatakayojadiliwa katika Mkutano huo ni pamoja na uboreshaji Mazingira  ya utoaji elimu kwa ajili ujifunzaji, uboreshaji Elimu jumuishi, uimarishaji Elimu ya Ufundi katika kuongeza Vijana wenye ujuzi, umuhimu wa vipaumbele vya elimu katika ngazi zote za elimu  kuwiana, maendeleo ya Teknolojia  yanavyochagiza na kutumika katika ujifunzaji na ufundishaji, umuhimu wa  kuwa na takwimu sahihi za Kitaifa za Sekta na pia umuhimu wa uwekezaji katika elimu ya awali katika ujifunzaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni