Jumatano, 6 Novemba 2019

WAZIRI NDALICHAKO AKUTANA NA MKUU MPYA WA ELIMU KUTOKA UNICEF



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako leo Novemba 6, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Elimu Tanzania kutoka Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Tanzania, Dkt. Daniel Baheta.

Dkt. Baheta amefika katika ofisi za Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia zilizopo Jijini Dodoma kwa lengo la kujitambulisha  baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo ambapo amemweleza waziri kuwa UNICEF inatekeleza vipaumbele vitatu katika sekta ya elimu.

Mkuu huyo amevitaja vipambele vya Kimataifa vya UNICEF kuwa ni kuwa ni ubora katika utoaji elimu na ujifunzaji, elimu kwa  vijana, ajira  na kutatua changamoto ya mdondoko wa wanafunzi katika shule.

Waziri Nadlichako amesema angependa kuona UNICEF ikishirikiana zaidi na Serikali  katika kuimarisha mafunzo ya stadi za maisha ambazo zitawawezesha wanafunzi wa kike kukwepa vishawishi vinavyosababisha mdondoko shuleni na ukuzaji wa ushirikishwaji jamii katika kusimamia ubora wa elimu na wanafunzi.

Katika mazungumzo yao wamekubaliana kutekeleza programu   ambazo ni pamoja na kuanzisha mfumo wa kidigitali wa kusimamia mahudhurio ya wanafunzi na kuwezesha mawasiliano kati ya Taasisi za elimu  na wazazi.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako awakiangalia kishikwambi pamoja na wageni kutoka UNICEF

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na Mkuu wa Elimu kutoka UNICEF Tanzania Dkt. Daniel Bahate (Mwenye suti ya bluu) aliyefika ofisi kwake leo jijini Dodoma kwa lengo la kujitambulisha. 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na Dkt Daniel Bahate (kushoto) Mkuu wa Elimu kutoka UNICEF Tanzania.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni